Baada ya kutoka Msumbiji nikiwa sina kitu nikarejea Tanzania nyumbani safari mpya nyingine ikaanza

Baada ya kutoka Msumbiji nikiwa sina kitu nikarejea Tanzania nyumbani safari mpya nyingine ikaanza

IBRA wa PILI

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2017
Posts
1,549
Reaction score
2,668
_8e5c6f35-ce3a-44e9-b144-86ed31ddad4a.jpeg
Niliwai leta mkasa wangu nafikri wapo wanao kumbuka baada ya kutoka Mozambique.

Akuna muda wa kupoteza

Tuendelee Sasa
Baada ya kurudi hapa tz nyumban nikiwa mfukoni Nina elf 30 TU naikimbuka sana hii siku nikawasili maskani ikiwa saa 3 usiku wife akuamka sio ishu ya chakula Wala kuweka maji ya kuoga na alinisikia nikifika ila mlango alifungua mtu mwingine.

Nikaweka beg langu uzuri nilisha kula stend mgahawan so sikuuliza nikaona ajiangaishi na chochote mi nikalala zangu hapo nikawa na mawazo chungu nzima naanzaje life.
Hapa machalii wapo wawili na kule Mozambique mambo yalienda ndivyo sivyo ila pesa kwa wife nilikua natuma sana,

nilipunguza kutuma baada ya kupata shoti kwenye Kaz yangu ambayo nilikua nafanya ya kununua dhahabu na ndio ilipelekea mpaka nikaludi nyumban nikiwa Sina kitu.

Asubuhi wife alikua wa kwanza kuamka akafanya shughuli zake alipomaliza akaenda kwenye mishe zake na hata akuniaga mi pia Nika amka nikafanya mambo yangu nikasepa kitaa.

Jioni aliporudi Yuko bize na mambo yake mpaka nikajiuliza uyu mtu kapatwa na nini Yani ni kama nilikuepo tu hapa na sijatoka mahali nikamuuliza toka nimerudi upo bize ni kama unioni kwani vipi akajibu we unayo Fanya uyaoni, nikamuuliza yapi ayo akajibu mkato mi sijui unajua mwenyew, nikamwambia kwaiyo utaendelea kua bize ivyo ivyo akajibu ndio nikasema sawa watoto si hawa hapa acha tupambanie watoto basi akuna shida we endelea kua bize akasema sawa.

Niliwaza sana pesa nilikua natuma ya matumizi alafu naludi naonekana kama nilijizila huko niliko au kama nilikua sikumbuki familia afu nikiyumba ndio inakua shida kwa wife.
wakati nakaribia kuludi ndio nikapata shoti sasa baada ya kupata shoti nilikua natuma pesa lakini ndogo tofauti na mwanzo nikaona shida ndio iliko anzia.

Ok Nika endelea ku unga unga kitaa na washkaji sometimes nikipata vijisent huko maisha yanasonga wife Yuko bize sikujali sababu niliona kashahamua kua ivyo ila Nilijua Kuna kidudu mtu kimeingia hapa sio bule
yeye alikua anafanya biashara ya dagaa Sasa huko kwenye biashara Kuna mengi marafiki wa ovyo wazuri pia wapo, vishawishi vingi n.k.

Hapo ilikua ni mwaka 2022 mwishoni Yani mwez wa 12 mshikaji wangu yule wa MSUMBIJI alisema tuonane tukakutana kwenye pub maarufu sana pale songea
LA CHALZ.

tukapiga stor sana zaidi alisema mwanang sitakutupa japo ulipata shoti ila mambo acha yakae sawa tutajua tunafanya Nini yeye alikua anakunywa bia safari mi nilikua napiga Pepsi wakati tuna endelea na maongezi akapita demu flani hivi tulikuaga nae huko msumbiji akajiunga bana stor mbili tatu wakaeleewana waende gest apo ni saa saba usiku.

