Arusha: Lema 'aendelea kuongoza' akiwa mahabusu

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (CHADEMA) ambaye yuko mahabusu katika Gereza la Kisongo anaendelea kutenda na kumudu kazi zake akiwa mahabusu. Taarifa za kuaminika zinaonesha kuwa Lema huombwa mawazo, maelekezo na ushauri kabla ya kufanyika jambo lolote Arusha.

Mambo yote yafanyikayo kwa kujadiliwa au kuamriwa na Baraza la Madiwani la Arusha ambalo linadhibitiwa na CHADEMA yanahusisha mawazo na melekezo ya Mbunge Lema. Taarifa zinaonesha kuwa Lema yu katika afya njema na mwenye ari kubwa ya kutenda kazi.

Lema, Mbunge wa kwanza wa upinzani jimbo la Arusha Mjini aliyeweza kutetea kiti chake cha Ubunge, anahusishwa na kuhusika na kila jambo jimboni Arusha katika kulipanga, kulijadili na kuliamua. Lema anatajwa kuwa ni mmoja wa Wabunge machachari wa upinzani nchini.

Yuko mahabusu baada ya kukosa dhamana katika mahakama huko Arusha katika kesi zake mbili za jinai. Bado Lema anapambania kupata dhamana huku akiendelea na kesi zake za jinai.

Mwafaaaaaaa!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 

Unawatesa wazazi wako, hebu jitokeze au mpigie simu kama mzazi hisia za kukukosa mwanae zinamuumiza.
 
Post ya ajabu kabisa hii. Inawezekana vipi Mzee kama wewe uandike habari kama mashairi ya taarabu!
 
Mkuu hizi ni herufi zisizopendwa kusikika wala kusomwa na wanafamilia pendwa, jiandae kupokea kila aina ya tusi kutoka kule.....!

Nimemiss ile signature yako ya "hutaki unaacha"
 
Mibunge ya ccm imekaaa tu kazi kusinzia nakupiga makofi. Bunge hakuna live ndiyo, mwenyekiti chenge ndiyo,
 

Network yao haijapotea. Wana fikra na kutenda tofauti na wewe.
 
Mbunge wa kwanza kwa wabunge wote waliowahi kuwa wabunge pale arusha kupata ubunge kwa vipindi 2 mfululizo!!! Na bado atapata kipindi cha 3.....Mungu ampe uhai!!! Wanaotaka kumpoteza watapotea wao kwanza!! Damu ya Yesu itamfunika milele!! Hapana unafiki pale wala uoga!
 
Mungu atamsaidia sana
 
Hivi Ni Kweli Kuwa Mawakili Wasomi wa Chadema Wameshindwa Kufurukuta Mbele Ya Mawakili Wa Serikali?
 
Mibunge ya ccm imekaaa tu kazi kusinzia nakupiga makofi. Bunge hakuna live ndiyo, mwenyekiti chenge ndiyo,
C unafiki ni ukweli uliowazi kuwa wabunge wa upinzani wanajitahidi kuwasilisha hoja zenye mrengo wa kitaifa hawa wa Lumumba chama kwanza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…