..........atoke........asitoke

..........atoke........asitoke

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,138
Yanasemwa mambo mbalimbali kumhusu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda. Ni juu ya hatma yake kama Mkuu wa Mkoa kufuatia sakata lake la makontena yanayoshikiliwa na TRA ambayo yatapigwa mnada kesho. Wapo wanaosema kuwa huu sasa ni mwisho wake kama mkuu wa mkoa na atatumbuliwa. Wapo wanaosema kuwa atabakia kuwa mkuu wa mkoa na atabakia alivyo.

Baada ya jana Mhe Rais kuvunja ukimya na kuweka nukta juu ya sakata hilo akiwa Wilaya ya Chato mkoani Geita, kila mwananchi aliyeweza kusema amesema lake. Wengi, lakini, wanatamani kuona mwisho wa Makonda ukifika. Wanachagiza mwisho wake na 'kashfa' zake mbalimbali mpya na za zamani kama kuwa na 'utajiri wa kutisha' na hata kumiliki Ardhi ya ukubwa wa viwanja 15 vya mpira mkoani Dodoma-kwa mujibu wa gazeti la Sauti Kubwa la jana.

Kiuhalisia na katika Maisha yetu ya kitanzania, ni nadra sana wananchi kutakiana laana au kuanguka. Mara nyingi, hata kinafiki, hutakiana mema na ya neema. Kutakiwa mabaya waziwazi si jambo la mchezo. Ni jambo la kuogofya na kutoa mafunzo kwa wananchi wote watakaobahatika kuwatumikia wengine. Inaonyesha jinsi wanachi walivyochoka na kuchoshwa na uwepo wa kiongozi katika nafasi aliyonayo.

Viongozi wetu wa Serikali na vyama tunawapenda na kuwaheshimu sana. Tunawapenda kwakuwa ndiyo Mungu aliotujaalia na kutubariki kuwa nao kwa muda husika. Tunawasikiliza na kuwafuata kutokana na wanachotuelekeza. Tunawapigania na kuwatetea; tunawaombea na kuwatakia mema kwa kiasi kikubwa. Lakini, kutokana na ubinaadamu wetu, kwa kiasi hichohicho huwatakia mabaya na kutamani kuona mwisho wao. Pale wanapotuonyesha kuwa hatukuwa tumepata ila tulipatikana.

Nasema, Makonda atoke au asitoke katika nafasi ya mkuu wa mkoa au nyingineyo, tunalo jambo kubwa la kujifunza. Viongozi, kama walivyo wananchi wao, wanapaswa kujinyenyekeza. Hata wakisema na kusema kwa staha, busara na hekima, mamlaka na madaraka yao hubakia na kuimarika. Kuheshimu na kujali unaowaongoza huongeza ulinzi, maombi, utetezi na baraka kupitia shukrani. Hata minara hujengwa kwa ukumbusho wa mema isipokuwa katika nchi za kidikteta kama kwa Marehemu Sadam Hussein wa Iraq
 
Suala la kuuliza atoke asitoke ni suala lisilo na maana, kutoka kwa Bashite ilikuwa ni phenomenon ya muda mrefu, tangu mwaka jana, hili jambo halikuwa ni jambo la kufikiria, Mhe. Hakutakiwa kwa kesi yake ya vyeti bado awepo madarakani, achana na hilo tuu, tazama ishu ya clouds, ila kaka si unajua tupo Afrika? yale mambo hayana nafasi tena kwenye vichwa vya watu ssa hivi.

Suala la makontena ni suala bichi sanal, huenda akalipa kodi, kwani si ndio suala tuu hilo?
ok, lets wait
 
Simkubali DAB ila itakua vema endapo akipewa nafasi nyingine,mji wa Dar unachangamoto nyingi sana kiutendaji mtumishi kuwa na conflict of interest jambo la kawaida inatokea mara kwa mara,mtu anakufata kwa lengo la urafiki kumbe ana hiden agenda.
 
Achen kupoteza Nguvu aiseee. Mnajichosha....jamaaa hatokaaa kutolewa hata kwa mbinde hatokaaaaaaa.

