Askari wa Mwanza Airport

Askari wa Mwanza Airport

brightoscar

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2013
Posts
369
Reaction score
544
Hawa jamaa inaonyesha huwa wanasubiria mafuta na perfume wachukue yaani ni big deal kwao leo perfume yangu inakaribia kuishi walivyoishambulia kama mpira wa kona..
 
Sasa mkuu utaingiaje kwenye ndege na perfume mkuu..... ni sheria hiyo ya anga mkuu kote duniani cyo bongo tuu soma kabla ya kuingia ndani kunabandiko Hapo airport vitu gani haviruhusiwi......
 
pole bwana mimi niliadithiwa na mtu eti hata maji ya kunywa huendi nayo.. hata lotion nakwambia... nataka mtu wakunipa offer ya kupanda ndege nibebe maji nione kama nitarudishwa
 
Sasa mkuu utaingiaje kwenye denge na perfume mkuu..... ni sheria hiyo ya anga mkuu kote duniani cyo bongo tuu soma kabla ya kuingia ndani kunabandiko Hapo airport vitu gani haviruhusiwi......

kwa hiyo nikifikanianze shoping upya?
 
Ok ,unaweka kwenye bag lile kubwa ambalo huwa huingii nalo ndani,kwenye handbag hairuhusiwi any liquid,pressurized container

kwa hiyo lazima nisafiri na begi kubwa linawekwa wapi?samahani naona umesema haliingii ndani.
 
Halafu bado wananuka vikwapa hao polisi wa ccm, kuiba kote perfume bado wananuka kama pipa la takataka. Mi huwa nawaitaga majambazi sio polisi
 
pole bwana mimi niliadithiwa na mtu eti hata maji ya kunywa huendi nayo.. hata lotion nakwambia... nataka mtu wakunipa offer ya kupanda ndege nibebe maji nione kama nitarudishwa

Mkuu tusiwalaumu wale maafisa usalama. Kwanza wanatekeleza wajibu wao kufuatana na sheria za ICAO.

Mwanzo hata mie sikuelewa ila niliambiwa kuwa lotion, maji au in short vimiminika vinaruhusiwa ndani ya ndege ILA ujazo wake usizidi 100mls.
 
Maada ni jinsi maaskari wa Mwanza wanavyofakamia perfumes ambazo wasafari wananyang'anywa wanapo check in.
 
perfumes inaruhusiwa ila iwe chini ya 100ml la sivyo iweke kwenye begi na iwe check in yaani mzigo unaokaa kwenye buti la ndege sio wa kuingia nao kwenye cabin
 
perfumes inaruhusiwa ila iwe chini ya 100ml la sivyo iweke kwenye begi na iwe check in yaani mzigo unaokaa kwenye buti la ndege sio wa kuingia nao kwenye cabin

Ila hapo Mwanza hao watu ni shida. Walinikomalia siku moja kwenye cologne na lotion za ujazo unaoruhusiwa na International airlines, mama mmoja akazichukua; nikamwambia mama hizo ni za wanaume, labda ukaziuze!.
 
Back
Top Bottom