Hapo arusha kipindi hicho 2010 niko form five pale Ilboru, nilikutana na fala mmoja (mtu mzima ana kitambi hivi very smart) anabonga kingereza akaanza kunichangamkia. Salam za hapa na pale mara kaanza kunisogelea huku akinisifia nilivojengeka na nilivo na mvuto. Mara sijakaa sawa anaanza kunitolea macho namna suruali yangu ilivotuna kwa mbele huku akitaka kunipapasa hayo maeneo. Akili ikanijia kuwa huyu mtu atakuwa punga ama tapeli tu. Nilipompa kisogo sikugeuka tena nyuma. Kweli Arusha sio sehemu salama kiviiile. Umakini unahitajika