AZSKY G6: Please share your experience

Paul S.S

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2009
Posts
6,408
Reaction score
3,269
Wakuu toka nimenunua hii kitu G6 kiukweli sijawahi kufurahia maisha kabisa na siku zinavyo sogea ndio hali inazidi kuwa mbaya,

Yafuatayo ni matatizo yanayoninyima raha na kuwa karaha
Mosi, kina kata kata sana kuliko hata Startimes

Pili chaneli kupotea potea kila mara

Niliambiwa tatizo ni net wakati hapa kwangu mnara ukianguka unaniangukia na kwenye pc napata speed ya hatari mitandao yote

Nikaambiwa labda dish dogo nikanunua kubwa futi 8 sijui kitu bado inazingua

Nikabadilisha lbn nikaweka sijui mnaita ya hd hadithi ipo pale pale

Nikaweka vifurushi kila aina ikiwemo kuweka vocha ya sh 20elf lakini kitu full kukata kata

Naanza kupata wasiwasi na uwezo wa G6 hizi sababu server hazina mashiko inaonyesha kila keys zikibadili basi ngoma zinapoload lazima itakatakata na kustuck

Pia inaonyesha hawa jamaa server zao zimeanza kuzidiwa na kadri watumiaji tunavyozidi hali inazidi kuwa mbaya wakati wa mechi za epl ngoma inapoteza poteza chaneli nk


Kusema kweli huduma zao ni asilimia kama 35 tu ya kile nilikuwa natarajia kutoka kwao


Labda kuna mahali nakosea au labda kunamtumiaji wa G6 anaipata vizuri tunaomba kushere uzoefu ili tupate tunachotarajia kwa kuwa wakweli na wawazi
Mnakaribishwa
 
umenena sawa kabisa kuna muda ipo poa kuna muda kinakata sana sana sana siku za mechi.... asilimia 98 umenena kweli kabsa
 
hiyo kitu ni kweli wakuu inabidi kuwavumilia ila kama ni mechi za soka nawashauli mfunge aljazeera sport sababu katika hiyo g6 huwa haigandi mala kwa mala iko vizuri sana. kwa wale wa xmaster wao wanapeta iko vizuri haigandi gandi hata ukicheki d*tv. najalibu kuweka cccam kwenye g6 nikifauli nitawajulisha wakuu ila japo cccam huwa ni ghalama kidogo hasa kwa server za uingeleza ndo zipo stable.
 
Mkuu munjy1 kuja pande hii utupe maelezo ya kueleweka maana hii kitu imekua kero sasa.
 
Last edited by a moderator:
Ndugu km unataka kula kama mwenye haki jisajili multichoice..kuwa mvulivu tu sie tulishazoea toka enzi za HAWK 7777 ndo maana kalaki na30 tuwazia kufanyie mambo mengne!!
 

pia nimesikia Xman G8 nayo haigandi gandi vp umekutana nayo na ni kweli wasemayo?
Pia kuna mtu kanambia Qsat Q13G na Q11G(same account with Xman G8) ziko poa huyu jamaa yuko Morrogoro kuna Mchina kanipa namba yake ili anipe experience lkn hajawa mwazi akifikiri mm ni mtu wa DSTV.

Prove this to me pls kama ume-come across hivi vi2
 

Nitajaribu kuweka hiyo eljazeera kisha nitaleta feedback
 
Ndugu km unataka kula kama mwenye haki jisajili multichoice..kuwa mvulivu tu sie tulishazoea toka enzi za HAWK 7777 ndo maana kalaki na30 tuwazia kufanyie mambo mengne!!

Mkuu natambua mwizi hawezi kula sawa na mwenye mali lakini sasa isiwe too much bana, kumbuka we pay for this kwa kutegemea angalau kupata kaunafuu na si karaha
 
kuna hii makitu inaitwa cccam ngoja wataalamu waje watujuze kidogo....!
 
Munanikatisha tamaa nina wazo la kununua hayo g6 .naomba ushauri
 
Munanikatisha tamaa nina wazo la kununua hayo g6 .naomba ushauri

kama huna haraka,vuta subira kwan wataalam wanasema kuna mnyama mwingne bora zaidi ya waliopo anafanyiwa uchunguzi akikaa sawa atawekwa hadharani!
Binafsi nna g6,naendlea nayo taratibu.
 
hivi vitu vilianza kufanya vizuri sana. lakini kwa sasa server zao zimezidiwa na wateja. wanauza dunia nzima sasa, kwa hiyo number of user imekuwa kubwa kuliko uwezo wa server zao. imekuja A+ hii ni kampuni tofauti na G1.G2...G6. hawa A+ wao havikati kabisa kama ilivyo G1 ya zamani.
ila nao hawa A+ watapopata wateja wengi ... tutegemee kama haya ya G6
 

mbona mi nina g2 na haikatikati sana.nahisi mitandao huko muliko inasumbua
 
mbona mi nina g2 na haikatikati sana.nahisi mitandao huko muliko inasumbua

Mkuu sijui kwa g2 kama ipo fresh
Lakini hii product yao mpya g6 inataka uvumilivu kuangalia hata kama una net ipo stable kiasi gani
 
Haya mavitu ni ovyo kabisa , najutia pesa nilizopoteza, kweli nmeamini bore ni gharama, nashauri kama hujanunua usinunue kabisa haya matakataka!
 
