Baada ya Umeya wa Dar es Salaam na Uchaguzi wa Marudio Zanzibar sioni mbeleni Kick ya UKAWA

Lizaboni

JF-Expert Member
Feb 21, 2013
33,894
20,372
Bila shaka mambo mawili ambayo yalikuwa yanatumiwa na wanaojiita UKAWA ijapokuwa ulishavunjika siku nyingi yamefikia ukingoni. Uchaguzi wa Meya wa Dar es Salaam umefanyika ambapo ISAYA MWITA wa CHADEMA alichaguliwa kuongoza jiji hilo. Shukrani kwa Rais John Pombe Magufuli ambaye aliweka mazingira ya kufanyika kwa uchaguzi huo kwa vile alijua kuwa uchaguzi huo ukifanyika tu UKAWA kwisha habari yao. Hutawasoma mitandaoni, kwenye magazeti wala kuwaona runingani.

Baada ya hapo, kick nyingine ya UKAWA ilikuwa Uchaguzi wa Marudio visiwani Zanzibar. Kabla ya uchaguzi huo, kulikuwa na tambo na majigambo mengi huku wakijiaminisha kuwa Wazanzibari watasusia uchaguzi huo. Tena vitisho vikawa vinatumika kuwatisha watu wasijitokeze kupiga kura. Miongoni mwa vitisho hivyo ni pamoja na kuchoma moto nyumba za wafuasi wa CCM.

Hata hivyo, kwa baraka za Mwenyezi, uchaguzi umefanyika salama salmini na Dr Ali Mohamed Shein akachaguliwa kwa zaidi ya asilimia 91 huku CCM ikizoa viti vyote vya ubunhe baada ya CUF kufanya ujinga ambao wataujutia wa kususia uchaguzi. Kwa sasa kinachosubiriwa ni kwa Dr Shein kuunda serikali ambayo bila shaka itakuwa ni ya upande mmoja. Kikubwa zaidi ni idadi kubwa ya wananchi waliojitokeza kupiga kura. Kati ya watu laki tano waliojiandikisha, zaidi ya laki tatu walipuuza wito wa CUF wa kususia uchaguzi na hivyo walijitokeza kupiga kura.

Baada ya kick hizo kupatiwa ufumbuzi, kwa kweli sioni mbeleni future ya upinzani. Kule Zanzibar najua CUF wameshajifuta wenyewe. Huku Bara hawa CHADEMA hawana jipya tena hasa baada ya kulikoroga kumchagua Katibu Mkuu wa Kichina ambaye hajui A, B, C za siasa za Kibongo.

Niwape pole sana wale wote ambao nafsi zao walizitoa kwa upinzani. CCM ni ile ile iliyoleta ukombozi Msumbiji, Angola, South Africa, Namibia na hata kwa majirani zetu wa kanda ya ziwa. Kama tuliweza kusimamia ukombozi wa nchi hizo, kitatushinda nini kuweka hatamu ya uongozi kwa nchi hii? Lazima Tuheshimiane
 
haya fanya kazi, acha porojo tanzania ni yakwetu wote siasa za upinzani siyo uadui kama tunavyozijenga. Tumeshamaliza uchaguz mkuu matokeo yaliyotokea tuyaheshimu comoooon inakuaje mwanaume mzima unakaa chini na kuanza kutunga mipasho yasiyo na tija kwa taifa
 
Bila shaka mambo mawili ambayo yalikuwa yanatumiwa na wanaojiita UKAWA ijapokuwa ulishavunjika siku nyingi yamefikia ukingoni. Uchaguzi wa Meya wa Dar es Salaam umefanyika ambapo ISAYA MWITA wa CHADEMA alichaguliwa kuongoza jiji hilo. Shukrani kwa Rais John Pombe Magufuli ambaye aliweka mazingira ya kufanyika kwa uchaguzi huo kwa vile alijua kuwa uchaguzi huo ukifanyika tu UKAWA kwisha habari yao. Hutawasoma mitandaoni, kwenye magazeti wala kuwaona runingani.

Baada ya hapo, kick nyingine ya UKAWA ilikuwa Uchaguzi wa Marudio visiwani Zanzibar. Kabla ya uchaguzi huo, kulikuwa na tambo na majigambo mengi huku wakijiaminisha kuwa Wazanzibari watasusia uchaguzi huo. Tena vitisho vikawa vinatumika kuwatisha watu wasijitokeze kupiga kura. Miongoni mwa vitisho hivyo ni pamoja na kuchoma moto nyumba za wafuasi wa CCM.

Hata hivyo, kwa baraka za Mwenyezi, uchaguzi umefanyika salama salmini na Dr Ali Mohamed Shein akachaguliwa kwa zaidi ya asilimia 91 huku CCM ikizoa viti vyote vya ubunhe baada ya CUF kufanya ujinga ambao wataujutia wa kususia uchaguzi. Kwa sasa kinachosubiriwa ni kwa Dr Shein kuunda serikali ambayo bila shaka itakuwa ni ya upande mmoja. Kikubwa zaidi ni idadi kubwa ya wananchi waliojitokeza kupiga kura. Kati ya watu laki tano waliojiandikisha, zaidi ya laki tatu walipuuza wito wa CUF wa kususia uchaguzi na hivyo walijitokeza kupiga kura.

