Ngwanakilala
JF-Expert Member
- Jun 25, 2011
- 774
- 1,456
Gazeti la Rai mwema toleo la 391la February 4, 2015 limemtaja kuwa perhaps ndie mwanadiplomasia anayeheshimika kuliko wote nchini Tanzania.
Pia limesema kuwa ni moja katiya watu wachache nchini Tanzania anayefaa kuwa Rais lakini hataki wala hana nia ya kuwa Rais.
Ni Muanzilishi wa idara ya Usalama wa taifa Tanzania na ni Mkurugenzi wa Kwanza
Mfahamu zaidi: WASIFU
Augustine Philip Mahiga (born28 August 1945) is a Tanzanian diplomat. He previously served as the PermanentRepresentative of Tanzania to the United Nations, and later as the UN Special Representativeand Head of the United Nations Political Office for Somalia.
EARLYHISTORY
In 1971, he earned a Bachelor of Arts (Education) at the Universityof East Africa in Dar es Salaam, Tanzania. That same year, Mahiga completed aMasters of Arts at the University of Toronto (U of T). He also received a PhDin International Relations in 1975 from the same institution. Mahiga is marriedand has children
CURRICULUMVITAE
DR. AUGUSTINE PHILIP MAHIGA
PERSONALDATA Name:Augustine Philip Mahiga
Dateof Birth: 28 August 1945 Nationality:Tanzanian
MaritalStatus: Married
EDUCATIONQUALIFICATIONS 1975Doctor of Philosophy (PhD) in International Relations, Universityof Toronto 1971Master of Arts (M.A.), University of Toronto, 1970 Bachelor of Arts withEducation (B.A. Ed.
Honors. University of East Africa, Dar-es-Salaam
SUMMARYOF WORK EXPERIENCE
2005 - Ambassador,Head of the Tanzania Delegation to the United Nations Security Council
2003 - Present - AmbassadorExtraordinary and Plenipotentiary,
presentPermanent Representative of the United Republic of Tanzania to the UnitedNations
2002 - 2003 UNHCR, Representative to Italy, Republic of Malta, Holy See andRepublic of San Marino.
1998 - 2002 UNHCR, Chief of Mission (Representative) in New Delhi,India.
1994 - 1998 Coordinator andDeputy Director of the Great Lakes Region of Africa Refugee Emergency Operationbased in Geneva.
1992 - 1994 UNHCR Chief ofMission (Representative) in
Monrovia, Liberia.
1993 Appointed bythe Government of the United Republic of Tanzania to the rank of Ambassadorwhile on secondment to UNHCR.
1989 - 1992 MinisterPlenipotentiary, Tanzania Permanent Mission to the United Nations in Geneva.
1977 - 1980 Director of Research andTraining, President?s Office, Dar-es-Salaam, Tanzania.
1975 - 1977 Senior Lecturer in International Affairs and Regional Cooperation, University ofDar-es-Salaam, Tanzania
PUBLICATIONS AND INTERNATIONAL CONFERENCE PAPERS
- Empowerment of Women and Millennium Development Goals in Empowerment of Women, Partners in Population and Development Publication, New York, 2004
- Forward to Refugees and the State Practices of Asylum and Care in India, 1947- 2000, Edited by Ranabir Samaddar, New Delhi, Sage Publishing, 2003
- Water Resources, Human Displacement and International Security (Paper presented to the Gorbachev Foundation Peace Conference, Rome, Italy, November 2002
- Demography Strategic Imperatives and Displacements in South Asia (Lecture delivered to the National Military Academy, New Delhi,India, 2001)
- Reconciling Refugee Protection and National Security(Paper presented to the University of Pune, Pune, India and Habitat Centre, New Delhi, India, 2001)
- Globalization and Forced Migrations (Lecture at the Press Club, Madras, India)
- International Response to the Post-Genocide Rwanda Emergency?, Reference document at Oxford University, Refugee Studies website
- Confidence Building Measures in Africa?, published by the United Nations Institute for Disarmament Research (UNIDIR)
- Pitfalls and Promises of East African Integration "TAAMULI" Journal of Political Science, University of Dar-es-Salaam
- Disarmament and Development in Africa (Paper presented to the Palme Commission Conference on Disarmament and Development, New Delhi, India,1986)
- Conflict Resolution and Security in Africa (Paper presented at a Conference on Conflict Resolution in Africa, Lome, Togo, 1989)
- Confidence Building Measures in Africa?, published by the United Nations Institute for Disarmament Research (UNIDIR)
=======
JUNI 10, 2015: Dkt. Mahiga achukua fomu kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
MWANADIPLOMASIA maarufu, Balozi Dk Augustine Mahiga ametangaza nia kukiomba Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumfikiria na hatimaye kupendekeza ili apate fursa ya kugombea nafasi ya Urais wa Tanzania.
