Baada ya tishio la Urusi; Je, Sweden na Finland watajiunga NATO? EU watakubali?

kt the irreplaceable

JF-Expert Member
Oct 12, 2017
2,363
4,851
Wakuu kheri ya pasaka, juzi juzi mkuu wa baraza la usalama la urusi na rais mstaafu Dimitry Medved alionya kua endapo Finland na Sweden watalazimisha kujiunga Nato, basi urusi itakuja na jibu la nguvu sana ili kuleta balansi ya dunia.

Medved alisema watalazimika kupeleka majeshi na mitambo ya nyukilia kwenye mpaka wa Finland, itakumbukwa kua Finland na Russia wanashare mpaka mrefu wa kilomita 1300, umbali wa kutoka dar mpaka Bukoba. Na pia akasisitiza ukraine watapaswa kuishi na mizinga ya nyukilia karibu kitu ambacho hakijawahi kutokea.

Katika hali ya kupigilia "msumari wa moto" Medved alidai pia watapeleka ndege vita zenye uwezo wa kubeba vichwa vya nyukilia, meli pamoja na wanajeshi ikiwemo mitambo ya ardhini ya nyukilia kwenye eneo lake la KALININGRAD lililopo kati kati ya Poland na lithunia. Wakifanya hivyo ina maana ulaya magharibi itakua na tishio la moja kwa moja la nyukilia kutoka Urusi. Swali ni je Ulaya itakubali hali hii kwa exchange ya Sweden na Finland kujiunga Nato?

Historia inatueleza bayana Russia alishawahi kua na mgogoro mkubwa wa kinyukilia na US mwaka 1960s, pale alipojenga mitambo ya nyukilia cuba pamoja na kusogeza nyambizi za nyukilia karibu kabisa na Marekani. Itakumbukwa kua mgogoro huu ulikua mkubwa sana tena sana mpaka wakafikia tamati ya mezani kupitia mkataba wa amani wa "CAMP DAVID PEACE ACCORDS "

Kwa jicho lako la kiuchambuzi na sio ushabiki, unadhani Finland na Sweden watakubaliwa Nato? Amani ya Dunia itakua kwenye hali gani ikiwa makombora ya nyukilia yakianza kuwekwa mipakani mwa nchi hasimu?

Nb: hapa chini nimeweka ramani ya ulaya, kuonesha eneo la urusi la KALININGRAD lililopo kati kati ya poland na lithunia karibu kabisa na Baltic sea. TUJADILI
The irreplaceable
Screenshot_20220418-135818_Chrome.jpg
 
Inaonekana huu mgogoro hautakwisha mapema coz hakuna upande unaotaka kuonekana ni DHAIFU dhidi ya mwingine

Pia naona Kama usalama wa ulaya unaingizwa mkenge na USA
Mambo bado yapo Moto ..... tuendelee kuhubiri

Labda ni wakati wa AFRICA KUWA WORLD SUPERPOWER
 
Inaonekana huu mgogoro hautakwisha mapema coz hakuna upande unaotaka kuonekana ni DHAIFU dhidi ya mwingine

Pia naona Kama usalama wa ulaya unaingizwa mkenge na USA
Mambo bado yapo Moto ..... tuendelee kuhubiri

Labda ni wakati wa AFRICA KUWA WORLD SUPERPOWER
Africa hii ya kuagiza hadi chakula? Kwa maoni yangu bado sana.
 
Wameshajua Russia ni tapeli anatishia msijiunge na Nato ili iwe rahisi kwake kukuvamia, wameshamjua na hakuna huyo mjinga atakaye tishika.

Yeye nyuklia asogeze tu jirani wala hakuna anayetishika mbona wengine wanazo ndani na hata huyo Finland na Sweden nao watapewa na marafiki zao na watazielekeza Russia.
 
Wameshajua Russia ni tapeli anatishia msijiunge na Nato ili iwe rahisi kwake kukuvamia, wameshamjua na hakuna huyo mjinga atakaye tishika.

