Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 25,176
- 48,460
Katika kile kinachoonekana ni muendelezo wale tuliowakabidhi jukumu la kulinda ama watu au Rasirimali zetu kuua Raia wasio na Hati, Askari wa wanyama Pori wa Hifadhi ya Taifa ya Ruaha wamemuua kwa kumpiga Risasi mtu mmoja kwa tuhuma za kumiliki nyara za serikali kinyume cha sheria.
Askari hao wakiwa kwenye Land Rover mbili walivamia nyumbani kwa Iddy Kiruma kitongoji cha Mbigima, kijiji cha Isele kwenye Kata ya Mlenge, Jimbo la uchaguzi Isimani Wilaya ya Iringa, Mkoani Iringa, na kumpiga risasi ya mguu kiruma. Kwenye Nyumba hiyo pia alikuwemo Shaabani Chalamila ambaye kwenye purukushani hiyo alifanikiwa kutoroka. Kiruma amekufa akiwa mikononi mwa Askari hao haijulikani walikuwa anampeleka wapi kama ni Hospitali au Kambini kwao.
Askari hao baada ya Shaaban kutoroka walikwenda nyumbani kwake na kumchukua mke wake, Anna Mahogola mwenye watoto mapacha walio na umri wa mwaka mmoja na kuondoka naye na mpaka sasa hawajamrudisha na habari tulizo nazo amepelekwa kituo Kikuu cha Polisi Iringa mijini kilomita 60 toka eneo la Tukio. Hao watoto hawajanyonya maziwa ya mama yao tangu Usiku wa saa tisa kuamkia leo.
Polisi wako eneo la tukio!!
Askari hao wakiwa kwenye Land Rover mbili walivamia nyumbani kwa Iddy Kiruma kitongoji cha Mbigima, kijiji cha Isele kwenye Kata ya Mlenge, Jimbo la uchaguzi Isimani Wilaya ya Iringa, Mkoani Iringa, na kumpiga risasi ya mguu kiruma. Kwenye Nyumba hiyo pia alikuwemo Shaabani Chalamila ambaye kwenye purukushani hiyo alifanikiwa kutoroka. Kiruma amekufa akiwa mikononi mwa Askari hao haijulikani walikuwa anampeleka wapi kama ni Hospitali au Kambini kwao.
Askari hao baada ya Shaaban kutoroka walikwenda nyumbani kwake na kumchukua mke wake, Anna Mahogola mwenye watoto mapacha walio na umri wa mwaka mmoja na kuondoka naye na mpaka sasa hawajamrudisha na habari tulizo nazo amepelekwa kituo Kikuu cha Polisi Iringa mijini kilomita 60 toka eneo la Tukio. Hao watoto hawajanyonya maziwa ya mama yao tangu Usiku wa saa tisa kuamkia leo.
Polisi wako eneo la tukio!!