Akaniambia nimsubiri pale wakaenda huko gest zimejaa zingine zimefungwa wakarudi pale jamaa akasema ngoja naenda kupiga mpenyoni uyu waka ondoka Tena baada ya robo saa wakarudi😄😄 jamaa akasema uhakika kapiga
, stor zikasonga baadae demu akaanza kudai ela jamaa akazama mfukoni akatoa elfu kumi akampa demu akasepa si tukaendelea pale mpaka saa 8 hivi tukatoka mshkaj akachukua boda mi akanipa buku 2 mhm niliguna moyoni ye akachukua boda tukaagana aka enda mi nikatoka mdogo mdogo ule usiku na Giza mpaka home sikupanda pkpk nafika maskani saa9 nikazama ndani kimya kimya tu wife alifungua mlango.

Tupo ndani wife akasema kwaiyo saiz ndio umeamua kuludi usiku namna hii nikamwambia hata nikiwai, niwai Nini si Kila mtu yupo bize Kuna tatizo na je kama nafanya kazi, akasema naomba iyo ela uliopata huko kazini nikamwambia kama nalipwa kwa wiki au mwezi nikamwambia alafu usinipande kichwani we uko bize endelea kua bize.

Asubuhi maisha yakasonga ubize kama kawaida Kuna mshkaj wangu alikua anasimamia tofali za bloku Kijiji flani hivi akaniambia kama vipi twenzetu mwanang tukapige kazi nikaona nifanye ivyo.

Iyo siku nikachukua godoro la kulalia na nguo zangu chache asubuhi wife nikamuaga Kuna sehemu naenda Fanya Kaz akajbu sawa akuuliz Tena chochote labda Kaz Gani, unaludi lini je malipo yake akuna alafu kumhaga upande wangu ilikua kutafuta amani niendako ila niliona akuna amani kwa alivyojibu.

mi nikasepa na mshikaji mpaka maeneo ya kazi tulienda na gari. So tulifika ile siku kama mida ya saa moja hivi tukaenda tafuta mgahawa tukala msosi fresh stor nyingi cheki mazngira maana mi ndio nilikua mgeni pale.

Siku ya pili asubuhi wakati tunataka kuanza kazi machine ya kuchanganyia mchanga na cement ikazngua ikabidi mpaka aje fundi kutengeneza baada ya kukaa sawa machine usiku hivi tukaanza kazi kama nusu saa ilitosha machine ikabuma Tena na kazi ikaishia hapo tukaenda kulala ili asubuhi mafundi waje Tena kurekebisha.

Asubuhi na mshkaj baada ya kupata chai tukawa tuna zurula TU tukisubiri mafundi na boss alivyofika akaja na wazee flani hivi ili kupiga ndagu pale maana alihisi anafanyiwa mchezo so akachinjwa mbuzi na maseke mengne kibao kwenda kuchimbia kwenye machine sjui ngozi na makolokolo mengne.

Sku ya pili baada ya kuweka fresh machine kazi ikaanza baadae ikaja Dili ya kupakia tofali kwenye Gari nikajiunga chapu na Mimi kupakia tukiwa tunapakia pale tofali wakati naweka tofali kwenye Gari Kuna jamaa tofali ilimtoka mkononi ikanigonga Mimi mkono wa kushoto nikaumia na kazi ikaishia hapo.

Nilikaa pale siku kama mbili hivi sjapona mkono, nilichua na dawa flani hivi alafu nikafunga na bandeji mkononi ikabidi nifanye mpango wa kusepa tu Sasa wife nikampa taarifa kwamba nimeumia jibu likawa sawa akutaka kujua ilikuaje na nimechukua hatua Gani akuna sikujali nikaludi home 🏠.

Kabla ya kufika nyumban nikapita sehemu flani hivi Kuna wi-fi ya kitonga nikatulia pale nikaperuz mpaka mida ya saa mbili nikaenda maskani, kufika pale home nikamsalimia wife Cha kwanza kwake akauliza ela uliopata huko ikwapi ?!
Nikamwambia ndio Cha kwanza kuuliza hicho nilikupa taarifa nimeumia uhulizi afya yangu unauliza pesa we ni mtu Gani ujali afya ya mwenzio Ivi bila afya njema iyo pesa natoa wapi we mpumbavu unaweza pesa kuliko Hutu hapo alikaa kimya na angeendelea ningempa viganja aliniboa sana.

