Inside10
JF-Expert Member
- May 20, 2011
- 26,079
- 23,961
*Na Baba Askofu Bagonza*✍✍
HEKIMA ZA WANYAMBO
"Jitu litishalo likikumbiza mwendo mrefu bila kukata tamaa, husababisha woga wako uishe"
"Mbu akitua kwenye korodani, hukufanya ujifunze kutumia akili kumwondoa kuliko kutumia nguvu".
"Ugomvi kati ya aliye na silaha na asiye nayo, huamuliwa na wakati"
"Tabia yako wakati wa mgogoro ndiyo huamua utaishije baada ya mgogoro. Usigeuze aibu kuwa hasira".
Kwa matumizi ya nguvu, utawashinda wote lakini hawa huwawezi:
1. Corona virus
2. Ujinga
3. Umaskini
4. Nguvu ya hoja
5. Mahesabu
6. Mioyo ya wafuasi
7. Uzalendo
8. Uzima wa milele
Umezidi mpaka kama:
1. Umeiba na kuficha, kisha ukasahau umeficha wapi
2. Umedanganywa, kisha ukadanganya kuliko aliyekudanganya,
3. Unaposimulia tukio ambalo hukuwapo kuliko aliyekuwepo.
Kweli tumesifiwa kuwa tunajua kukimbia, tukapitiliza hata nyumbani kwetu.
Kumpiga mwanamke yeyote ni kumpiga mama yako.
HEKIMA ZA WANYAMBO
"Jitu litishalo likikumbiza mwendo mrefu bila kukata tamaa, husababisha woga wako uishe"
"Mbu akitua kwenye korodani, hukufanya ujifunze kutumia akili kumwondoa kuliko kutumia nguvu".
"Ugomvi kati ya aliye na silaha na asiye nayo, huamuliwa na wakati"
"Tabia yako wakati wa mgogoro ndiyo huamua utaishije baada ya mgogoro. Usigeuze aibu kuwa hasira".
Kwa matumizi ya nguvu, utawashinda wote lakini hawa huwawezi:
1. Corona virus
2. Ujinga
3. Umaskini
4. Nguvu ya hoja
5. Mahesabu
6. Mioyo ya wafuasi
7. Uzalendo
8. Uzima wa milele
Umezidi mpaka kama:
1. Umeiba na kuficha, kisha ukasahau umeficha wapi
2. Umedanganywa, kisha ukadanganya kuliko aliyekudanganya,
3. Unaposimulia tukio ambalo hukuwapo kuliko aliyekuwepo.
Kweli tumesifiwa kuwa tunajua kukimbia, tukapitiliza hata nyumbani kwetu.
Kumpiga mwanamke yeyote ni kumpiga mama yako.