Usiku wa Oct 31,2025 nilikuwa nachati na Mkuu wa Mkoa fulani ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Mkoa ule,tulikuwa tunajaribu "kudigest" kujua nini hasa kimetokea na nani hasa alitufikisha katika matukio yale ya Oct 29 na kuendelea.
Aliyoniambia Mkuu wangu yule niliogopa,nikasema hata huyu anaweza kufanya haya?Ndio maana nasema tu je,niweke wapi sura yangu kesho kuelekea kutangazwa kwa ripoti ya Ex-Jaji Mkuu Chande.
Kwa kifupi kuna watu watatajwa na ripoti ya kesho na Watanzania hawatoamini.Na ndio hapo watanzania wengi watajua ukweli kwamba kwanini hawa jamaa walikuwa wanaipinga hii ripoti.
Cha kushangaza zaidi kuna KANISA moja kubwa hapa Nchini lilitumia eneo lake kama uwanja wa kupanga matukio ya Oct 29.
Kesho ndio Watanzania wataweza "kuconnect dots"kwamba kwanini baadhi ya watu fulani fulani waliendelea kuishambulia Serikali mitandaoni hata baada ya Oct 29 mpaka leo.
Yule Mzee wa "Freka Fyeka Fyeka" kama namuona huko alipo.
Dah,October 29 ilikuwa na SIRI kubwa sana na bila Tume ya Ex-Jaji Mstaafu Chande Watanzania wengi tungekuwa gizani.
Kuna kijana mmoja mfuasi wa KANISA la Fyeka Fyeka Fyeka Mkoa fulani alipokamatwa simu yake ilikutwa "anachat" na KIongozi wa KANISA HILO MKOA fulani.
Walichokuwa wanapanga ni JINSI ya kutumiana FEDHA ya Mafuta kwa ajili ya choma choma yao.MESSAGE ZIPO na naamini Ex -JaJi Mkuu Chande atakuwa nazo hizo SMS.
Katika Mkoa fulani Nyanda za Juu Kusini wapo Wanyarwanda walikamatwa kwenye maandamano yale.Waziri Mkuu Mh Mwigulu Nchemba anaposema wapo watu kutoka Nje walilipwa kuja kuongeza nguvu kufanikisha MAPINDUZI yale,watu walimbeza sana.
Mwigulu hawezi kuongea VITU bila kuwa na taarifa za ndani kutoka katika Vyombo vya Ulinzi na Usalama vya Serikali.
Swali?Tuwafanye nini watu hawa?☝🏽☝🏽☝🏽