Siku ya pili au ya tatu toka niludi kule kwenye tofali mama yangu mkubwa ana guest na grocery eneo flani hivi akaniambia nikamsaidie kusimamia angalau nikapata sehemu ya kupotezea muda na kupata vijisent siku nyingne nikawa nalala huko nikachukua na nguo chache fresh ikawa nikipga hesabu pesa kidogo napeleka home, lakini hapo nikawa nawaza nipate mishe ya maana ya kufanya na sio kutegemea pale.

Bana bana bana wife akiwa huko na wenzake akatangaza nyumban pale nimehama aisee na sikumwambia nalala wapi na nimepata ka kibarua wapi kwasababu hata nikimwambia ajali chochote nikaamua kukaa kimya tu ndio akatangaza nyumban pale nimehama akikutana na jamaa zangu maneno ndio ayo.

Sikujali Mimi nikaendelea pale na ile kazi Kuna siku nikawasiliana na mshikaji wangu mmoja alikua pwani Dar kwenye kiwanda anafanya kazi kiwanda Cha Tiles (malumalu) nikamwambia anifanyie mpango na Mimi niende kupiga kazi akasema nijipange ye anaweka michongo fresh niwe na nida, tin number kwajili ya nssf na nifungue account nmb.
Akasema ana mpanga kiongozi niandae 50 nikasema poa nikajichanga chap nikapata nauli na iyo 50 ya kumpa kiongozi aongee na meneja Nika mtel na bi mkubwa nae akaniongezea pesa safari ikakamilika wazee.

Nida nilikua nayo tin number nikaenda website ya Tra chap nikapata tin number, akaunt sikufungua jamaa akasema ntafungua Kule pwani nikifika.

Kesho kutwa safari Leo nikaenda hom bana sikukuta funguo inapokaa ili niweke mazngira fresh ya kuondoka nikamcheki wife kwa simu akaniambia unataka Nini hapo nyumban we si umehama nikamwambia nilikwambia nimehama lini mbona nguo zangu na vitu vyangu vipo ndani niambie funguo ipo wapi

Nataka Kuingia ndani gari inanisubiri natak kuondoka Nika mzingua una nichelewwsha ujue funguo inakaa nyumbani je ukipoteza huko ulikobeba nataka funguo Sasa hivi nikija huko ulipo ukorofi.

Akasema mi nipo mbali na funguo Kuna mtu nime muachia nikamuuliza umeenda wapi na kwann funguo umkabizi mtu ilikua na maana Gani we kuibeba huko nikamwambia naondoka endelea na mambo Yako gari nishachelewa nikasepa.

Siku ya pili asubuhi nikaenda maskani sikua na stor nyingi kwake nikampa elfu kumi kwanza nikanunua dagaa dumla moja kwake hapo nilikua na mafuta ya kula alizet pamoja na unga ili nikifika kwa washkaji nisiwe mzigo,
Baadae nikamuachia pesa ya matumizi.

Hapo nilikua nakopaga hela pesa x nilifikisha EF 50 nikakopa hii niliwapiga sikuwai kulipa mpaka Leo hii,
ila walisumbua sana na bahat mbaya niliweka namba ya broo wakawa Wana msumbua kinoma.

Ilikua ni mwezi wa tatu iyo ya mwaka 2023 tarehe sikumbuki.

Siku iliwadia wife nilimuhaga jibu ni sawa akuuliza chochote huko niendako na akuwai kuuliza, na hata akujua naenda Fanya kazi gani
Asubuhi ya saa kumi na moja siku ya pili ake nilipanda selous express na saa kumi na mbili chuma ilianza safari kuelekea pwani

Hapa Sasa ni maisha mengine mapya ya kazi niendako ni Pwani, Dar es Salaam najua ni mikoa miwili tofauti ila pwani ziko nyingi Sasa hii ni Pwani ya Dar wilaya ya kibiti sijui ni mkuranga nafikiri msha elewa......


Tukutane baadae tukijaaliwa tuendelee nilipo ishia chiiiiiiiaaaziii

(Tusamehane uandishi)
 
Tuendelee
Sio vyote nta andika vingine ambavyo avina umuhimu Sito andika.

