white wizard
JF-Expert Member
- May 18, 2011
- 8,317
- 13,285
Ni pipa na mfuniko!!msanii tu, jana anaulizwa kuhusu Ponds za samaki, hizo 26, ambazo wawekezaji wana vibari, vya kutumia maji hayo, anakimbia kimbia tu!!zigo anaenda kutwishwa mtendaji wa kata eti alikuwa wapi, watu wanatumia maji ovyo!!sasa watu wana vibali toka bodi ya bonde husika wewe mtendaji unasauti ipi tena?!!Kwahio huyo waziri mpenda sifa na Magu hawatofautiani sana,kama Jinsi alivyo okota vichwa vya treni pale bandarini?
Nikisema kuna watu ni Wapuuzi naambiwa eti Mimi sio Mzalendo, asante sana mleta madaMamlaka ya maji inajitapa kuwa baada ya kuwakamata waliokuwa wanachepusha maji imewasja mtambo wa Ubungo baada ya kina cha maji kuongezeka! Sijui ni utaalamu gani huu au ni siasa. Kina cha maji kinawezaje kuongezeka wakati yanakoanzia maji hakuna ongezeko la maji! Jibu tutalipata wiki ijayo mgao wa maji utakapo isha.
Tuanze na sisi wenyewe at individual level, Je huwa tunavuna kiasi gani cha maji msimu wa mvua kutoka kwenye maji yanayotiririka kwenye mapaa ya nyumba zetu? Kwa maoni yangu Nchi yetu haiwezi mudu Gharama za kutengeneza bwawa la kuvuna maji ya mvua kwa ajili ya watu milioni 5 wa jiji la Dar kutumia mwaka mzimaDuu kumbe hata mabwawa ya kuhifadhi maji hakuna ?
Hao wataalamu bogus kabisa na mawaziri wote wa maji wamepita bila kuliona hilo
Sikulijua hili poleni sana
Maji ya Mtera huwezi kupeleka Dodoma kwasababu ndiyo hayo yakitoka hapo yanaenda kuzalisha umeme kwenye bwawa la kidatu. Ukipeleka Dodoma ina maana bwawa la kidatu life.Ninakumbuka zamani mji wa Mbeya haukuwa na bwawa pamoja na maji kutiririka toka milimani, mji wa Iringa pia wanakinga maji kwenye mto Ruaha badala ya bwawa, Morogoro Mindu lilijengwa miaka ya tisini mwanzoni, nalo linanaharibiwa na wachimba dhahabu hivyo halijafikia lengo, Tabora Gombe lilijengwa na mwingereza kabla ya uhuru, Dodoma Mtera ingeweza kuipatia maji.
Hahaha walifanya maamuzi ya kidwanzi, walidhani wangelisha taifa kwa chakula walichohifadhi watu mia!! Tena kwenye vigunia kumi, ishirini!Inanikumbusha wakati wa Nyerere kulikuwa na uhaba wa chakula, msako ulifanyika majumbani kutafuta wanaoficha chakula, wakapatika wenye ndoo za mchele na unga tukawaita wahujumu uchumi, nafaka hizo zikapelekwa kwenye maduka ya bidhaa muhimu watu na mawe wakajipanga foleni kununua, waliofanikiwa kuuziwa watu wachache tu zikaisha, tatizo likabaki palepale mpaka mmarekani akatuletea yanga na mchina akaleta kitumbo.
Kwahiyo serikali haina uwezo wa kujenga bwawa! Kwa taarifa yako serikali inao uwezo huo.Wewe at individual level huwa unavuna kiasi gani cha maji msimu wa mvua? Unajua gharama za kutengeneza bwawa la kuvuna maji ya mvua kwa ajili ya watu milioni 5 wa jiji la dar?
Mkuu, serikali yenyewe hapo ilipo ina madeni ambayo hata hatujui yataisha lini. Ukiachana na madeni bado kuna vipaumbele vingine vingi sana. Inawezekana lkn at the expense of other priorities au tuongeze tozoKwahiyo serikali haina uwezo wa kujenga bwawa! Kwa taarifa yako serikali inao uwezo huo.
Tangu tumepata uhuru wangeweza kujenga endapo wangekuwa na akili hiyo, wao walibakia na walichoachiwa na mwingereza.Mkuu, serikali yenyewe hapo ilipo ina madeni ambayo hata hatujui yataisha lini. Ukiachana na madeni bado kuna vipaumbele vingine vingi sana. Inawezekana lkn at the expense of other priorities au tuongeze tozo
Tuanze na sisi wenyewe at individual level huwa tunavuna kiasi gani cha maji msimu wa mvua kutoka kwenye maji yanayotiririka kwenye mapaa ya nyumba zetu? Kwa maoni yangu Nchi yetu haiwezi mudu Gharama za kutengeneza bwawa la kuvuna maji ya mvua kwa ajili ya watu milioni 5 wa jiji la Dar kutumia mwaka mzima
Weka dauNinachojua Mimi bandari ya Bagamoyo haitajengwa...
Jiandaeni kula matembele kabisa 😂😂Hizo mboga mboga na matunda wanayomwagila ndo vimejaa sokoni,sasa wakiacha kumwagilia tujiandae na njaa pia Mboga mboga zitapanda bei.