Baadhi vipimo vya kuzingatia unapojenga nyumba

Baadhi vipimo vya kuzingatia unapojenga nyumba

stabilityman

JF-Expert Member
Joined
Jul 9, 2024
Posts
811
Reaction score
1,753
*Urefu wa nyumba wakati wa ujenzi - Orodha:



vipimo vyako visipungue hivyo

nimeandika kwa experience yangu



1. Sebule - 4m x 5m au 4.5m x 5m

2. Chumba master - 4m x 4m au 4m x 3.5m

3. Vyumba vya kawaida - 3m x 3.5m. Chini ya 3m x 3m kinabana

4. Jiko - 3m x 4m

5. Bafu/Choo - 1.8m x 2.5m

6. Ukumbi - Upana 1.2m hadi 1.5m

7. Urefu wa kuta - 3m hadi 3.5m kutoka sakafu. Chini ya 2.8m epuka

8. Mapigo ya paa - Isipungue 30cm ili mvua isigonge ukuta

9. Mwinuko wa paa - Nyuzi 20-25 kwa bati

10. Urefu wa bati - Tumia 3m au 3.6m lifike bila kuunganisha katikati

11. Mlango - Upana 90cm, urefu 2.1m

12. Setback - Acha 1.5m pembeni, 3m mbele na nyuma kutoka mpaka wa kiwanja

13. Nyumba ya vyumba 2 - Urefu jumla 8m - 10m

14. Nyumba ya vyumba 3 - Urefu jumla 10m - 14m

15. Nyumba ya vyumba 4 - Urefu jumla 14m - 18m





kama unataka kuchorewa raman ya nyumba na ujenzi 0 7 4 3 2 5 7 6 6 9
 
Jielemishe zaidi kwenye hiyo namba 7. Hiyo 'epuka chini ya 2.8m' sio sawa maeneo ya baridi.
 
Safi sana, kwa nyumba ya chumba kimoja master, sebule na jiko. Nikifanya sebule 4.5×4. Bedroom atleast 4×4, jiko 3×2.5, choo 1.5×2.5. Hapo si nitakuwa na nyumba ndogo lakini kubwa?
 
Back
Top Bottom