DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Karagwe, Dkt. Benson Bagonza, amesema kuwa taifa linapitia mkwamo wa kisiasa na kiutendaji ambao unahitaji hatua ya dhati ya kujitafakari na kurudi kwenye misingi ya mazungumzo, siyo mapambano.
Akizungumza hivi karibuni kupitia mahojiano maalum na televisheni ya mtandao ya Sauti Digital, Askofu Bagonza amesema mchakato wa ndani wa kisiasa unaoendelea, hususan ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), unaonesha dalili za sintofahamu na upungufu wa misingi imara ya maadili ya kisiasa.
“Kuna mtu amejiunga na chama leo, siku hiyo hiyo anachukua fomu. Unajiuliza, hii ni nini? amesema Askofu Bagonza.
Ameelezea mshangao wake juu ya viongozi waliowahi kuwa sehemu ya tume ya uchaguzi iliyolalamikiwa, kisha kujiingiza katika mchakato wa kugombea, akisema hali hiyo inaleta maswali makubwa kuhusu uadilifu wa mchakato huo.
Akijibu hoja za baadhi ya watu wanaodai kuwa kutoshiriki kwa CHADEMA hakutaleta athari kwa kuwa kuna vyama vingine 18 vinavyoshiriki uchaguzi, Askofu Bagonza ametoa changamoto:
“Ebu wafikirie tuwe na uchaguzi mkuu usiokuwa na CCM, viwe hivyo 18 vingine na CHADEMA halafu aniambie kama huo ni uchaguzi, kwahiyo wanaoona CHADEMA haipo kwahiyo kuna mushkeli, pia wageuze akili zao waangalie kama hakuna CCM kama uchaguzi unaweza kufanyika. Mawazo yangu sina maana kwamba vyama vingine havifai. Ninaamini taifa ambalo linajumuisha kuliko kutawanya, natamani vyama vyote, tena hata vingine ambavyo havijasajiliwa”.
Amesema taifa linahitaji kuwa na "utaratibu jumuishi" ambapo kila Mtanzania anahusishwa kikamilifu bila kubaguliwa – hata wale wasiokuwa na vyama – na kusisitiza kuwa hekima haijachelewa.
“Hekima hata ikichelewa, siku moja inatosha. Kinachotakiwa ni utashi wa kisiasa (political will) wa kutupeleka kwenye taifa la mazungumzo, siyo taifa la mapambano,” alihitimisha Askofu Bagonza.
Kauli yake imekuja wakati wa mchakato unaoendelea wa uchukuaji na urejeshaji wa fomu za kugombea ubunge na udiwani ndani ya CCM, huku kukiwa na sintofahamu juu ya ushiriki wa CHADEMA- chama kikuu cha upinzani nchini katika uchaguzi mkuu wa 2025.
Akizungumza hivi karibuni kupitia mahojiano maalum na televisheni ya mtandao ya Sauti Digital, Askofu Bagonza amesema mchakato wa ndani wa kisiasa unaoendelea, hususan ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), unaonesha dalili za sintofahamu na upungufu wa misingi imara ya maadili ya kisiasa.
“Kuna mtu amejiunga na chama leo, siku hiyo hiyo anachukua fomu. Unajiuliza, hii ni nini? amesema Askofu Bagonza.
Ameelezea mshangao wake juu ya viongozi waliowahi kuwa sehemu ya tume ya uchaguzi iliyolalamikiwa, kisha kujiingiza katika mchakato wa kugombea, akisema hali hiyo inaleta maswali makubwa kuhusu uadilifu wa mchakato huo.
Akijibu hoja za baadhi ya watu wanaodai kuwa kutoshiriki kwa CHADEMA hakutaleta athari kwa kuwa kuna vyama vingine 18 vinavyoshiriki uchaguzi, Askofu Bagonza ametoa changamoto:
“Ebu wafikirie tuwe na uchaguzi mkuu usiokuwa na CCM, viwe hivyo 18 vingine na CHADEMA halafu aniambie kama huo ni uchaguzi, kwahiyo wanaoona CHADEMA haipo kwahiyo kuna mushkeli, pia wageuze akili zao waangalie kama hakuna CCM kama uchaguzi unaweza kufanyika. Mawazo yangu sina maana kwamba vyama vingine havifai. Ninaamini taifa ambalo linajumuisha kuliko kutawanya, natamani vyama vyote, tena hata vingine ambavyo havijasajiliwa”.
Amesema taifa linahitaji kuwa na "utaratibu jumuishi" ambapo kila Mtanzania anahusishwa kikamilifu bila kubaguliwa – hata wale wasiokuwa na vyama – na kusisitiza kuwa hekima haijachelewa.
“Hekima hata ikichelewa, siku moja inatosha. Kinachotakiwa ni utashi wa kisiasa (political will) wa kutupeleka kwenye taifa la mazungumzo, siyo taifa la mapambano,” alihitimisha Askofu Bagonza.
Kauli yake imekuja wakati wa mchakato unaoendelea wa uchukuaji na urejeshaji wa fomu za kugombea ubunge na udiwani ndani ya CCM, huku kukiwa na sintofahamu juu ya ushiriki wa CHADEMA- chama kikuu cha upinzani nchini katika uchaguzi mkuu wa 2025.