PreGE2025 Askofu Mwamalanga akerwa na kauli ya Amos Makalla kuhusu Chadema, akemea pia siasa za aina hiyo

PreGE2025 Askofu Mwamalanga akerwa na kauli ya Amos Makalla kuhusu Chadema, akemea pia siasa za aina hiyo

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Wont be the same

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2024
Posts
1,564
Reaction score
2,483
Askofu William Mwamalanga ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati maalum ya Maaskofu na Masheikh ya Haki, Amani na Maadili Tanzania ameoneshwa kukerwa na kauli iliyotolewa na Katibu wa NEC Itikadi, Uenezi na Mafunzo CCM Taifa Amos Makalla

Hivi karibuni akiwa mkoani Simiyu ambapo alidai kuwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kina mpango wa kununua virusi vya Ebola na Mpox na kuvisambaza nchini.

Akiwa kwenye mahojiano maalum na Jambo TV, Askofu Mwamalanga amekemea siasa za aina hiyo, sambamba na kutoa wito kwake binafsi na chama chake kutafakari upya kama anastahili kuendelea kutumikia nafasi hiyo.

Soma
 
Kukemewa kwake Makala ndio kumenifanya nikumbuke kuwa Makala ndo mwenezi wa CCM

Huyu jamaa anasahaulika akiwa ofisini? Akitumbuliwa itakuweje?
 
Back
Top Bottom