View attachment 453494
Historia ya kupaka rangi kwenye midomo kwa kusudi la urembo inaonyesha kuwa jambo hili lilianza zamani sana na inasemekana kuwa lilianzia huko Misri.
Wanawake wa Kimisri wakati huo walikuwa wanapaka
rangi nyekundu kwenye midomo yao ili kuonyesha kuwa WAKO TAYARI KWA AJILI YA NGONO.
Maana halisi ya desturi hii ilikuwa ni kupeleka ujumbe kwa wanaume kuwa uchi wa mwanamke anayepaka rangi
nyekundu mdomoni anapopata hamu ya ngono, midomo ya uchi wake inageuka kuwa na rangi nyekundu kama ile iliyopakwa kwenye midomo ya usoni.
Mwanasayansi na mtafiti wa mabadiliko ya tabia za
wanadamu na maisha ya wanyama ambaye ni mwenyeji wa huko Uingereza, Desmond Morris katika kitabu chake cha
“The Naked Ape (1967)” naye anaunga mkono dhana na madai hayo na anasema kuwa desturi ya wanawake
kupaka rangi nyekundu kwenye midomo imetokana na wanawake kuifananisha midomo ya usoni na midomo ya uke inapovimba na kuwa na rangi nyekundu pale mwanamke anapokuwa na hamu kali ya kufanya ngono.
Kabla ya karne ya 19, kanisa Katoliki lilipinga na kuzuia
matumizi ya lipstick miongoni mwa waumini wake kutokana na kuamini kuwa desturi ya upakaji wa rangi nyekundu katika midomo ya mwanamke ilikuwa na CHIMBUKO LAKE KUTOKA KATIKA IBADA ZA KISHETANI NA UFUSKA AU UMALAYA .
_____________________________________________
Huo ndio ukweli kuhusu "Lipstick"
Wala Sisemi usitumie... Lakini pia sijasema utumie