Dk Mahiga pamoja na nia yake amekuja na vipaumbele vyake kuwa ni kuleta umoja, amani na maadili, kupambana na rushwa na ufisadi, kukuza uchumi na kuimarisha uhusiano wa kimataifa.
Akitangaza nia jana mbele ya waandishi wa habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO), alisema ameamua kuchukua hatua hiyo kwa kuwa ni haki yake, lakini pia amepata fursa ya kuielewa nchi yake, dira, uchumi, siasa na utamaduni wake na kuitangaza ndani na nje ya nchi.
“Ningependa kusimama na kugombea nafasi ya Urais wa Tanzania kupitia CCM katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu. Nimetafakari muda mrefu na nikafikia muafaka wa kujitosa katika kinyanganyiro hiki, naomba nifikiriwe na hatimaye kupendekezwa na kupata fursa ya kuongoza taifa hili,” alisema.
Vipaumbele vyake
Mwanadiplomasia huyo alibainisha kuwa akichaguliwa, jambo la kwanza litakuwa kuandaa miongozo ya nchi na kutekeleza ilani ya CCM kwa nguvu zote.
Balozi Mahiga, aliyeanza hotuba yake kwa kueleza wasifu wake wa elimu na mafanikio ya kazi zake mbalimbali alizofanya ndani na nje ya nchi, alisema akipata ridhaa kipaumbele chake cha kwanza ni kuimarisha misingi ya Taifa ambayo ni umoja, amani na maadili.
Alitaja vipaumbele vingine kuwa ni mkakati wa kuipeleka nchi kwenye uchumi wa kipato cha kati na kukuza uchumi kwa kupambana na umaskini, kukuza kilimo, viwanda, uchukuzi, na utalii.
Dk Mahiga, ambaye kabla ya kustaafu alikuwa mwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia na mkuu wa ofisi ya siasa za Somalia (UNPOS), alisema atashughulikia uboreshaji wa mfumo wa elimu, kuimarisha uhusiano na Jumuiya ya Kimataifa na kukabiliana na changamoto mpya za vitisho vya ugaidi na biashara ya dawa za kulevya.
Alifafanua kuwa kwa muda mrefu umoja wa nchi, umekuwa ukiyumbishwa na watu wachache wenye masilahi binafsi, hivyo atapambana nalo kwa karibu iwapo atapata fursa ya kuiongoza nchi baada ya kupitishwa na CCM.
“Umoja wetu ulikuwa ni nguvu pekee ya kumwondoa mkoloni, kupambana na udini, ukabila, ukanda na ndiyo uliofanikisha mapinduzi ya Zanzibar na kuanzisha Jamhuri ya Muungano Tanzania,” alisema Balozi Mahiga.
“Lakini sasa tumeanza kuona uadui, ukabila, ukanda na hata rika… mara hee wazee, mara vijana. Pia, tumeanza kuona watu wachache wanayumbisha Muungano wetu, umoja ukiyumba na amani itayumba.”
Kwa kutumia uzoefu wake katika kusuluhisha amani nchi za Afrika Magharibi na ukanda wa Maziwa Makuu, Balozi huyo alisema: “Nitasemea hilo kwa uchungu na nisingependa uvunjifu wa amani usitokee nchini.”
Alisema Tanzania inapitia katika kipindi kigumu kwa sababu za kiitikadi, hivyo njia pekee za kujinasua ni kutatua kero za Muungano, kuruhusu uwanja mpana na wa wazi wa ushiriki wa vyama vya siasa na kuimarisha taasisi za kidini, Serikali na asasi za kiraia.