Haya mavitu ni ovyo kabisa , najutia pesa nilizopoteza, kweli nmeamini bore ni gharama, nashauri kama hujanunua usinunue kabisa haya matakataka!

angalia kidude chako inawezekana account yako ime-expire au huenda kuna technical problem ktk device yako,nashangaa unalalamika kifaa chako hakitingi wakati watu kadhaa nikiwemo mimi tunashuhudia maajabu ya ufanisi wa leo??
Mh weka waz tatzo lako usaidiwe,kuna wataalam kibao humu jf.
 
Haya mavitu ni ovyo kabisa , najutia pesa nilizopoteza, kweli nmeamini bore ni gharama, nashauri kama hujanunua usinunue kabisa haya matakataka!

Binafsi naona kama huna ubavu wa kumudu DSTV sio vibaya ukanunua hii G6 labda huko baadae itakuja kuwa stable.
Kama mwanzo ulikuwa unatumia DSTV na ukaamua kuachana nayo na kuitegemea hii hapo sikushauri maana hii sio mbadala wa DSTV kabisa na itakukera sana bora uwe bado hukawahi kutumia dstv

Kinachotia matumaini kuhusu product za AZSKY ni kuwa hata kama watatoa bidhaa mpya hawaitelekezi ile ya awali so tuwe na subira
 
yangu G6
kila asubuhi saa 1 mpaka saa 5inagoma.
hata saahii imegoma
 
Mkuu, acha kupotosha, inaonekana wewe experience yako katika kutumia hivi vi2 bado ni ndogo. Kwanza kabisa inatakiwa ujue kuwa tunaotumia hii huduma tunaiba tu ili nasi tuwe na angalau ya access ya DS nyumbani hivyo hatuwezi kuwa sawa na wale wanaokula kwa halali. Wengine sisi ni wapenzi wa free to air tv na hii receiver inatupa thamani ya receiver ya Mpeg 4 PLUS pay tvs. Hapo tu DS anasubiri kwa maana DS hauwezi kuitumia kupata free tvs zilizo nje wa muelekeo wa DS. Pia Premium packages ambayo yunaipata hapa DS inauzwa 135,000 wewe unasema bei ya receiver ni bora ununue DS? Ina maana hata bei ya installation ya DS huijui achilia mbali bei ya mwezi. Binafsi mara ya kwanza niliona nimepoteza lengo kwa kununua hii kitu, lakini nilichogundua kua ki2 kikubwa kinachotuangaisha ni stability ya net zetu. Mfano eneo ninaloishi mitandao yote inaspeed ya hatari isipokua Zantel hivyo akili yangu ilikua inanituma nitumie hiyo mitandao ku unlock pay tvs lakini sikupata matokeo mazuri, siku moja nikajaribu hii ambayo ndio slowest ndio imeniletea matokeo mazuri na hata kukatakata inachukua muda sana. Wengine wanasema kinakata kama startimes bahati mbaya mimi ninayo startimes ambayo inakatakata hiyo nimeshindwa kabisa kuitumia lakini hii ngoma ni masaa 24 maana mama yeye ni Magic swahili, Madogo cn na mimi mwenyewe ni ss mwanzo mwisho. Ni kweli napenda kuwe na marekebisho ili isikate kabisa tuzidi kuinjoy lakini sio kusema hamna kitu kabisa kwamba watu wamepoteza - fedha zao laaaa. Mkuu kuwepo nyumbani kwa sisi wapenzi wa mpira na kuchagua game unalolitaka sio jambo dogo, au kuangalia free tvs kutoka kila upande plus ds na Aj sio jambo dogo oh!
 
Mkuu natambua mwizi hawezi kula sawa na mwenye mali lakini sasa isiwe too much bana, kumbuka we pay for this kwa kutegemea angalau kupata kaunafuu na si karaha

Mkuu kuna mtu humu JF aliniuzia G2 haikuchukua hata mwezi ikakata mazima!alijitangaza weeee na mbwembwe nyiingi,(na ni maarufu sana humu JF kwenye ulimwengu wa Electronics) baada ya kununua na kukata namuuliza tatizo ni nin hajibu,kuanzia PM hajibu, Text Sms hajibu even my calls. Kwa kweli nimemnyamazia na kutomwanika just kulinda heshima yake,bt kama atasoma hapa (najua atajifahamu) afahamu alichofanya sio ustaarabu hata kidogo!
Kwa hivo kuanzia hapo wala sichangaamkii hivi vitu,kwa wanao amin na kuhangaika navo siwalaumu,bt mie nimeingia cost ya almost 600,000 (as nilinunua viwili) bt for nothing!kwa mnaotaka kujaribu good luck but kwa atakayependa ushaur wangu,then kuwa makini..!
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…