Baada ya kukiuka mkataba wa NATO kuwa isijitanue zaidi na kuweka makombora Poland na Romania. Warusi wamerudi tena Cuba

enery

JF-Expert Member
Aug 21, 2015
368
437
Katika hotuba yake kwa Bunge la Urusi mnamo tarehe 18 Aprili 2014, ambapo Rais wa Urusi Putin alithibitisha kuingizwa kwa Crimea katika nchi ya Urusi na kuwa sehemu ya Urusi, alisisitiza udhalilishaji wa Russia uliotoka kwa sababu ya ahadi nyingi zilizoharibika na zinazo endelea kuhaibiwa na Magharibi, ikiwa ni pamoja na ahadi ya kudai kutokukua NATO zaidi ya mipaka ya Ujerumani.

Upanuzi wa NATO kwa Georgia na Ukraine unahatarisha usalama wa nci ya Urusi, Rais Vladimir Putin alisema katika mahojiano na mwandishi wa habari wa Fox News "Chris Wallace", muda mfupi baada ya mkutano wake na Rais wa U.S.A Donald Trump huko Helsinki mnamo Julai 16, 2018.

Alipoulizwa nini msimamo wa Kremlin ikiwa Georgia na Ukraine watakubali kuingia katika shirikisho la NATO, Putin alisema kusogea kwa miundombinu ya kijeshi ya NATO karibu na mipaka ya Urusi inaweka "tishio la moja kwa moja" kwa usalama wake na kwamba itaangalia mchakato wa kufanya na hakika utakuwa ni msumali na mwiba kwa upande wa shirikisho hilo akisisiiza kuwa utakuwa "mbaya sana."

Maneno haya ya Vladimir Putin yanajitokeza chini ya wiki baada ya Azimio la Mkutano wa Mkutano wa Brussels, ambayo ilielezea uamuzi uliofanywa katika Mkutano wa Bucharest wa 2008 "kwamba Georgia itakuwa mwanachama wa Muungano wa NATO.

Ukweli napenda sana kuwa na washirika wazuri kama Cuba maishani mambo yakienda kombo ukizungumza nae anakuelewa. Baada ya Missile crisis warusi waliondoka Cuba, na sasa mgogoro mkubwa unaendelea duniani wameamua kurudi tena Cuba na Wacuba wamewapokea na mikono miwili na jamaa wanafunga tena mitambo yao kuweza kum monitor Mmarekani pamoja.

Ukweli Putin ni kiongozi mwenye maono ya mabli na kutafakari kwa kina, endapo zisingekuwa busara za Putin kwa sasa dunia ingekuwa si sehemu salama hata kidogo, ila mara nyingi hutulia na kufanya maamuzi kwa mustakabali wa dunia. Mathalani wamarekani na washirika wake wawili wasijitambua wale Uingereza na Ufaransa walivyopiga Syria mwezi april angeamua kujibu basi dunia ingekuwa pabaya mpaka sasa

 

Attachments

  • Russia has restored Soviet military base in Cuba! U.S. is in madness!.mp4
    3.4 MB · Views: 31
Kwakweli heshima lazima irudi mmarekani lazima aone kizunguzungu amezoea kuteka nchi za wenzake na kuweka base sasa base ya mhasimu inasogea mlangoni na wanasema wapo tayari kwa vita na wanajiandaa kwa vita kama anavyofanya mmarekani
 
Heheee " haya yajayo " yanafurahisha zaidi kuliko hata yale ya Voda
 
Dunia imebadilika sana hivyo mataifa yenye nguvu si Urusi na Marekani pekee maana hata China imeinuka hivyo ulingo wa vita baridi umepata bondia mpya.
 
Dunia imebadilika sana hivyo mataifa yenye nguvu si Urusi na Marekani pekee maana hata China imeinuka hivyo ulingo wa vita baridi umepata bondia mpya.
Naona na India inanunua silaha kwa kasi kubwa sana kiasi kwamba ndani ya miaka kumi BRICS itakuwa na mataifa matatu yenye nguvu kubwa mno za kijeshi kwa maana ya Urus,China na India yenyewe achilia mbali Brazil na Afika Kusin. Nahisi Marekani na wenzake kuna kitu walijisahau wakati wa kusambaratika kwa uliokuwa muungano wa Kisoviet, walipaswa kwa namna ya pekee waiangamize Urus kijeshi na kiteknolojia ikiwa ni pamoja na ama kuwaua wanasayansi wa Urus au Kuwaiba wote lkn ona sasa story inavyo badilika kwa kasi.

Warus wanarudi kwa kasi mno ktk medani ya kijeshi na kiteknolojia kiasi kwamba wanaweza kukabiliana na Marekani katika uwanja wa medani jambo ambalo nilikuwa ndoto miaka ya 1990. Putin na viongozi wengi hasa ambao ni mazao ya Kisoviet ni watu hatari sana. Mifumo yao ni ya siri mno na ujanja-ujanja. So, Marekani inahitaji uturivu wa hali ya juu na viongozi makini haswai kuwadhibiti hawa jamaa. Kibaya zaidi hata post-soviet generation washaharibiwa na hawa viongozi nguli kama Putin,Lavrov,Ryabkov,Medvedev,Sechin,Ivanov kwa kuwataja wachache.

Kwa aina ya uongozi unabadilika-badilika wa Trump na has a usiotabirika watajikuta katika hari ambayo hawakuitarajia kutoka Moscow kibaya zaidi wana-transfer saba teknolojia yao kwa nchi nyingi jambo ambalo si la afya sana kwa Washington
 
Naona na India inanunua silaha kwa kasi kubwa sana kiasi kwamba ndani ya miaka kumi BRICS itakuwa na mataifa matatu yenye nguvu kubwa mno za kijeshi kwa maana ya Urus,China na India yenyewe achilia mbali Brazil na Afika Kusin. Nahisi Marekani na wenzake kuna kitu walijisahau wakati wa kusambaratika kwa uliokuwa muungano wa Kisoviet, walipaswa kwa namna ya pekee waiangamize Urus kijeshi na kiteknolojia ikiwa ni pamoja na ama kuwaua wanasayansi wa Urus au Kuwaiba wote lkn ona sasa story inavyo badilika kwa kasi.

Warus wanarudi kwa kasi mno ktk medani ya kijeshi na kiteknolojia kiasi kwamba wanaweza kukabiliana na Marekani katika uwanja wa medani jambo ambalo nilikuwa ndoto miaka ya 1990. Putin na viongozi wengi hasa ambao ni mazao ya Kisoviet ni watu hatari sana. Mifumo yao ni ya siri mno na ujanja-ujanja. So, Marekani inahitaji uturivu wa hali ya juu na viongozi makini haswai kuwadhibiti hawa jamaa. Kibaya zaidi hata post-soviet generation washaharibiwa na hawa viongozi nguli kama Putin,Lavrov,Ryabkov,Medvedev,Sechin,Ivanov kwa kuwataja wachache.

Kwa aina ya uongozi unabadilika-badilika wa Trump na has a usiotabirika watajikuta katika hari ambayo hawakuitarajia kutoka Moscow kibaya zaidi wana-transfer saba teknolojia yao kwa nchi nyingi jambo ambalo si la afya sana kwa Washington
Sasa na wewe unashauri. mmarekani angemsambaratisha mrrusi mapema kwanini? au mahaba juu ya mmarekani. ndio yamesababisha kuongea hivyo mrusi anamuonea nani? sio ukishashiba kande basi ni kubwabwaja tu.
 
Back
Top Bottom