Askari wa selious game aua mwanafunzi

Askari wa selious game aua mwanafunzi

MndemeF

Member
Joined
Jan 15, 2011
Posts
35
Reaction score
5
Wana jamii hv kweli hii ni sawa kwa askari wa selous game kuua mwanafunzi aliyekuwa anavua samaki ndani ya hifadhi?
 
Ndio sawa kama ni mwanafunzi angekuwa darasani. Hao ndio majangiri wanazuga na uniform mbugani wanatafuta faru wa kikwete
 
Wana jamii hv kweli hii ni sawa kwa askari wa selous game kuua mwanafunzi aliyekuwa anavua samaki ndani ya hifadhi?
Tatizo la hao askari wanafikiri zaidi kinyama kuliko kibinadamu, ni sawa hiyo hifadhi, lakini hakuweza kutumia njia nyingine mbadala kumkamata badala ya kumuua? Wanyama ama samaki nini bwana! Na jamii inayozunguka hifadhi hiyo kubwa kuliko zote Tanzania wanafaidika katika nn? na hata huyo askari najua katekeleza tu sheria na bado analalamika mazingira ya kazi yalivyokuwa magumu. Imefikia wakati kupima kati ya samaki na binadamu yupi analeta maendeleo ya nchi, hao samaki wanahifadhiwa ili iweje na kwa faida ya nani? Inatia uchungu sana.
 
wasi wasi wangu ni pale watanzania watakapochukulia kwamba kufa ni kitu kidogo na cha kawaida halafu roho ya kisasi ikawaingia walah hatabaki mtu na hatakuwepo wa kuwatuliza na hata wakiwatuliza wema wao wa asili utakuwa umeshayeyuka tayari.
 
Ndio sawa kama ni mwanafunzi angekuwa darasani. Hao ndio majangiri wanazuga na uniform mbugani wanatafuta faru wa kikwete

mkuu ungemwona jinsi yule mama mjane anavomlilia mtoto wake aliekua anamtegemea kamwe usingetoa hiyo kauli,. Omba Mungu akusamehe
 
Ndio sawa kama ni mwanafunzi angekuwa darasani. Hao ndio majangiri wanazuga na uniform mbugani wanatafuta faru wa kikwete

Samaki wawili au watatu tu? Ndio watoe roho ya mtoto? Embu kuweni na busara nyie magamba! Mnajua mnapandikiza chuki? Ebo!
 
Back
Top Bottom