Wakuacha
JF-Expert Member
- May 19, 2015
- 2,041
- 1,323
Habari wana JF,
Ni siku nyingine tulivu namshukuru Mungu kwa kuniwezesha kuiona siku hii ya Leo maana wengi walitamani lakini hawajafanikiwa kuiona na wengine wapo mahospitalini eeh Mungu wasaidie wapone.
Katika maisha wanawake si wa kuwaamini kwa asilimia 100 zote hapana kabisa. Mwaka 2009 niliajiriwa baada ya kuanza kazi mwaka huo 2009 nilijikita zaidi katika kujiendeleza kielimu nilijiunga na Chuo Kikuu huria na hatimaye mwaka 2012 nilihitimu Degree yangu.
Mwaka huo waliajiriwa wafanyakazi wengine walikuwepo ma binti kadhaa pamoja na wanaume kadhaa kama ilivyo wafanyakazi wanapoajiriwa kidogo mambo yao huwa yanakuwa hayajakaa sawa sawa. Nilitokea kumpenda binti mmoja kati ya wale wageni nikasema huyu ndiye na lazima atakuwa mke wangu.
Kiukweli nilimpenda na hata yeye pia alinipenda uhusiano wetu ulikuwa imara baadae mimi na yeye tukawa tunatembeleana kwa kuwa naye alikuwa amepanga nikawa naenda kwake nalala au yeye anakuja analala kwangu.
Mwaka 2013 mwezi wa 11 nilipatwa na matatizo kazini na kupelekea kufikishwa mahakamani kwa kosa la MAUAJI, wakati nikiwa gerezani nikisubiria vikao vya jaji kwa sababu mimi nipo pembezoni mwa Tanzania.
Nilikaa gerezani takribani mwaka mmoja na miezi kadhaa ndio jaji alikuja na kuanza kusikiliza kesi yangu katika kipindi chote hicho huyo mchumba wangu alikuwa akija na kuanza kunifariji sana Mara nyingi alikuwa akija siku za Jumapili pale Gerezani aliniahidi atanivumilia.
Kwa kuwa mshahara ulikuwa ukiendelea kusoma nilimkabidhi kadi yangu ya bank na vitu vyangu vyote nilimkabidhi yeye, mwaka 2015 mwanzoni ndipo nilipatikana na HATIA YA KUUA BILA KUKUSUDIA na nikahukumiwa kwenda Jela miaka 5, alilia sana huyo mchumba wangu nilimsihi asilie maana hii yote ni mipango ya Mungu nilimuambia asijali mimi nitatoka tu maana HAKI YA MTU HUWA HAIPOTEI.
Wakati nipo Gerezani baada ya hukumu ile akaanza kubadilika nilikaa mwezi mzima bila kumuona nikaanza kusikia kwa watu kuwa mchumba wako yule Fred ambaye ni mdogo wako kikazi nasikia wanatoka niliumia sana kusikia vile niliamua kukata Rufaa na bahati nzuri niliachiwa huru mwaka Jana.
Niliwakuta tayari wamwashaoana na wanaishi kama mke na mume nilimfuata nikamuambia anipe vitu vyangu kwa aibu yule dogo alijificha chumbani, nilichukua vitu vyangu na kuondoka pale.
Tufanyeni kazi lakini watu sio wazuri pata matatizo ndo utajua nani ni mchumba/mke wa kweli.
Ni siku nyingine tulivu namshukuru Mungu kwa kuniwezesha kuiona siku hii ya Leo maana wengi walitamani lakini hawajafanikiwa kuiona na wengine wapo mahospitalini eeh Mungu wasaidie wapone.
Katika maisha wanawake si wa kuwaamini kwa asilimia 100 zote hapana kabisa. Mwaka 2009 niliajiriwa baada ya kuanza kazi mwaka huo 2009 nilijikita zaidi katika kujiendeleza kielimu nilijiunga na Chuo Kikuu huria na hatimaye mwaka 2012 nilihitimu Degree yangu.
Mwaka huo waliajiriwa wafanyakazi wengine walikuwepo ma binti kadhaa pamoja na wanaume kadhaa kama ilivyo wafanyakazi wanapoajiriwa kidogo mambo yao huwa yanakuwa hayajakaa sawa sawa. Nilitokea kumpenda binti mmoja kati ya wale wageni nikasema huyu ndiye na lazima atakuwa mke wangu.
Kiukweli nilimpenda na hata yeye pia alinipenda uhusiano wetu ulikuwa imara baadae mimi na yeye tukawa tunatembeleana kwa kuwa naye alikuwa amepanga nikawa naenda kwake nalala au yeye anakuja analala kwangu.
Mwaka 2013 mwezi wa 11 nilipatwa na matatizo kazini na kupelekea kufikishwa mahakamani kwa kosa la MAUAJI, wakati nikiwa gerezani nikisubiria vikao vya jaji kwa sababu mimi nipo pembezoni mwa Tanzania.
Nilikaa gerezani takribani mwaka mmoja na miezi kadhaa ndio jaji alikuja na kuanza kusikiliza kesi yangu katika kipindi chote hicho huyo mchumba wangu alikuwa akija na kuanza kunifariji sana Mara nyingi alikuwa akija siku za Jumapili pale Gerezani aliniahidi atanivumilia.
Kwa kuwa mshahara ulikuwa ukiendelea kusoma nilimkabidhi kadi yangu ya bank na vitu vyangu vyote nilimkabidhi yeye, mwaka 2015 mwanzoni ndipo nilipatikana na HATIA YA KUUA BILA KUKUSUDIA na nikahukumiwa kwenda Jela miaka 5, alilia sana huyo mchumba wangu nilimsihi asilie maana hii yote ni mipango ya Mungu nilimuambia asijali mimi nitatoka tu maana HAKI YA MTU HUWA HAIPOTEI.
Wakati nipo Gerezani baada ya hukumu ile akaanza kubadilika nilikaa mwezi mzima bila kumuona nikaanza kusikia kwa watu kuwa mchumba wako yule Fred ambaye ni mdogo wako kikazi nasikia wanatoka niliumia sana kusikia vile niliamua kukata Rufaa na bahati nzuri niliachiwa huru mwaka Jana.
Niliwakuta tayari wamwashaoana na wanaishi kama mke na mume nilimfuata nikamuambia anipe vitu vyangu kwa aibu yule dogo alijificha chumbani, nilichukua vitu vyangu na kuondoka pale.
Tufanyeni kazi lakini watu sio wazuri pata matatizo ndo utajua nani ni mchumba/mke wa kweli.