Kumbuka, tunaishi katika siku za mwisho mwisho wa mfumo wa maisha tulionao 2Timotheo3:1-5. Ukiweza kuzitambua nyakati hizi, utakuwa na amani. Hutajiuliza sana maswali mengi, kwa kuwa utakuwa unaelewa nini kinachoendelea. Ishara nyingi ambazo Yesu kristo alizitabiri kuwa zitatokea katika siku za mwisho, tumezishuhudia. Kibaya ni kuwa, wengi wetu tumezaliwa NDANI ya hizi siku za mwisho, ambazo kulingana na unabii wa Biblia, zilianza rasmi mwaka 1914. Hivyo, kwa wengi inakuwa vigumu kuzitofautisha siku. Wanaona ni kawaida tu. Lakini kwa anayependa kuchunguza unabii, nyakati hizi ni tofauti saaanaaaaaa na nyakati za kabla ya 1914. Zinatimiza unabii kweli kweli.
Pia, unaweza kuona kuwa ni muda mrefu sana umesikia juu ya siku za mwisho. Kwa sbb, kwa ukuu wa Mungu, miaka 1,000 ni sawa na siku moja tu kwake. Jipime, katika miaka 1,ooo umeishi masaa mangapi kwa maoni ya Mungu??? Hata siku moja hujamaliza, wala mimi sijaimaliza.
Tafakari.