ARUSHA (NJIRO) HAWANA MAJI YA BOMBA?

ARUSHA (NJIRO) HAWANA MAJI YA BOMBA?

Mparee2

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2012
Posts
3,288
Reaction score
5,762
Nilibahatika kutembelea eneo la Njiro round about kwa Rafiki yangu, nakukuta yupo busy kupakia madumu kwenda kuteka maji.

Binafsi nilishangaa kwani pamoja na Arusha kuwa na vyanzo vingi vya maji na NJIRO kuwa ndani ya kms 10 hivi kutoka mjinikati tena Eneo lililojengeka vizuri, inakuwaje halina maji ya bomba?
Naomba nieleweke Vizuri, MTANDAO WA BOMBA UPO ILA NIMEAMBIWA KUWA UNAWEZA KUCHUKUA MIEZI MIWILI NA KUENDELEA BILA KUTOA MAJI HATA SIKU MOJA.
Nimeambiwa hili tatizo la maji linahusu maeneo yote kuanzia barabara mpya ya East Africa kuelekea mwisho wa Lami na ni la muda mrefu ....nina maanisha miaka kadhaa
Nionavyo mimi, hii ni fursa ya wazi kwa Idara ya maji kutengeneza Pesa; hata sijui tatizo ni nini?
 
Its so sad heavily gated and affluent neighbourhood like Njiro to have problem of clean safe and running water despite the fact Arusha has very many sufficient water sources.

Africans especially Tanzanians under this tyran regime we are a rejected race!
 
Infrastructures kubwa za maji alizifanya Mjerumani, hata kwenye maji mikubwa mabomba aliyoweka Mkerumani sasa yana kutu na pata haya kidhi ongezeko la mahitaji kwani watu wameongezeka sana.

Maji yamekuwa turufu ya siasa, kila anaeomba kura anaahidi kutatua shida ya maji kwa miaka zaidi ya 50 baada ya kuapata uhuru.

Maji ni moja ya mahitaji muhimu ya uhai wa minadamu pamoja na chakula na hewa safi. Moja ya moingozo ya UN ni kuhakikisha kila binadamu anapata maji safi na kuwasaidia wale wasio na uwezo ili wayapate.

Viongozi wetu mmechukua hiatus gani katika hili?
 
Mbezi na kimara nao kupakia madumu kwenye vitoyo na pick ups na kwenda kusaka maji mbali ilikuwa ni desturi yao sijui kwa sasa.
 
Ni kweli Mparee2 Tatizo la Maji njiro limekuwa sugu na AUWSA ni kama wameziba masikio pia wana majibu ya kunatisha tamaa pia wana dharau. Unapokwenda kutoa report kuhusu kukosekana kwa maji kuwa ni mwezi sasa hatujapata Maji wao hukunijibu: "Shukuru Mungu hamjapata Maji ndani ya mwezi mmoja tu kuna wenzenu huko huko njiro wana miezi miwili hawajapata Maji" ni kichefuchefu huko idara ya Maji watumishi wamejisahau hawana kauli njema kwa wateja.
 
Hiyo ni hatari, mtaa maarufu kama njiro kukosa Maji?
sasa kama waliweka mtandao wa mabomba ambao hautoi maji hiyo haijakaa sawa
Nafikiri wangejenga hata Tank la maji mitaa hiyo ili waweze kusambaza maji walau mara mbili kwa wiki
 
Billion 600 zimetengwa kutatua tatizo la maji Arusha.....na utekelezaji wake umeanza....yeyte atakayekwamisha mpango huu tutamfukuza kazi, akizingua sana tunamuwasha risasi
 
Billion 600 zimetengwa kutatua tatizo la maji Arusha.....na utekelezaji wake umeanza....yeyte atakayekwamisha mpango huu tutamfukuza kazi, akizingua sana tunamuwasha risasi
 
Hata bomba mpya naona zimekomea pale relini /Pepsi. Ila nenda mpaka kule radio five maji ni changamoto.
 
Back
Top Bottom