Baada ya kick hizo kupatiwa ufumbuzi, kwa kweli sioni mbeleni future ya upinzani. Kule Zanzibar najua CUF wameshajifuta wenyewe. Huku Bara hawa CHADEMA hawana jipya tena hasa baada ya kulikoroga kumchagua Katibu Mkuu wa Kichina ambaye hajui A, B, C za siasa za Kibongo.

Niwape pole sana wale wote ambao nafsi zao walizitoa kwa upinzani. CCM ni ile ile iliyoleta ukombozi Msumbiji, Angola, South Africa, Namibia na hata kwa majirani zetu wa kanda ya ziwa. Kama tuliweza kusimamia ukombozi wa nchi hizo, kitatushinda nini kuweka hatamu ya uongozi kwa nchi hii? Lazima Tuheshimiane
Jana nimemuona Meya wa manispaa ya kinondoni akihojiwa azam tv katika kipindi kizima,akielezea uongozi wake na manispaa ya kinondoni so far....sasa nadhani uchaguzi wa meya wa jiji ulikua ushafanyika.
 
Ukishavimbiwa pitiku na maboga ya kuchemsha una shida sana wewe kijana.
Hahahahahaaaaaaaaa! Unanitamanisha sana hiyo kitu pitiku. Muda si mrefu wamepita mama zetu wa Kiyao wakinadi,haya jamani nauza majani ya maboga, njegele, matembele, chinese, nk. Yaani inakuwa raha kabisa. Wanawake wa Kiyao hakika wanatusaidia sana hapa mjini
 
Kwa hiyo upinzani tunauonesha tukiwa bungeni ama siyo? Hahahahahaaaaaaa! Lizaboni kaeleza ukweli. Sisi wapinzani tufike mahala tujue kuwa tunafanya siasa za maigizo na matukio

Wewe sio mpinzani, msukule wa lumumba! Tunasubiri bunge tupate mrejesho wa utendaji wa serikali. Sasa unategemea siasa ifanywe wapi? JF au? Narrow minded, period
 
Bila shaka mambo mawili ambayo yalikuwa yanatumiwa na wanaojiita UKAWA ijapokuwa ulishavunjika siku nyingi yamefikia ukingoni. Uchaguzi wa Meya wa Dar es Salaam umefanyika ambapo ISAYA MWITA wa CHADEMA alichaguliwa kuongoza jiji hilo. Shukrani kwa Rais John Pombe Magufuli ambaye aliweka mazingira ya kufanyika kwa uchaguzi huo kwa vile alijua kuwa uchaguzi huo ukifanyika tu UKAWA kwisha habari yao. Hutawasoma mitandaoni, kwenye magazeti wala kuwaona runingani.

Baada ya hapo, kick nyingine ya UKAWA ilikuwa Uchaguzi wa Marudio visiwani Zanzibar. Kabla ya uchaguzi huo, kulikuwa na tambo na majigambo mengi huku wakijiaminisha kuwa Wazanzibari watasusia uchaguzi huo. Tena vitisho vikawa vinatumika kuwatisha watu wasijitokeze kupiga kura. Miongoni mwa vitisho hivyo ni pamoja na kuchoma moto nyumba za wafuasi wa CCM.

Hata hivyo, kwa baraka za Mwenyezi, uchaguzi umefanyika salama salmini na Dr Ali Mohamed Shein akachaguliwa kwa zaidi ya asilimia 91 huku CCM ikizoa viti vyote vya ubunhe baada ya CUF kufanya ujinga ambao wataujutia wa kususia uchaguzi. Kwa sasa kinachosubiriwa ni kwa Dr Shein kuunda serikali ambayo bila shaka itakuwa ni ya upande mmoja. Kikubwa zaidi ni idadi kubwa ya wananchi waliojitokeza kupiga kura. Kati ya watu laki tano waliojiandikisha, zaidi ya laki tatu walipuuza wito wa CUF wa kususia uchaguzi na hivyo walijitokeza kupiga kura.

Baada ya kick hizo kupatiwa ufumbuzi, kwa kweli sioni mbeleni future ya upinzani. Kule Zanzibar najua CUF wameshajifuta wenyewe. Huku Bara hawa CHADEMA hawana jipya tena hasa baada ya kulikoroga kumchagua Katibu Mkuu wa Kichina ambaye hajui A, B, C za siasa za Kibongo.

Niwape pole sana wale wote ambao nafsi zao walizitoa kwa upinzani. CCM ni ile ile iliyoleta ukombozi Msumbiji, Angola, South Africa, Namibia na hata kwa majirani zetu wa kanda ya ziwa. Kama tuliweza kusimamia ukombozi wa nchi hizo, kitatushinda nini kuweka hatamu ya uongozi kwa nchi hii? Lazima Tuheshimiane



umenena mkuu...UKIWA ni ukiwa tu...ni muda wa majonzi na masononeko.... wanaotaka kurudi CCM tayari utaratibu umetolewa wawahi fasta kabla zile kanuni hazijaundwa.....ha ha ha haaaaaa......... wazee wa matukio.... sasa Matukio yamebaki ya Mhe. Rais na Watedaji wake. ...shiiiiiiiiii kimyaaaa
 
Back
Top Bottom