Frank Wanjiru
JF-Expert Member
- Apr 12, 2012
- 24,706
- 44,066
Baba mmoja huko MBAGALA Charambe Njia Panda Nzassa Jana jioni amemchinja Mtoto wake wa kumzaa na kumuua but cha kushangaza Wananchi wenye hasira kali wakamchinja na kutenganisha kichaa na kiwiliwili bila kumuhoji Baba huyo Sababu ya kuchinja mtoto wake.
=========================================================
=========================================================
Mwalimu wa madrasa ya Ali Munawar,
ustaadhi Mohamed Ngulanjwa (36) wa
Mbagala Mianzini jijini Dar es Salaam,
ameuawa baada ya kumchinja mwanafunzi
wake.
Ustaadhi huyo aliyekuwa mwalimu wa
madrasa na shule ya awali ya Ali Munawar,
alimchinja mwanafunzi huyo jana saa 12.10
jioni kwenye eneo la madrasa baada ya
kutenganisha kichwa na kiwiliwili
Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa
Temeke, Jonathan Shana, akizungumzia
mauaji hayo , alisema tukio hilo la kinyama,
lilishuhudiwa na wananchi waliomuua
ustadhi huyo.
Alisema baada ya mwalimu kumuua
mwanafunzi wake wa kiume alichukua kisu
alichotumia pamoja na msahafu na kukimbia.
"Ilidaiwa kuwa alimchukua mtoto huyo ,
kumlaza chini kisha kumchinja kwa
kutenganisha kichwa na kiwiliwili na
kutelekeza vipande vya mwili wake kwenye
varanda," alisema Kamanda Shana.
Baada ya mauaji hayo mtuhumiwa alianza
kukimbia lakini wananchi walimvamia na
kumshambulia kwa mawe na kila silaha
iliyokuwa karibu na kumuua papo hapo.
Shana alieleza kuwa polisi walifika eneo la
tukio na kuchukua maiti hizo na kuzipeleka
hospitali ya Temeke.
Hata hivyo alisema jina la mtoto huyo
mwenye umri kati ya miaka 10- 12
halikufahamika na polisi inaendelea na
uchunguzi.
Nipashe J'pili