Nilifika pwani saa 2 kama na nusu hivi baada ya kushuka jamaa yangu alikuja hapo kama robo saa baadae, nilipo panda garini nilibeba unga, mafuta hivi vilikaa kwenye buti alafu dagaa niliingia nao ndani ya gari.
Unga na mafuta vilipotea konda nae maelezo ayafungamani nikaamua kupotezea ndio ikiawa imeisha iyo,

tumefika geto kwa mshikaji ni geto ambalo wao walikua wawili na Mimi Sasa tukawa wa tatu na nikaanza maisha ivyo jamaa akafanya harakati zake kule kiwandani nikakamilisha Kila kitu mpaka muda ukafika nikapigiwa simu niende siku flani kuanza kazi.

Tarehe 14 ya mwez wa tatu mwaka huo nilifika asubuhi mapema kiwandani nikakutana na wenzangu ambao nao walipigiwa simu tukachukuliwa na HR mpaka ofisini tulikua 20 na kidogo wachache wakaitwa Majina wakatolewa pale wakaondoka na HR baadae akarudi yule hr akatuchukua sisi mpaka kwa kiongozi mmoja akatukabizi hapo.

Na yeye kuondoka tukiwa pale kiongozi akatuambia nyie mmekuja kuanza kazi na mtambue Sasa kitengo chenu ni kitengo Cha ujenzi ivyo humu ndani masuala ya ujenzi nyie ndio mta husika na mmeingia muda ambao godauni linaanza kujengwa kwaiyo kazi zipo za kutosha.

Kidogo atuja kaa sawa yakaja masululu na chepe tukachukuliwa mpaka sehemu ya kazi kufika pale tukagawana wawili wawili mmoja chepe mwingine sululu kazi ikawa kuchimba mashimo ya nguzo za godauni mt 150 kwenda chini na upana 100 hizi kazi sikuwaigi kufanya Sasa hapa ndio kimbembe e bana tulipiga kazi na kiongozi anasema mkishndwa kumaliza basi ujue umeshindwa kazi.

Ile sehemu limepita skalveta kusawazisha na kushindilia ebana pagumu ni balaa tulipiga kazi alafu kama mnavyojua ukanda wa pwani huku jua Kali ile siku naikimbuka wazee nilikunywa maji mpaka basi kama sikufikisha ndoo dogo basi ni kidogo sana maana jua Kali pakujificha akuna na kiongozi anakwambia akuna kupumzika mchina anataka aone kazi inafanyika kwaiyo kazi iendelee kwa Kasi.

Jasho linatoka mwilini mpaka unapata was wasi ntaishiwa maji kufika saa 6 muda wa kula kiongozi akatuambia Sasa tukale tupumzike mpaka saa 7 turudi kazini hapo ndio kupumua hoiiiiiii kweli Kweli bin taaaabani tumekula fresh tumepumzka pale na Kuna Wi-Fi tukawa tuna peruzi pale kuvuta muda kidogo saa 7 hii watu kazini piga kazi kiongozi mkishndwa maliza Aya mashimo ndio mwisho hii ni interview yenu mchina anawatoa kazini.

Piga kazi mpaka saa 12 jioni kazi aikwisha nilichoka kinyama sio Mimi mpaka na wenzangu Kila mtu anasema lake hasa ukizingatia tulijua tunaenda kwenye malumalu mule ndani Kuna vitengo vingi, umeme, kuchomea , dereva folk , fundi magari , operator wa skalveta na wheel loader n.k

So hapa niliingia kitengo Cha ujenzi ni heavyweight kitengo na kama ujazoea kazi ngumu unalo aiseee pale wengi tuliingia Kaz ngumu atujafanyaga mtaani.

Siku ikaisha nimerud goti nipo hoi mshkaj akasema du kitengo Cha ujenzi ni balaa ila Sasa tunafanyaje ndio nishaingia inabidi kukomaa tu alafu huko mbele tuangalie ikiwezekana tubadilishe,

hapa niliwaza hii kazi siwezi nimetoka mbali kuja huku ila hii kazi hapana sitoboi narudiji nyumban hata bi mkubwa nilimwambia naenda sehemu flani kufanya kazi na home Kuna wife na watoto wawili Leo naludi nimeshindwa kazi na gaharama pia nimetumia kuja huku kurudi Nako gharama Sina pesa ya kuludia na je ntaonekana vipi mtoto wa kiume nimeshindwa kazi niliwaza sana.

