Arusha: Daladala zadaiwa kugoma kisa kupanda kwa bei za mafuta

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,815
4,557
1651743235688.png

Wakazi wa Kwa Mrombo mkoani Arusha wamelazimika kutembea kwa miguu baada ya madereva wa daladala kugoma kutoa huduma ya usafiri kwa kile wanachoeleza kuwa ni kutokana na kupanda kwa bei ya mafuta.

Madereva wa Daladala katika Mkoa wa Arusha wamegoma kuendesha magari yao kwa madai ya kupanda kwa gharama za uendeshaji ikiwemo ongezeko la mafuta huku bei ya nauli ikiwa ni ileile.

“Tumegoma kwa sababu mafuta yamepanda bei sana na nauli zipo chini zimetumika ndani ya miaka 15 nauli ni ileile na Matajiri wanalalamika” Fatma, Kondakta

Kwa upande wake Meneja wa LATRA Mkoa wa Arusha Aman Mwakalebela amesema utaratibu wa kisheria ni lazima siku 14 zipite na nauli zilizotangazwa zibandikwe kwenye magari hivyo kwa sasa Madereva hawaruhusiwi kupandisha nauli.

Chanzo ITV
 
Wakazi wa Kwa Mrombo mkoani Arusha wamelazimika kutembea kwa miguu baada ya madereva wa daladala kugoma kutoa huduma ya usafiri kwa kile wanachoeleza kuwa ni kutokana na kupanda kwa bei ya mafuta.

Taarifa zaidi kukujia hivi punde

Chanzo ITV
Wapo sahihi
 

Wakazi wa Kwa Mrombo mkoani Arusha wamelazimika kutembea kwa miguu baada ya madereva wa daladala kugoma kutoa huduma ya usafiri kwa kile wanachoeleza kuwa ni kutokana na kupanda kwa bei ya mafuta.

Madereva wa Daladala katika Mkoa wa Arusha wamegoma kuendesha magari yao kwa madai ya kupanda kwa gharama za uendeshaji ikiwemo ongezeko la mafuta huku bei ya nauli ikiwa ni ileile.

“Tumegoma kwa sababu mafuta yamepanda bei sana na nauli zipo chini zimetumika ndani ya miaka 15 nauli ni ileile na Matajiri wanalalamika” Fatma, Kondakta

Kwa upande wake Meneja wa LATRA Mkoa wa Arusha Aman Mwakalebela amesema utaratibu wa kisheria ni lazima siku 14 zipite na nauli zilizotangazwa zibandikwe kwenye magari hivyo kwa sasa Madereva hawaruhusiwi kupandisha nauli.

Chanzo ITV
Safi Arusha mnaonesha njia, wengine tufuate kuna mengi ya kuteta mfano katiba mpya, nk .
 
Hakuna mtu wa usafirishaji anaweza kugoma zaidi ya siku moja Tanzania
Ili uamini wataanza kufanya kazi wenyewe bila hata kuambiwa fanyeni

Hii ndio sekta hovyo Tanzania lakini muhimu
Inaendeshwa na watu wajinga wasioenda shule ndio maana Serikali ikitaka hela inakimbilia huko.
 
Hakuna mtu wa usafirishaji anaweza kugoma zaidi ya siku moja Tanzania
Ili uamini wataanza kufanya kazi wenyewe bila hata kuambiwa fanyeni

Hii ndio sekta hovyo Tanzania lakini muhimu
Inaendeshwa na watu wajinga wasioenda shule ndio maana Serikali ikitaka hela inakimbilia huko.
Wacha kutukana wananchi bwashee, mjinga ni wewe mwenyewe!
 
Chugga c wanajifanya wagumu wao hata kupanda daladala wanasema ni udarisalama!
 
Hakuna mtu wa usafirishaji anaweza kugoma zaidi ya siku moja Tanzania
Ili uamini wataanza kufanya kazi wenyewe bila hata kuambiwa fanyeni

Hii ndio sekta hovyo Tanzania lakini muhimu
Inaendeshwa na watu wajinga wasioenda shule ndio maana Serikali ikitaka hela inakimbilia huko.

Nakuunga mkono moja kwa moja, Na asilimia kubwa wa viongozi wao ni makada wa CCM, hua nashndwa kufahamu huchaguliwa kwa njia gani.
 
Back
Top Bottom