Azam TV inapeta, wengine wanachechemea

Azam TV inapeta, wengine wanachechemea

ImageUploadedByJamiiForums1436897476.468031.jpg
 
Ni ukweli mtupu. Hata Mimi nikipata kahela mwisho wa mwezi naondoa huu uchafu niliofunga naweka azam. Kweli wanastahili pongezi siwezi kila uchao kuanzalia habari kwa jirani hadi naonekana kero!! Mko wapi akina Charles Hilary?? Safi sana

Mkuu mimi nilishakitupa ghalani, maana nikisema store nakipa hadhi hicho startimes. Kwa kweli nina enjoy sana AzamTV salsa.
 
CEO wa AZAM TV.Tido Muhando anahojiwa muda huu yupo live akihojiwa na Patrick Nyembera.
Kwamba kuanzia Tarehe 10th August wataonyesha La Liga Liveeeee(Spanish League)

AZAM imepata haki miliki ya kuonyesha Mechi zoote za LA LIGA
TIDO,anasema kwamba alikutana na Uongozi wa La Liga DUBAI,na kuwaambie uwezo wa AZAM TV.
Na haikuwa kazi rahisi kupata Haki miliki kwa kuwa jopo la La Liga lazima lijue uwezo wa Kituo husika na ubora wake.
Ilichukua muda mrefu saana tangu wawasilishe maombI yao,hatimae yamekuwa

Amegusia tena kuhusu Arsenal TV,wapo kwenye mazungumzo hatua za mwisho na amesema kuna uwezekano wa kupata haki miliki ya kuonyesha mechi zao muda sio mrefu.

Manchester United na Liverpool wapo kwenye mazungumzo na yanaendelea vizuri.

Amegusia Tena Kuhusu EPL,wapo kwenye mazungumzo nao,Uongozi mkuu wa AZAM TV ulitoka na kuwafuata viongozi wa EPL UK.
TIDO anakiri kwamba nikazi kubwa zaidi kwa hili,lakini amesema watafika hatua nzuri tu.

AZAM TV ndio habari ya MJINI
 
Hapa tunazungumzia Azam na usawa wa kuonyesha mikutano yote ya vyama vya siasa kama alivyoahidi Tido, lakini naona wao na kijani tu.

CDM wanajificha hawatak kujulikana walipo-ha ha ha , waandishi walikuwa wanalalamika BBC-CDM hawana confidence
 
Mpaka kufungiwa ni zaidi ya Tsh 130,000 ila naona promo Tsh99,000
Haifiki mkuu,inategemea umeenda kwa wakala gani.
Maana mie niliongeza elfu 10 tu kumlipa mafuta ya gari fundi wao aje kunifungia,na fundi humlipi.
Ukitaka uende kwa Wakala mkuu na wanatambulika Rasmi,ila wapo wanaonunua na wao kuuza hapo ndio utauziwa bei na charges nyingi..

Kwa Dar,mawakala wapo kibao na wamedhibitishwa na Kampuni ya AZAM,sasa hapo ndio pa kwenda
 
Lambalamba anakimbiza mbaya..... kiukweli pamoja na ubora wa DSTV lakini walau mswahili mwenzetu anawaweka roho juu....siku hizi hata mabaa yanafunga DSTV na Azam tv ili wateja wasikose mechi yoyote muhimu......
 
Hongereni kwa hilo Azam ila wazee wa dezo msilalamike tu kuambiwa mlipie 50,000
 
Back
Top Bottom