Siku ya pili kazini tukasimama paledi mawaiza kidogo baadae Tena kama Kawa kiongozi akasema watu wangu tuka endelee na mashimo yetu duh akuna kupoa tukarudi mzigoni aisee piga kazi ikafika muda tukakuta maji Sasa ikawa ni tope hapa ndio balaa bana acha tu niliekua nafanya nae kazi baada ya chakula Cha mchana akaenda omba ruhusa anaumwa akasepa nikabaki pekee angu nikaona ndio muda wa kupumzika huu nafanya kazi kidogo natulia.

Alikuja kiongozi mbona hapa nyinyi Bado nikamwambia nipo peke angu, mwingine yupo wapi kaomba ruhusa anaumwa ameondoka kiongozi akasema Hawa watu wazembe awatakiwi kabisa uvivu TU akasema endelea mwanang aka ondoka mi ndio ikawa pona yangu mdogo mdgo mpaka jioni siku ikaisha ivyo lakini Bado nipo hoii.

Nilikua na mawazo sana juu ya ile kazi na kile kitengo Cha ujenzi wengne siku 2 TU walikimbia, kazi wameshindwa Kaz ngumu mi Bado nilipambana Kuna siku ikawa afazali unapangwa sehemu nyingine upigiki sana Kuna siku unaingia mtaroni kutoa uchafu mitaro michafu balaa, Leo kuhamisha nondo kesho vyuma , usisahau zege hapo. Baadae nikajua sio siku zote Utakua sehemu ngumu siku nyingne unapata nafuu na kadri unavyo zidi kuzoea mazngira basi Kuna Ka unafuu kidogo ila hapo tulishapungua mi nilijiona mvivu ila nilikutana na wavivu kazi iliwashinda kudadeki.

Kuna kupasua floor kama zege imeharibika imeweka hufa Kuna nyundo iyo balaa zile kubwa za kupasulia mawe mnavunja kwenye ilo eneo, ile nyundo nzito usipime mnavunja
mna sawazisha Kisha zege inafata Tena msiombe iyo zege mchanganye kwa mkono alafu eneo liwe kubwa mtakoma aisee Bora ichanganye machine ndio itakua pona yenu .

Mara ya kwanza ndio nashka ile nyundo tulikua tunapasua zege ili lichimbwe shimo la nguzo nilipiga pafu za nyundo tatu nikakaa pembeni na homa hapo hapo malaria Nilichukua ruhusa ya siku tatu nikapona then nikarudi kazini.

Kazi iendelee kumbuka hapo atujapewa mkataba ukizingua mda wowote unatimuliwa hatimae mwez ukaisha na sisi tuliingia katikati ya mwezi muda wa mshahara ukafika tukapokea ambae ana mkataba na asie na mkataba utoafuti upo hivi mwenye mkataba mshahara upo juu na asie na mkataba mshahara upo chini mnatofautiana.

Mi nimepokea basi pesa nikamtumia bi mkubwa kidogo na wife nae ila mara zote nipo huku kwa huo muda wife ilikua nisipo mtafuta Mimi basi imeisha iyo sikujali maisha mapya ya kazi yakawa Yana songa nikaanza kuzoea ile kazi na mwili ukawa una kubali taratibu ivyo ivyo mpka ikafika miezi mitano hapa sishangai Tena kazi zote nazijua sio kusuka nondo kwajili ya madaraja sio zege, kuvunja ukuta, kugonga paleti za kuwekea malumalu n.k
Ila tuliendelea kupungua kadri muda unavyozidi kwenda watu waliacha kazi lakini pia kama unakaza ujuzi pia unapata.

Ikafika muda wa kupewa mikataba hapa Sasa kikawa kisanga imepita miez 7 alafu Sasa kiongozi ndie ana andika Majina nani apewe mkataba nani asipewe mkataba Majina yalipelekwa ofisini na watu wakawa wanaitwa kwenda kusaini mpaka watu wanaisha Mimi sikuepo na jamaa zangu flani tukahoji vipi kwa viongozi Kila mmoja ana mlushia mpira mwenzake tukaenda ofisini kuuliza tukapewa majibu kwamba waliopewa mikataba wanasimamiwa na hao viongozi na ndio wamesema hao ndio wanafanya kazi kwa bidii mliobaki wazembe kwaiyo muongeze juhudi mtapewa mikataba duuuu.