Yeye nyuklia asogeze tu jirani wala hakuna anayetishika mbona wengine wanazo ndani na hata huyo Finland na Sweden nao watapewa na marafiki zao na watazielekeza Russia.
Kama kuna jambo wakubwa wa ulaya hasa Germany, Uingereza na France watalifikiria mara mbili ni hili. Ni rahisi kusema kwamba waweke tu, ila unapozungumza nyukilia unazungumza kitu kingine kabisa.. ikiwa vita yake itaanza dunia itashuhudia mabadiliko makubwa sana. Ngoja tuone wataishia wapi...
 
Binafsi naona hiyo ni njia ya kujihami ili kuendelea kuwa mbali na adui.

Nyukilia sio silaha inayomilikiwa na Urusi pekee, USA na washirika wake NATO baadhi wanazo nyukilia za kutosha. Hivyo hawezi ijaribu sumu kwa kuilamba.

Kiuhalisia bado Urusi hana ubavu wa kupambana na USA+NATO, kwa wakati mmoja akabaki salama. Ulaya ina madude kama Germany, UK na France yaani hao pekee wakiungana bila msaada wa USA pamoja na washirika wengine wa NATO waliosalia bado Urusi hatatoboa hiyo mbungi.
 
Kama kuna jambo wakubwa wa ulaya hasa Germany, Uingereza na France watalifikiria mara mbili ni hili. Ni rahisi kusema kwamba waweke tu, ila unapozungumza nyukilia unazungumza kitu kingine kabisa.. ikiwa vita yake itaanza dunia itashuhudia mabadiliko makubwa sana. Ngoja tuone wataishia wapi...
Kabsa mkuu......mmarekan mwenyewe alisalimu amri baada ya kupelekewa pale CUBA ......ingawa yeye alimpelekea mwenzake pale turkey
 
Binafsi naona hiyo ni njia ya kujihami ili kuendelea kuwa mbali na adui.
Nyukilia sio silaha inayomilikiwa na Urusi pekee, USA na washirika wake NATO baadhi wanazo nyukilia za kutosha. Hivyo hawezi ijaribu sumu kwa kuilamba.

Kiuhalisia bado Urusi hana ubavu wa kupambana na USA+NATO, kwa wakati mmoja akabaki salama. Ulaya ina madude kama Germany, UK na France yaani hao pekee wakiungana bila msaada wa USA pamoja na washirika wengine wa NATO waliosalia bado Urusi hatatoboa hiyo mbungi.
Mkuu.m, umeongea kishabiki kwenye hili.

Kwenye upande wa Nyuklia hakuna mbabe, wote mnapukutika that's y nchi zenye nukes zinaogopana

Trump alishindwa kumvamia kiduku ..ingawa ana silaha chache kabisa kuliko USA .....so USA anajua shughuli ya hizo Nyuklia
 
Binafsi naona hiyo ni njia ya kujihami ili kuendelea kuwa mbali na adui.
Nyukilia sio silaha inayomilikiwa na Urusi pekee, USA na washirika wake NATO baadhi wanazo nyukilia za kutosha. Hivyo hawezi ijaribu sumu kwa kuilamba.

Kiuhalisia bado Urusi hana ubavu wa kupambana na USA+NATO, kwa wakati mmoja akabaki salama. Ulaya ina madude kama Germany, UK na France yaani hao pekee wakiungana bila msaada wa USA pamoja na washirika wengine wa NATO waliosalia bado Urusi hatatoboa hiyo mbungi.
Inaweza ukawa sahihi lakini pia usiwe sahihi, baada ya vita ya pili ya dunia Germany waliwekewa vikwazo vya kujiwekeza kijeshi kusema Germany anaweza kua na nguvu ya kupigana na Russia ni kujidanganya wenyewe. Ni juzi tu ndio wamepitisha wazo la kutaka 2% ya mapato yake yaka finance jeshi, Europe kwa kiasi kikubwa wanamtegemea US kiulinzi hasa baada ya WW2
 
Wenye IQ kubwa kama sisi tunajua hiyo ni propaganda (mikwara) na pia hakuna mtu au taifa atakae piga bomu la nyuklia kwenye taifa lingine kwa hiyo jomba usiwe na hofu hakuna lolote hapo
 
Back
Top Bottom