“Nadhani hizi kero za Muungano zimejadiliwa na kupatiwa majawabu. Zikipatikana katika Katiba mpya zitawaridhisha Wazanzibari na watu wa Bara na kudumisha amani na umoja,” alisema.
Hata hivyo, alipoulizwa iwapo akipata urais atabadilisha Katiba Inayopendekezwa ili kutatua baadhi ya kero za Muungano zinazolalamikiwa ukiwamo Muundo wa Muungano, alijibu; “katika siasa kuna mambo mengi yanayoweza kutokea” na kwamba mchakato wa Katiba ni shughuli endelevu.
Pia, alisema iwapo atapata ridhaa hiyo, kuna ulazima wa kuufanya mfumo wa vyama vingi kuwa wa kidemokrasia zaidi. “Lazima tujifunze kuwa na utamaduni wa vyama vingi. Ushindani wa kisiasa usiwe mapambano na kuyumbisha amani na umoja,” alisema.
Kwa muda mwingi, Balozi Mahiga alikuwa akisisitiza maadili ya viongozi na nchi akisema kuwa yataimarishwa kwa kukuza uzalendo, uadilifu, uwajibikaji na ukweli. Alisema kwa kipindi kirefu maadili nchini yameanza kuporomoka, hivyo suala hilo halitakiwi lizungumziwe kirahisi, bali ni lazima livaliwe njuga
.
“Tusiogope kujikosoa, kukosolewa kuwa maadili yamemomonyoka na yanatakiwa kushughulikiwa na kuboreshwa. Jambo la haraka ni kupambana na udanganyifu, rushwa na ufisadi ambao kwa ujumla ni wizi tu,” alisema.
Alisema mapambano ya rushwa na ufisadi yanapaswa yafanyike katika chama na uchumi.
Atangaza vita dhidi ya ufisadi
“Siyo kwamba haya mambo ya uhujumu uchumi hayakuwapo, yalikuwapo tangu zamani… nakumbuka nilipokuwa Usalama wa Taifa pamoja na Marehemu (Waziri Mkuu wa zamani Edward Sokoine) tulipambana sana.
“Lakini sasa watu wachache ni wala rushwa na mafisadi, wakiachwa wanaweza kuliangamiza Taifa na ina madhara makubwa kiuchumi na kwa heshima ya Tanzania,” alisema.
Alisema kuna haja ya kufanya uratibu wa kupambana na ubadhirifu wa kisiasa ili kuliwezesha Taifa kuwa na mwelekeo mpya wa siasa usio wa kuuza au kununua kura na utu.
Balozi huyo pia aligusia suala la matumizi ya fedha kwenye uchaguzi akisema inabidi yawekewe ukomo.
“Lazima kuwe na kikomo cha kugombea nafasi mbalimbali na matumizi ya fedha. Chama kitoe fursa ya kugombea na kuchaguliwa kwa kila mtu… tusifike mahali uwezo wa kuchaguliwa ukawa mikononi mwa wenye fedha,” alisema.
“Kuwe na uwazi katika chaguzi ili usitengenezwe mwanya kati walionacho na wasionacho na matabaka siyo dhamira ya CCM.”
Kama ilivyokuwa kwa wagombea wengine waliotangulia, Balozi Mahiga alitumia muda mrefu kuzungumzia rushwa kwa kina akieleza kuwa ili kupambana na ufisadi wa kiuchumi atatangaza vita maalumu.
Alisema ufisadi ni kuliibia Taifa na vita hiyo ikitangazwa kama kampeni maalumu kama ilivyokuwa katika kuwezesha wanawake, mwelekeo imara wa taifa utapatikana.
Utekelezaji wa kukomesha ufisadi na uonevu utafanyika kwa kubadili mfumo wa Serikali na sheria ili kutoa haki kwa watu wote.
Ili kukuza uchumi, alisema: “Kuna haja ya kupambana na umaskini kwa kuwawezesha Watanzania wa kawaida kuongeza pato lao mifukoni na kumudu gharama za maisha.
“Pia, inatakiwa kuipa Serikali uwezo wa kutoa huduma muhimu kwa watu wote. Mkulima, mjasiriamali, mvuvi, mfanyakazi na wengineo ni lazima wazipate huduma bora kwa haki bila kununua.”
Alisema inatakiwa kuboresha mfumo wa kuendesha uchumi wa kuendesha soko huria na sekta binafsi ambao utatatua tatizo la ajira, masoko na uwekezaji.
Alisema iwapo sekta binafsi na serikali zitashirikiana kwa pamoja, zitafanya kazi ya kubaini mwelekeo wa Taifa wa uchumi na idadi ya watu kwa kuzingatia ongezeko la tatizo la ajira kwa vijana.
“Suala la kuwawezesha vijana liingizwe kwenye mfumo wa Serikali. Kila kiongozi ajiulize ubunifu wangu unanipeleka wapi kujibu changamoto za vijana,” alisema
Balozi Mahiga alieleza kuwa katika kilimo ataweka kipaumbele katika kutatua matatizo ya migogoro ya ardhi baina ya wafugaji na wakulima au wakulima na wakulima.
Alisema kuwa baada ya hapo ataandaa mfumo madhubuti wa kukuza kilimo kwa pamoja kwa kuboresha masoko, uhifadhi wa mbegu bora, na ardhi.
Katika ukuzaji wa viwanda, Balozi huyo aliyejinasibu kuwa alichangia zaidi kuwavutia wawekezaji wa kigeni, alisema atatoa fursa kwa wazawa na wageni kuchangia maendeleo hayo.
“Tutatengeneza mazingira bora ambayo wananchi watashiriki kikamilifu katika viwanda kutokana na mitaji itakayopatikana kwenye kilimo na biashara,” alisema.
“Kwa wawekezaji wa nje tutahakikisha tunawawekea mazingira rafiki ya kuwavutia waje kuwekeza… kwa sasa bado wawekezaji hao wanalalamika kuna vikwazo vinavyowafanya wengine washindwe na kuondoka,”
Pia, alidokeza kuwa katika sekta ya uchukuzi ataweka utaratibu maalumu wenye uwiano baina ya usafiri wa reli, barabara na majini ili visiathiriane.
Alisema suala la uchukuzi linahitaji mipango madhubuti na utekelezaji na iwapo itafanywa vizuri, barabara hazitaharibika wala malori hayatakosa mizigo.
Pia, alieleza kuinua utalii kwa kutunza vivutio vyote hususan vinavyotambuliwa na Umoja wa Mataifa kama urithi, ikiwamo kuzuia ujangili wa wanyamapori.
Balozi Mahiga alisema akiridhiwa na CCM na wananchi kugombea nafasi hiyo, atahakikisha anabadili mfumo wa elimu utakaojikita katika utaalamu na ufundi ili uendane na ushindani wa soko huria.
“Tuachane na ule msemo wa kwamba nimejenga shule 20 au 30 lazima tuangalie na ubora,” alisema.
Masuala yanayompa nguvu
Pamoja na kuonekana kutokuwa maarufu kwenye siasa za ndani, Balozi Mahiga alisema ana uzoefu mkubwa kwa kuitumikia nchi ndani na nje, jambo ambalo anaamini litasaidia kumvusha katika kinyang’anyiro hicho.
“Mchango wangu siyo kitu cha kuonekana mara moja lakini ni mkubwa sana katika maendeleo ya nchi hii,” alisema ofisa huyo mwandamizi wa zamani wa Idara ya Usalama wa Taifa. “Nikiwa katika uwakilishi wa Tanzania katika jumuiya za Kimataifa niliweza kuanzisha jukwaa la kuleta wawekezaji na watalii wengi na kuwezesha kuiweka nchi katika ramani… ni kitu ambacho hakipimiki,” alisema.
Plan B
Alipoulizwa endapo hatapitishwa na CCM kuwania urais atamuunga mkono mgombea gani, Balozi Mahiga alijibu kuwa licha ya kujitokeza makada wengi katika kinyang’anyiro hicho kwake anaona ni shule mpya.
“Kati ya wote tunaowania ni lazima atoke rais mmoja, hata viongozi wenzangu watajua kumbe kuna watu wenye uwezo wa kuongoza... kwa kuwa tunaendelea na mchakato siwezi kusema nani ntamuunga mkono… atakayepita tufanya kazi kama timu,” alisema.
Pia limesema kuwa ni moja katiya watu wachache nchini Tanzania anayefaa kuwa Rais lakini hataki wala hana nia ya kuwa Rais.
Ni Muanzilishi wa idara ya Usalama wa taifa Tanzania na ni Mkurugenzi wa Kwanza
Mfahamu zaidi: WASIFU
Augustine Philip Mahiga (born28 August 1945) is a Tanzanian diplomat. He previously served as the PermanentRepresentative of Tanzania to the United Nations, and later as the UN Special Representativeand Head of the United Nations Political Office for Somalia.
EARLYHISTORY
In 1971, he earned a Bachelor of Arts (Education) at the Universityof East Africa in Dar es Salaam, Tanzania. That same year, Mahiga completed aMasters of Arts at the University of Toronto (U of T). He also received a PhDin International Relations in 1975 from the same institution. Mahiga is marriedand has children
CURRICULUMVITAE
DR. AUGUSTINE PHILIP MAHIGA
PERSONALDATA Name:Augustine Philip Mahiga
Dateof Birth: 28 August 1945 Nationality:Tanzanian
MaritalStatus: Married
EDUCATIONQUALIFICATIONS 1975Doctor of Philosophy (PhD) in International Relations, Universityof Toronto 1971Master of Arts (M.A.), University of Toronto, 1970 Bachelor of Arts withEducation (B.A. Ed.
Honors. University of East Africa, Dar-es-Salaam
SUMMARYOF WORK EXPERIENCE
2005 - Ambassador,Head of the Tanzania Delegation to the United Nations Security Council
2003 - Present - AmbassadorExtraordinary and Plenipotentiary,
presentPermanent Representative of the United Republic of Tanzania to the UnitedNations
2002 - 2003 UNHCR, Representative to Italy, Republic of Malta, Holy See andRepublic of San Marino.
1998 - 2002 UNHCR, Chief of Mission (Representative) in New Delhi,India.
1994 - 1998 Coordinator andDeputy Director of the Great Lakes Region of Africa Refugee Emergency Operationbased in Geneva.
1992 - 1994 UNHCR Chief ofMission (Representative) in
Monrovia, Liberia.
1993 Appointed bythe Government of the United Republic of Tanzania to the rank of Ambassadorwhile on secondment to UNHCR.
1989 - 1992 MinisterPlenipotentiary, Tanzania Permanent Mission to the United Nations in Geneva.
1977 - 1980 Director of Research andTraining, President?s Office, Dar-es-Salaam, Tanzania.
1975 - 1977 Senior Lecturer in International Affairs and Regional Cooperation, University ofDar-es-Salaam, Tanzania
PUBLICATIONS AND INTERNATIONAL CONFERENCE PAPERS
- Empowerment of Women and Millennium Development Goals in Empowerment of Women, Partners in Population and Development Publication, New York, 2004
- Forward to Refugees and the State Practices of Asylum and Care in India, 1947- 2000, Edited by Ranabir Samaddar, New Delhi, Sage Publishing, 2003
- Water Resources, Human Displacement and International Security (Paper presented to the Gorbachev Foundation Peace Conference, Rome, Italy, November 2002
- Demography Strategic Imperatives and Displacements in South Asia (Lecture delivered to the National Military Academy, New Delhi,India, 2001)
- Reconciling Refugee Protection and National Security(Paper presented to the University of Pune, Pune, India and Habitat Centre, New Delhi, India, 2001)
- Globalization and Forced Migrations (Lecture at the Press Club, Madras, India)
- International Response to the Post-Genocide Rwanda Emergency?, Reference document at Oxford University, Refugee Studies website
- Confidence Building Measures in Africa?, published by the United Nations Institute for Disarmament Research (UNIDIR)
- Pitfalls and Promises of East African Integration "TAAMULI" Journal of Political Science, University of Dar-es-Salaam
- Disarmament and Development in Africa (Paper presented to the Palme Commission Conference on Disarmament and Development, New Delhi, India,1986)
- Conflict Resolution and Security in Africa (Paper presented at a Conference on Conflict Resolution in Africa, Lome, Togo, 1989)
- Confidence Building Measures in Africa?, published by the United Nations Institute for Disarmament Research (UNIDIR)
=======
JUNI 10, 2015: Dkt. Mahiga achukua fomu kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
MWANADIPLOMASIA maarufu, Balozi Dk Augustine Mahiga ametangaza nia kukiomba Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumfikiria na hatimaye kupendekeza ili apate fursa ya kugombea nafasi ya Urais wa Tanzania.
Dk Mahiga pamoja na nia yake amekuja na vipaumbele vyake kuwa ni kuleta umoja, amani na maadili, kupambana na rushwa na ufisadi, kukuza uchumi na kuimarisha uhusiano wa kimataifa.
Akitangaza nia jana mbele ya waandishi wa habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO), alisema ameamua kuchukua hatua hiyo kwa kuwa ni haki yake, lakini pia amepata fursa ya kuielewa nchi yake, dira, uchumi, siasa na utamaduni wake na kuitangaza ndani na nje ya nchi.
“Ningependa kusimama na kugombea nafasi ya Urais wa Tanzania kupitia CCM katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu. Nimetafakari muda mrefu na nikafikia muafaka wa kujitosa katika kinyanganyiro hiki, naomba nifikiriwe na hatimaye kupendekezwa na kupata fursa ya kuongoza taifa hili,” alisema.
Vipaumbele vyake
Mwanadiplomasia huyo alibainisha kuwa akichaguliwa, jambo la kwanza litakuwa kuandaa miongozo ya nchi na kutekeleza ilani ya CCM kwa nguvu zote.
Balozi Mahiga, aliyeanza hotuba yake kwa kueleza wasifu wake wa elimu na mafanikio ya kazi zake mbalimbali alizofanya ndani na nje ya nchi, alisema akipata ridhaa kipaumbele chake cha kwanza ni kuimarisha misingi ya Taifa ambayo ni umoja, amani na maadili.
Alitaja vipaumbele vingine kuwa ni mkakati wa kuipeleka nchi kwenye uchumi wa kipato cha kati na kukuza uchumi kwa kupambana na umaskini, kukuza kilimo, viwanda, uchukuzi, na utalii.
Dk Mahiga, ambaye kabla ya kustaafu alikuwa mwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia na mkuu wa ofisi ya siasa za Somalia (UNPOS), alisema atashughulikia uboreshaji wa mfumo wa elimu, kuimarisha uhusiano na Jumuiya ya Kimataifa na kukabiliana na changamoto mpya za vitisho vya ugaidi na biashara ya dawa za kulevya.
Alifafanua kuwa kwa muda mrefu umoja wa nchi, umekuwa ukiyumbishwa na watu wachache wenye masilahi binafsi, hivyo atapambana nalo kwa karibu iwapo atapata fursa ya kuiongoza nchi baada ya kupitishwa na CCM.
“Umoja wetu ulikuwa ni nguvu pekee ya kumwondoa mkoloni, kupambana na udini, ukabila, ukanda na ndiyo uliofanikisha mapinduzi ya Zanzibar na kuanzisha Jamhuri ya Muungano Tanzania,” alisema Balozi Mahiga.
“Lakini sasa tumeanza kuona uadui, ukabila, ukanda na hata rika… mara hee wazee, mara vijana. Pia, tumeanza kuona watu wachache wanayumbisha Muungano wetu, umoja ukiyumba na amani itayumba.”
Kwa kutumia uzoefu wake katika kusuluhisha amani nchi za Afrika Magharibi na ukanda wa Maziwa Makuu, Balozi huyo alisema: “Nitasemea hilo kwa uchungu na nisingependa uvunjifu wa amani usitokee nchini.”
Alisema Tanzania inapitia katika kipindi kigumu kwa sababu za kiitikadi, hivyo njia pekee za kujinasua ni kutatua kero za Muungano, kuruhusu uwanja mpana na wa wazi wa ushiriki wa vyama vya siasa na kuimarisha taasisi za kidini, Serikali na asasi za kiraia.
“Nadhani hizi kero za Muungano zimejadiliwa na kupatiwa majawabu. Zikipatikana katika Katiba mpya zitawaridhisha Wazanzibari na watu wa Bara na kudumisha amani na umoja,” alisema.
Hata hivyo, alipoulizwa iwapo akipata urais atabadilisha Katiba Inayopendekezwa ili kutatua baadhi ya kero za Muungano zinazolalamikiwa ukiwamo Muundo wa Muungano, alijibu; “katika siasa kuna mambo mengi yanayoweza kutokea” na kwamba mchakato wa Katiba ni shughuli endelevu.
Pia, alisema iwapo atapata ridhaa hiyo, kuna ulazima wa kuufanya mfumo wa vyama vingi kuwa wa kidemokrasia zaidi. “Lazima tujifunze kuwa na utamaduni wa vyama vingi. Ushindani wa kisiasa usiwe mapambano na kuyumbisha amani na umoja,” alisema.
Kwa muda mwingi, Balozi Mahiga alikuwa akisisitiza maadili ya viongozi na nchi akisema kuwa yataimarishwa kwa kukuza uzalendo, uadilifu, uwajibikaji na ukweli. Alisema kwa kipindi kirefu maadili nchini yameanza kuporomoka, hivyo suala hilo halitakiwi lizungumziwe kirahisi, bali ni lazima livaliwe njuga
.
“Tusiogope kujikosoa, kukosolewa kuwa maadili yamemomonyoka na yanatakiwa kushughulikiwa na kuboreshwa. Jambo la haraka ni kupambana na udanganyifu, rushwa na ufisadi ambao kwa ujumla ni wizi tu,” alisema.
Alisema mapambano ya rushwa na ufisadi yanapaswa yafanyike katika chama na uchumi.
Atangaza vita dhidi ya ufisadi
“Siyo kwamba haya mambo ya uhujumu uchumi hayakuwapo, yalikuwapo tangu zamani… nakumbuka nilipokuwa Usalama wa Taifa pamoja na Marehemu (Waziri Mkuu wa zamani Edward Sokoine) tulipambana sana.
“Lakini sasa watu wachache ni wala rushwa na mafisadi, wakiachwa wanaweza kuliangamiza Taifa na ina madhara makubwa kiuchumi na kwa heshima ya Tanzania,” alisema.
Alisema kuna haja ya kufanya uratibu wa kupambana na ubadhirifu wa kisiasa ili kuliwezesha Taifa kuwa na mwelekeo mpya wa siasa usio wa kuuza au kununua kura na utu.
Balozi huyo pia aligusia suala la matumizi ya fedha kwenye uchaguzi akisema inabidi yawekewe ukomo.
“Lazima kuwe na kikomo cha kugombea nafasi mbalimbali na matumizi ya fedha. Chama kitoe fursa ya kugombea na kuchaguliwa kwa kila mtu… tusifike mahali uwezo wa kuchaguliwa ukawa mikononi mwa wenye fedha,” alisema.
“Kuwe na uwazi katika chaguzi ili usitengenezwe mwanya kati walionacho na wasionacho na matabaka siyo dhamira ya CCM.”
Kama ilivyokuwa kwa wagombea wengine waliotangulia, Balozi Mahiga alitumia muda mrefu kuzungumzia rushwa kwa kina akieleza kuwa ili kupambana na ufisadi wa kiuchumi atatangaza vita maalumu.
Alisema ufisadi ni kuliibia Taifa na vita hiyo ikitangazwa kama kampeni maalumu kama ilivyokuwa katika kuwezesha wanawake, mwelekeo imara wa taifa utapatikana.
Utekelezaji wa kukomesha ufisadi na uonevu utafanyika kwa kubadili mfumo wa Serikali na sheria ili kutoa haki kwa watu wote.
Ili kukuza uchumi, alisema: “Kuna haja ya kupambana na umaskini kwa kuwawezesha Watanzania wa kawaida kuongeza pato lao mifukoni na kumudu gharama za maisha.
“Pia, inatakiwa kuipa Serikali uwezo wa kutoa huduma muhimu kwa watu wote. Mkulima, mjasiriamali, mvuvi, mfanyakazi na wengineo ni lazima wazipate huduma bora kwa haki bila kununua.”
Alisema inatakiwa kuboresha mfumo wa kuendesha uchumi wa kuendesha soko huria na sekta binafsi ambao utatatua tatizo la ajira, masoko na uwekezaji.
Alisema iwapo sekta binafsi na serikali zitashirikiana kwa pamoja, zitafanya kazi ya kubaini mwelekeo wa Taifa wa uchumi na idadi ya watu kwa kuzingatia ongezeko la tatizo la ajira kwa vijana.
“Suala la kuwawezesha vijana liingizwe kwenye mfumo wa Serikali. Kila kiongozi ajiulize ubunifu wangu unanipeleka wapi kujibu changamoto za vijana,” alisema
Balozi Mahiga alieleza kuwa katika kilimo ataweka kipaumbele katika kutatua matatizo ya migogoro ya ardhi baina ya wafugaji na wakulima au wakulima na wakulima.
Alisema kuwa baada ya hapo ataandaa mfumo madhubuti wa kukuza kilimo kwa pamoja kwa kuboresha masoko, uhifadhi wa mbegu bora, na ardhi.
Katika ukuzaji wa viwanda, Balozi huyo aliyejinasibu kuwa alichangia zaidi kuwavutia wawekezaji wa kigeni, alisema atatoa fursa kwa wazawa na wageni kuchangia maendeleo hayo.
“Tutatengeneza mazingira bora ambayo wananchi watashiriki kikamilifu katika viwanda kutokana na mitaji itakayopatikana kwenye kilimo na biashara,” alisema.
“Kwa wawekezaji wa nje tutahakikisha tunawawekea mazingira rafiki ya kuwavutia waje kuwekeza… kwa sasa bado wawekezaji hao wanalalamika kuna vikwazo vinavyowafanya wengine washindwe na kuondoka,”
Pia, alidokeza kuwa katika sekta ya uchukuzi ataweka utaratibu maalumu wenye uwiano baina ya usafiri wa reli, barabara na majini ili visiathiriane.
Alisema suala la uchukuzi linahitaji mipango madhubuti na utekelezaji na iwapo itafanywa vizuri, barabara hazitaharibika wala malori hayatakosa mizigo.
Pia, alieleza kuinua utalii kwa kutunza vivutio vyote hususan vinavyotambuliwa na Umoja wa Mataifa kama urithi, ikiwamo kuzuia ujangili wa wanyamapori.
Balozi Mahiga alisema akiridhiwa na CCM na wananchi kugombea nafasi hiyo, atahakikisha anabadili mfumo wa elimu utakaojikita katika utaalamu na ufundi ili uendane na ushindani wa soko huria.
“Tuachane na ule msemo wa kwamba nimejenga shule 20 au 30 lazima tuangalie na ubora,” alisema.
Masuala yanayompa nguvu
Pamoja na kuonekana kutokuwa maarufu kwenye siasa za ndani, Balozi Mahiga alisema ana uzoefu mkubwa kwa kuitumikia nchi ndani na nje, jambo ambalo anaamini litasaidia kumvusha katika kinyang’anyiro hicho.
“Mchango wangu siyo kitu cha kuonekana mara moja lakini ni mkubwa sana katika maendeleo ya nchi hii,” alisema ofisa huyo mwandamizi wa zamani wa Idara ya Usalama wa Taifa. “Nikiwa katika uwakilishi wa Tanzania katika jumuiya za Kimataifa niliweza kuanzisha jukwaa la kuleta wawekezaji na watalii wengi na kuwezesha kuiweka nchi katika ramani… ni kitu ambacho hakipimiki,” alisema.
Plan B
Alipoulizwa endapo hatapitishwa na CCM kuwania urais atamuunga mkono mgombea gani, Balozi Mahiga alijibu kuwa licha ya kujitokeza makada wengi katika kinyang’anyiro hicho kwake anaona ni shule mpya.
“Kati ya wote tunaowania ni lazima atoke rais mmoja, hata viongozi wenzangu watajua kumbe kuna watu wenye uwezo wa kuongoza... kwa kuwa tunaendelea na mchakato siwezi kusema nani ntamuunga mkono… atakayepita tufanya kazi kama timu,” alisema.