Hii ishu iliniuma sana sana Yani kupambana kote kule una onekana useless viongozi tukiwauliza wanasema bosi ndio kaamua Yani mchina wakati ssi kazi tunafanya na wao aisee niliona zarau kubwa sana tukakubali na maisha ya kaendelea ila niliweka chuki sana na wale viongozi.

Basi bana tuka endelea na kazi kumbuka na wife mambo sio mazuri yeye nikipiga simu kumjulia hali na watoto Cha kwanza vipi hela ya matumizi hata umwambie napokea mwisho wa mwez nikituma jibane.

Pia pale kwa washkaji nilihama nikaenda kupanga kwaiyo na mim huku pango na matumizi mengine pia ninayo yeye aelewi ndio kwanza anatangaza nimetelekeza familia ivyo Kila kitu anafanya yeye.

Yani mambo chungu nzima, mi Nika endelea na kazi nika jifunza folk lift iyo hapo kwa wasio ijua👇
IMG_20250621_085032.jpg
nikawa na endesha na ku oparete vizuri.

Alafu Kuna jamaa tumetoka mkoa mmoja alikua ni opareta wa wheel loader iyo hapo👇 kwa wasio ijua
IMG_20250621_085222.jpg

akaanza nifundisha nae kama wiki hivi akafanya kosa mchina aka mtimua nikaishia hapo wengine ukiwafata wakufundishe wanataka ela nyingi hapo unajifunza ki wizi wiz ukipata chance ndio hapo hapo.

Ikatimia mwaka mmoja bila ya mkataba hapo tushapambania sana holaa
tarehe 5 ya mwez wa 4 mwaka huo tukapewa mkataba hapa tumebaki wachache sana ambao tuliingia.

Wale waliopewa mkataba ambao ndio walisema wanafanya kazi kwa bidii waliachaga kitambo sana kipindi hiki Sasa nipo kwenye upande wa nondo
Sasa mi ni fundi nakunja nondo nasuka bezi za madaraja nanyosha natengeneza bimu nakunja lingi vipimo ukinipa fresh tu.

wale viongozi waliotunyima mkataba this time ndio walikua Wana niona wa muhimu tulikuwa watu Ka 8 hivi ambao ndio tulikua upande wa nondo Yani kipindi hiki kazi ya nondo wale viongozi ndio utwasikia flani sehemu flani zinahitajika nondo na nini kwaiyo tukapige kazi pale
moyoni nilikua nachuki nao niseme ukweli
Kwanini nasema hivi kwa sababu ya ile mikataba kuchelewa kupata ukiwa na mkataba mshahara si unajua juu na hata nssf inakua juu
Na kama ahuna mkataba nssf inakua chini sababu mshahara upo chini yupo mshikaji wangu aliniacha mbali kwenye nssf alipata mkataba mapema yeye alikua fundi seremala.

Tuendelee siku iyo tupo tunapiga usafi kulikua na mvua mvua zile ndogo ndogo nimebeba uchafu kwenye toroli naenda mwaga ile nimemwaga nikateleza alafu toroli bahati mbaya alikua na stendi zile za kusimamia ivyo nikaanguka chini alafu ile mishikio au mikono ya toroli ikaja kwa juu ikaniponda pembeni ya jicho ilibaki kidogo sana ingepasua jicho aisee ilinichana kwa pale sikujua japo nilihisi kama sipo vizuri nokasimama Nika ondoka washkaji zangu waliponiona wakashtuka vipi hapo damu zinaanza toka kwa wingi Sasa alafu wameshika vichwa kujicheki kwenye kioo Cha dirisha nimeumia aisee ikabidi niende kwa dokta.

Dokta akanipa hudumua ya kwanza akaja meneja akanipiga picha akatuma kwa wachina Kisha nikachukuliwa mpaka hospital kwajili ya kwenda kushonwa muda huu ndio nimevimba jicho alionekani mtu akini angalia aludii kunitazama Tena.........

Ntaludi kuendelea nilikua safarini kidogo saiz bandika bandua mpaka tuna maliza Poleni
 
Back
Top Bottom