August 12: Siku ya vijana kimataifa, kuna mengi vijana kama nguvu ya taifa na mabadiliko hupitia

Ryan Herman

Member
Jul 26, 2019
42
46
Kila tarehe ya 12 August ni siku ya vijana kimataifa. Kuna mambo mengi ambayo vijana kama nguvu ya taifa na mabadiliko hupitia.

1. Ukosefu wa ajira. Je ni nini kifanyike kuwakwamua vijana kwenye janga hili? Jambo la kusema vijana wajiajiri je ni kweli kuna mazingira wezeshi ya vijana kujiajiri? Kujiajiri ni kuwa na kiasi cha fedha cha kuanza nacho.

Pia wapo wanaomba ajira sehemu mbalimbali na kuambiwa wawe na uzoefu(experience) ya miaka3 na zaidi. Huu uzoefu wanapata wapi ilihali ndio wametoka vyuoni au hata ngazi yoyote ya elimu.

2. Ukuaji wa matumizi ya mitandao ya kijamii. Ni kweli vijana wananufaika na mitandao ya kijamii au ndio kuharibikiwa?
Mitandao ya kijamii husaidia kujifunza mambo mapya hivyo elimu zaidi inahitajika kwa vijana kuhusu matumiz chanya ya mitandao ya kijamii.

3. Afya na elimu.

Hivi ni vitu viwili muhimu kwa vijana kujua au kivipata kama huduma. Vijana wanapaswa kujua afya zao hususani magonjwa yanayoweza kuwaathiri katika ukuaji wao. Elimu juu ya magonjwa inahitajika zaidi hasa magonjwa ya zinaa na yale yanayoweza kuepukika kwa kufata ushauri wa wataalamu.

Elimu ya ujuzi pia inahitajika sio kumaliza elimu za makaratasi na kukaa tu.

4. Matumizi ya madawa ya kulevya.

Hili ni tatizo kubwa kwa vijana ila wanapata msaada gani kuhakikisha wanaweza kukwepa hili tatizo? Kuanzia ngazi ya familia mpaka jamii vijana wasaidiwe kujua matatizo na athari za madawa ya kulevya.

Mambo ni mengi ya kuzungumza na maswali ya kujiuliza kuhusu vijana.

#Happy International Youth Day
 
Siku ya Kimataifa ya Vijana huadhimishwa Agosti 12 kila mwaka. Ilianzishwa na Umoja wa Mataifa (UN) mwaka 2000 na lengo lake ni kutazama masuala mbalimbali yanayowahusu vijana

Siku ya Vijana hutoa nafasi ya kusherehekea harakati, vitendo na sauti za vijana. Vilevile ni fursa kwa Serikali na taasisi nyingine kuangalia kwa karibu yale yanayowagusa vijana moja kwa moja.

Siku hii hulenga kuonesha umuhimu wa vijana sio tu kwa kizazi kijacho bali kama nguvu itakayoleta mabadiliko. Mwaka huu, UN ilizindua kampeni ya #31DaysOfYouth ambayo inasherehekea vijana kwa mwezi mzima wa Agosti.

Kaulimbiu ya 2020 ni: "Ushiriki na ushirikishwaji wa vijana katika masuala ya kitaifa na kimataifa"

===

1597213717488.png

International Youth Day was designated by the United Nations (UN) in the year 1999, in an attempt to raise awareness regarding the cultural and legal issue concerning youth. The first IYD was observed on 12 August 2000 and has been observed annually ever since. In 1999, the General Assembly endorsed the recommendation made the ‘World Conference of Ministers Responsible for Youth’, and subsequently International Youth Day came to be celebrated annually.

This day is meant to signify and highlight the importance of young people, not just as a future generation, but also as the current driving force of change in the world. Various activities like concerts, workshops, cultural events and meetings are organised to engage the youth and in order to bring their voices, actions, and initiatives to the mainstream. This year, due to the coronavirus pandemic, the UN is commemorating IYD with a podcast-style discussion that will be hosted by the youth for the youth.

Each year, the observance of International Youth Day is marked with a theme, relevant to the times. The theme for 2020 is ‘Youth Engagement for Global Action’, and this has never been of more significance, than during the current conditions. The theme seeks to shed light on “the ways in which the engagement of young people at the local, national and global levels is enriching national and multilateral institutions and processes.” It highlights the importance of the influence that youth can have over where the future is headed and how their political and social involvement can aid in creating better, more sustainable policies for the world as a whole.

It is also important to note that the current challenges that humanity is facing can only be tackled with global action. From the Covid-19 pandemic that has brought the world to a standstill, to the Black Lives Matter Movement – the youth, globally, is unabashedly representing their ideologies and beliefs for better living and societal conditions.

With internet effectively joining every single person on earth in an expansive digital space, the call for global action is easily heard and answered by the youth all over the world. At this point in history they can literally ‘start a revolution from their beds.’

In observance of the day, the UN has launched a social media campaign, #31DaysOfYouth, that is celebrating young people all throughout the month of August, leading up to and following International Youth Day. It is meant to spread awareness and initiate conversations surrounding ‘Youth Engagement for Global Action’.
 
Mpango wa serikali ya Magufuli kwa vijana hususan suala la ajira ukoje?
 
Back
Top Bottom