DeepPond
JF-Expert Member
- Nov 18, 2017
- 40,485
- 99,200
WOTE HAWAAMINI...
Na Askofu Benson Bagonza, KKKT Dayosisi ya Karagwe
Waliopiga kura hawaamini,
Waliogoma kupiga kura hawaamini,
"Walioshinda" hawaamini,
"Walioshindwa" hawaamini,
Walioshuhudia hawaamini,
Waliohesabu kura hawaamini,
Wasimamizi hawaamini,
Waangalizi wa ndani na nje hawaamini,
Walinzi wa amani hawaamini,
Kwa nini lakini?
KWA sababu mwaka 2019 baada ya Uchaguzi wa serikali za mitaa,
"Walioshinda" hawakuwa na furaha,
"Walioshindwa" hawakuwa na furaha,
Waliopiga kura, ambao hawakupiga kura, waliohesabu, waliotangaza na waliosikia, WOTE hawakuwa na furaha. FURAHA alipotea, hajarudi. Sasa na IMANI ametoweka.
Usinibishie kwa sababu ubishi ni hulka ya watu waliopoteza furaha na Imani.
Nani anafuata kuwafuata FURAHA na IMANI?
Na Askofu Benson Bagonza, KKKT Dayosisi ya Karagwe
Waliopiga kura hawaamini,
Waliogoma kupiga kura hawaamini,
"Walioshinda" hawaamini,
"Walioshindwa" hawaamini,
Walioshuhudia hawaamini,
Waliohesabu kura hawaamini,
Wasimamizi hawaamini,
Waangalizi wa ndani na nje hawaamini,
Walinzi wa amani hawaamini,
Kwa nini lakini?
KWA sababu mwaka 2019 baada ya Uchaguzi wa serikali za mitaa,
"Walioshinda" hawakuwa na furaha,
"Walioshindwa" hawakuwa na furaha,
Waliopiga kura, ambao hawakupiga kura, waliohesabu, waliotangaza na waliosikia, WOTE hawakuwa na furaha. FURAHA alipotea, hajarudi. Sasa na IMANI ametoweka.
Usinibishie kwa sababu ubishi ni hulka ya watu waliopoteza furaha na Imani.
Nani anafuata kuwafuata FURAHA na IMANI?