YESU KRISTO NI MUNGU !
sifa na utukufu apewe yeye tu !
LICHA YA BIBLIA KUTWAMBIA WAZI WAZI KUWA YESU NI MUNGU !
Katika Biblia neno Bwana/ BWANA hurejerea Mungu/MUNGU !
sasa Leo tunaona namna ambavyo Yesu Kristo ndiye MUNGU, kwa kulichunguza hili jina " Bwana "
"Mimi ni Bwana, wala hapana mwingine ; zaidi ya mimi hapana Mungu " ( Isaya 45:5).
Bwana ni Mungu !
Kipindi waisraeli wakiteswa huko utumwani misri , aliyekuja kuwaokoa bado alikuwa YESU huyo huyo ambaye ndiye Bwana !
" Bwana akasema , Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko misri , nami nimesikia kilo chao kwa sababu ya wasimamizi wao ; maana nayajua maumivu yao"
( kutoka 3:7).
Lakini Musa alitaka kumkwepa Bwana kwa kusema kuwa eti yeye si mfasaha wa kusema , kwahiyo asitumwe yeye kwenda kuwatoa waisraeli huko misri mbele ya farao.
Lakini :
" Bwana akamwambia, Ninani aliyekifanya kinywa cha mwanadamu ?Au ni nani afanyaye mtu kuwa bubu au kiziwi , au Mwenye kuona au kuwa kipofu? Si Mimi , Bwana ?
( kutoka 4:11).
Bwana ndiye muumbaji !
Basi hata hivyo Musa alikuwa ameuliza jina la huyo Mungu ni lipi;
" Mungu akamwambia Musa , MIMI NIKO AMBAYE NIKO; akasema , ndivyo utakavyowaambia wana wa Israeli ; MIMI NIKO amenituma kwenu"( kutoka 3:14).
YESU alipokuwa hapa duniani alijitaja wazi kuwa yeye ndiye " MIMI NIKO " mbele za wayahudi.
" Yesu akawaambia, Amin , Amin nawaambia, yeye Ibrahimu asijakuwako , Mimi Niko "
( Yohana 8:58)..
Huo ulikuwa ushuhuda kuwa yeye ndiye yule waliyemsikia akinenwa ndani ya Vitabu walivyokuwa navyo;
YESU aliwaambia wayahudi kuwa maandiko yote wanayoyasoma yanamshuhudia yeye YESU, yaani maandiko yote yanatoa sifa na ukufufu wa Yesu Kristo AMBAYE ndiye Mungu aliyejidhihirisha wazi katika mwili.
" Mwayachunguza maandiko , kwa sababu mnadhani ninyi mna uzima wa milele ndani yake ; na hayo ndiyo yanayonishuhudia "( Yohana 5:39).
Lakini hapa pia baada ya wana wa Israeli walipoyashuhudia mambo makuu ya Bwana kwa kuwatupa wamisri baharini , WALIMWAMINI BWANA, WAKAMCHA BWANA , NA Musa mtumishi wake ( kutoka 14:31)
Wakasema haya ;
"Bwana ni mtu wa vita , Bwana ndilo jina lake "( kutoka 15:3).
Sasa ;
Yesu Kristo alikubali HADHARANI KUWA YEYE NDIYE Bwana (siyo bwana maana bwana ni yeyote yule hata mimi ni bwana ) LAKINI Bwana/ BWANA ni jina ambalo hupewa MUNGU Pekee .
" Ninyi mwaniita , Mwalimu , na Bwana ; nanyi mwanena vema, maana ndivyo nilivyo"
( Yohana 13:13).
Yesu ndiye Bwana yaani ndiye Mungu.
Wana wa Israeli walisema wanatoka misri ili wakamtumikie Bwana , Mungu ;
" La, tutakwenda safari ya siku tatu jangwani , tumchinjie dhabihu Bwana , Mungu wetu kama atakavyotuagiza"
( kutoka 8:27).
Ndugu ;
Bado hili jina Bwana ni la Mungu mwenyewe , YESU ni Mungu.
Baadaye katika safari ya wana wa Israeli kutoka utumwani misri , Bwana hakupenda watu wake waishi kama walivyokuwa wanaishi huko misri , aliwapa sheria zake ili ziwaongoze namna ya kuishi wao kwa wao na namna ya kumtumikia Bwana Mungu.
Alianza kwa kujitaja kuwa yeye ni Bwana , Mungu wetu ;
"Mimi ni Bwana , Mungu wako , niliyekutoa katika nchi ya utumwa,usiwe na miungu mingine ila Mimi" ( kutoka 20:2). Endelea mpaka msitari wa 17 amri kumi alizitoa Bwana.
Sasa,
Huyu MUNGU wetu baada ya kuona kuwa wanadamu tumetenda dhambi na tunakabiliwa na kifo , aliamua yeye mwenyewe kujitoa kwa ajili yetu ili tusife milele
( Yohana 3:16).
NDUGU YANGU !
Kwa YESU kila goti litapigwa ,na
kila ulimi utakiri , Yakuwa KRISTO NI Bwana , kwa utukufu wa MUNGU Baba, hata waliomchukia watampigia Magoti kwa kutahayari na kutetemeka huku wakikiri KRISTO NI BWANA ( Flipi 2:11)
& Isaya 45:23-24.
Sasa huyu Bwana ndiye anayeumba mbingu mpya na nchi mpya ambapo wanadamu wote watakwenda mbele zake kuabudu kila siku ya sabato;
"22.Kama vile mbingu mpya na nchi mpya ,nitakazofanya , zitakavyokaa mbele zangu , asema Bwana , ndivyo uzao wenu utakavyokaa.
23. Na itakuwa mwezi mpya hata mwezi mpya , na sabato hata sabato , wanadamu wote watakuja kuabudu mbele zangu asema Bwana "
(Isaya 66:22-23)..
Na siku ya Bwana :
" Bwana atakuwa Mwenye kuwatisha sana; kwa maana atawasafisha kwa njaa miungu yote ya dunia ; na watu watamsujudia yeye , kila mtu toka Mahali pake ; nchi zote za mataifa"
( sefania 2:11).
NDUGU YANGU YESU KRISTO NDIYE MUNGU AKIWAKILISHA UTATU MTAKATIFU.
"Kwa maana wako watatu washuhudiao mbinguni , Baba , na Mwana , na Roho Mtakatifu , na watatu hawa ni umoja "(1yohana 5:8)
Amua kuwa upande wake !
BWANA Awabariki
jifunze:horn: