Askari shupavu akifa, mapambano hayakomi

Askari shupavu akifa, mapambano hayakomi

hard core

Member
Joined
Jan 11, 2015
Posts
46
Reaction score
28
Na. Julius Mtatiro,

Mapambano yaendee, askari amekufa mstari wa mbele wakati vita inakaribia kuisha, ni bahati mbaya, chukueni mwili wake, upeni heshima zote za mwisho kisha uhifadhini na kukumbuka mchango wa askari huyo.

Si muda wa kumbeza na kumsimanga, si muda wa kumuombea mabaya.

Wanaweza kufa askari wengi sana dakika za mwisho za mapigano lakini kusaka ushindi vitani ni jukumu la askari waliobakia, hata wakibaki wachache ni lazima washikamane na vita iendelee, huu siyo wakati wa kujiuliza kama sababu za kuingia vitani zilikuwa sahihi au la, huu siyo muda wa kuacha vita na kuanza mjadala juu ya askari shupavu aliyeuawa mstari wa mbele, huu ni muda wa kupigana vita, vitani hakuna msalie mtume na ukitaka salamu ya upande wa adui umeshakaribisha kifo chako.

Vita haina macho, yeyote yule anaweza kuuawa.

juliusmtatiri@yahoo.com,
 
"Ukitaka Salamu ya Upande wa Adui Umeshakaribisha Kifo Chako", Hii Ina Maana Pana Sana.Do!Wazee Tuliowaamini Wameuawa Wakati

Tunakaribia Ushindi.; Kweli Adui Huyu Ni Noma, Ila Mwisho wa Siku Ushindi Muhimu.
 
Well said mheshimiwa ningesikia cuf imejitoa ukawa ningeumia sana kumbe aliyetoka ni mwenyekiti peke yake kwa wakati huu siasa za upinzani zimepanuka watu wenye uwezo wapo wengi wa kuendeleza mapambano maana ifike mahali iwapo tuna mapenzi ya dhati na nchi yetu tuseme kwamba hata asipokuwepo slaa , mbowe, mnyika , lipumba bado vita itaendelea na ushindi ni lazima mapambano yanapopamba moto ujue ushindi umekaribia . n kupambana tu hadi tone la mwisho marufuku kukata tamaa .
 
Wakuu mtu mmoja akituzingua tunamweka kando tuna songs mbele
Taifa kwanza, chama na mwisho mtu

a UKAWA SONGA MBELE MSIFARAKANE TAFADHALI WATANZANIA TUNAPENDA SN UMOJA WENU HUO NI MPANGO WA MUNGU
 
MURA CHULI, BHITA NI BHITA MURA!

Hii kauli ya Julius Mtatiro ni sawia sana. Kuna haja hata ya kuanzisha kitengo cha kuelemisha watu katika kampaini hii na hasa watu kama yule msukuma wa zeze kwenye website ya CHDEMA kila kona ya nchi wanafikisha ujumbe haraka hasa vijijini na wawe trained kabisa na if possible na slogans zinazo beba ujumbe wa ubaya wa CCM wote tangu iasisiwe na faida za UKAWA

1. Katiba mpya yenye kuzingatia mapenzi ya watanzania, 2. Nguvu ya umma kwemye kuwajibisha viongozi wao, na miiko mingine yote na nini na namna gani hasa rasilimali yetu itamnufaisha kila mmoja nk, nk, nk, nk
 
ASKARI SHUPAVU AKIFA, MAPAMBANO HAYAKOMI:

Na. Julius Mtatiro,

Mapambano yaendee, askari amekufa mstari wa mbele wakati vita inakaribia kuisha, ni bahati mbaya, chukueni mwili wake, upeni heshima zote za mwisho kisha uhifadhini na kukumbuka mchango wa askari huyo.

Si muda wa kumbeza na kumsimanga, si muda wa kumuombea mabaya.

Wanaweza kufa askari wengi sana dakika za mwisho za mapigano lakini kusaka ushindi vitani ni jukumu la askari waliobakia, hata wakibaki wachache ni lazima washikamane na vita iendelee, huu siyo wakati wa kujiuliza kama sababu za kuingia vitani zilikuwa sahihi au la, huu siyo muda wa kuacha vita na kuanza mjadala juu ya askari shupavu aliyeuawa mstari wa mbele, huu ni muda wa kupigana vita, vitani hakuna msalie mtume na ukitaka salamu ya upande wa adui umeshakaribisha kifo chako. Vita haina macho, yeyote yule anaweza kuuawa.

juliusmtatiri@yahoo.com,
0787536759.
 
Maneno murua sana heko mtatiro
 
Aluta Kontiniua!!!!!!!!!!!!!!!!. Mapambano yanaendelea tena kwa nguvu ya pekee na maarifa ya ajabu.

Tuko pamoja Kamanda Mtatiro. Ukombozi ni lazima!!!!!!!!!!!!!!

Viva UKAWA!!!!!!!!!!!!!!
 
ASKARI SHUPAVU AKIFA, MAPAMBANO HAYAKOMI:

Na. Julius Mtatiro,

Mapambano yaendee, askari amekufa mstari wa mbele wakati vita inakaribia kuisha, ni bahati mbaya, chukueni mwili wake, upeni heshima zote za mwisho kisha uhifadhini na kukumbuka mchango wa askari huyo.

Si muda wa kumbeza na kumsimanga, si muda wa kumuombea mabaya.

Wanaweza kufa askari wengi sana dakika za mwisho za mapigano lakini kusaka ushindi vitani ni jukumu la askari waliobakia, hata wakibaki wachache ni lazima washikamane na vita iendelee, huu siyo wakati wa kujiuliza kama sababu za kuingia vitani zilikuwa sahihi au la, huu siyo muda wa kuacha vita na kuanza mjadala juu ya askari shupavu aliyeuawa mstari wa mbele, huu ni muda wa kupigana vita, vitani hakuna msalie mtume na ukitaka salamu ya upande wa adui umeshakaribisha kifo chako. Vita haina macho, yeyote yule anaweza kuuawa.

juliusmtatiri@yahoo.com,
0787536759.

Hongera kaka hii vita ni nzuri na mtashinda. Huku kijijini wananchi wapo tayari
 
Mafisadi wa upinzani wanaitwa askari shupavu .wanawahadaa watanzania nchi nxima na wimbo wa ufisadi .sasa wameingiza ufisadi rasmi cdm ni aibu sana.hakuna vita ya kusema adui ni msafi
 
Napambano yaendelee hadi adui asalimu amri.Naamini kuna wana CUF wengi wenye uwezo wa kuongoza.Hivyo tusitoke kwenye malengo kipindi hiki kuelekea uchaguzi mkuu
 
Asante kamanda Mtatiro........mpk sasa sielewi lengo la hawa waheshimiwa wawili waliojitoa, sijui ndio kutaka sifa au ni nini hasa......nimeumia sana lkn sikomi kusali UKAWA izidi kusimama imara.
 
Wananchi tuna kiu ya mabadiliko..ccm lazima iangamizwe
 
...inyeshe ama liwake kamwe hatutarudi nyuma, tutapambana usiku na chana hadi tumgoe mkoloni mweusi oct 25...tutakaofanya mabadiliko ni sisi tunaoteseka kwa huu
utawala dhalim wa CCM na sio hao viongozi ambao wana maisha mazuri...
 
Back
Top Bottom