Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 359,880
- 828,445
kwenye ulimwengu wa vipimo kuna ujazo mbalimbali kama robo nusu na kitu kamili nk.. nusu mbili hutengeneza kitu kamili robo mbili hutengeneza nusu moja
Kuna kamchezo ukimtuma mtu asiye mwaminifu akuletee kitu kinachohusika na vipimo kupiga bao! Ukimtuma kilo moja yeye ataleta nusu na robo.
Duniani tuna imani mbalimbali kuanzia zinazoabudu Mungu mmoja,miungu vitu vinavyoonekana, hata masanamu... kwenye hizi imani kuna mitifuano na mikanganyiko mingi tuu..lakini kiboko ya imani zote ni hii isiyomwamini Mungu mmoja
Jaribu kumuuliza atheist yeyote kwanini huamini katika Mungu atakwambia kwakuwa hajawahi kumuona! Ila muulize kama alishawahi kuiona akili yake au roho yake...hatakupa jibu moja na la moja kwa moja
Hii ni imani isiyotimia isiyojua dhima yake mwanzo wake wala muktadha wa nini inasimamia
Ni imani chongo yenye kengeza barobaro...ikiamini isichokiamini..ikifuata isichokijua
Je atheism ni;
Kuabudu miungu?
Kuabudu shetani?
Kuabudu masanamu?
Kuabudu vitu ?
Ama kutoabudu chochote?
Kila imani ina maelezo fulani kwenye chochote na kila swali lina jibu lake tusiiweke sayansi kwenye kundi la imani..hili ni Somo kama masomo mengine
Kutoamini chochote ni mkanganyiko tu wa akili kwakuwa mwisho wa siku utajikuta unaangukia kwenye imani yoyote japo kwa kificho na imani ya kutoamini chochote ni imani isiyotimia