Vyet havikumuondosha sembuse ili aloambiwa alipe kodi??? Sana sana watu wajiandae kuumia

*I shall kindly Knee to leave my Pride*
 
Kiuhalisia na katika Maisha yetu ya kitanzania, ni nadra sana wananchi kutakiana laana au kuanguka. Mara nyingi, hata kinafiki, hutakiana mema na ya neema. Kutakiwa mabaya waziwazi si jambo la mchezo. Ni jambo la kuogofya na kutoa mafunzo kwa wananchi wote watakaobahatika kuwatumikia wengine. Inaonyesha jinsi wanachi walivyochoka na kuchoshwa na uwepo wa kiongozi katika
Mkuu sikubaliani na wewe katika suala la kutakiana mema nchi hii. Watanzania wengi kwa takriban miaka 5 na zaidi ni watu wanaopenda sana kuona anguko la wenzao. Nitakupa mifano michache.
1. Wakati wa sakata la Escrow katika ukumbi wa Diamond Jubilee. Mhe. Kikwete alitangaza kumuengua aliyekuwa waziri wa Ardhi Prof. Tibaijuka katika nafasi yake. Mamia ya waliokwepo ukumbini walipiga nderemo na vigelegele kama vile Tibaijuka ndiye aliekwenda BoT na kuiba pesa. Watu walikuwa wanafurahia anguko lake !
2. Wakati Mhe. Magufuli akimtumbua aliyekuwa mkurugenzi wa Jiji, marehemu Kabwe. Aliuliza wananchi waliokuwa kwenye mkutano wake kama amtumbue au la. Umati ule kwa uwingi wake walipaza sauti atumbuliwe mithini ya wale wayahudi walivyokuwa wanamtaka Yesu asulubiwe! Naye Rais akamtumbua. Watu wale walikuwa wanafurahia anguko la Kabwe. Hiyo ni mifano miwili tu lakini list iko ndefu mkuu.
Itoshe tu kusema kuwa watanzania walio wengi wanapenda na kufurahia sana anguko la wenzao.
 
Niswali LA kujiuliza mda huu nikwanini huyu jamaa bado yupo oficin alitakiwa awepo keko akinyea debeee na asipokwenda awamu hii basi ajue awamu ijayo atakwenda tuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu sikubaliani na wewe katika suala la kutakiana mema nchi hii. Watanzania wengi kwa takriban miaka 5 na zaidi ni watu wanaopenda sana kuona anguko la wenzao. Nitakupa mifano michache.
1. Wakati wa sakata la Escrow katika ukumbi wa Diamond Jubilee. Mhe. Kikwete alitangaza kumuengua aliyekuwa waziri wa Ardhi Prof. Tibaijuka katika nafasi yake. Mamia ya waliokwepo ukumbini walipiga nderemo na vigelegele kama vile Tibaijuka ndiye aliekwenda BoT na kuiba pesa. Watu walikuwa wanafurahia anguko lake !
2. Wakati Mhe. Magufuli akimtumbua aliyekuwa mkurugenzi wa Jiji, marehemu Kabwe. Aliuliza wananchi waliokuwa kwenye mkutano wake kama amtumbue au la. Umati ule kwa uwingi wake walipaza sauti atumbuliwe mithini ya wale wayahudi walivyokuwa wanamtaka Yesu asulubiwe! Naye Rais akamtumbua. Watu wale walikuwa wanafurahia anguko la Kabwe. Hiyo ni mifano miwili tu lakini list iko ndefu mkuu.
Itoshe tu kusema kuwa watanzania walio wengi wanapenda na kufurahia sana anguko la wenzao.
Ili uwe mchawi haihitaji kuwa na matunguli
1 wivu
2 chuki
3 rohombaya
Hao ndiyo watanzania rohombaya mwanzo mwisho
 
Makonda ndiye waziri wenu mkuu baada ya 2020. Mnavyonyamazia manunuzi ya madiwani na wabunge ni kuwa baba na mtoto wanajijengea himaya.

Kuna uvumi kuwa makontena 36 yalikuwa ni kwa hoteli ya baba huko chattel kingdom na mtoto ndiye mratibu na mwenye siri zote za baba. Wakutumbuliwa yuko wapi?
Baba ana hoteli yenye presidential suites 16, chumba cha bei ya chini kabisa ni 180,000. Msafara wa baba huwa na watu 100 ambao wanalala kwenye hoteli hiyo kwa gharama za kodi zetu.

Wananchi wa kawaida waliozoea kupata rizki kwa uvuvi Ziwa Victoria wamekazwa kumbe sababu ni kuwa baba anajenga kiwanda cha kusindika samaki na anataka samaki wawe wa kubwa kiwanda kiki anza kuzakisha how selfish.
 
Back
Top Bottom