Nyankuru Wankuru
JF-Expert Member
- Apr 22, 2018
- 1,199
- 1,346
Wadau habari za asubuhi?, jana nimesafiri kwa gari tajwa hapo juu linalofanya safari zake kutoka mwanza-shinyanga-singida hadi arusha.
Basi hilo kwa kweli limekuwa na tabia ya kutotii sheria za usalama barabarani, yani kuovatake hovyo hovyo bila kufuata sheria kwake ni kawaida. Hadi madereva wa magari mengine huwa wanamunyooshea kidole dereva wa hilo basi kuwa spidi na kuovatake kwake hakufai .
Haya kwa mfano mtu unataka kupanda hilo basi , wahudumu wanakwambia mwisho wa gari hilo ni arusha stand na unaamua kupanda ,mkifika arusha wanakwambia wao hawaingiagi stend badala yake wana stand yao maeneo ya seliani na ndiko wataenda kushusha abiria.
Mfano mtu ulikuwa na safari ya kuunganisha ukifika arusha inakubidi ulipie boda boda uende stand kuu na itakubidi ulipie uzito wa mzigo uliobeba kwa hilo basi na itakubidi ulipie gharama ya kuutoa hapo kwenye stand yao hadi stend kuu.
Abiria tunapazaga sauti zetu askali amfuatilii mnasubiriaga mpake majanga yatokee au mnataka yatokee kama Yale ya tukio la ajali la lucky Vincent ndipo mchukue hatua?.
Muwakanye madereva wa hilo basi waache tabia za kutotii sheria za usalama barabarani na wawashushe abiria wao kwa mujibu wa matamko yao wanapowakaribisha kupanda hayo magari na sio kushusha vichochoroni kwani wanawaongezea gharama zisizo za lazima.
Hizi ndizo taarifa za kiinterijensia RTO arusha tunaomba ulifuatilie gari hilo na muda wowote nitapita maeneo ya ofisi zenu kujua kama mmepata hizi taarifa na kuzifanyia kazi.
Wananchi wanawapa taarifa nyie hamzizingatii badala yake mnasubiria ajali zitokee ndipo mnaanza kuchukua hatua.
Basi hilo kwa kweli limekuwa na tabia ya kutotii sheria za usalama barabarani, yani kuovatake hovyo hovyo bila kufuata sheria kwake ni kawaida. Hadi madereva wa magari mengine huwa wanamunyooshea kidole dereva wa hilo basi kuwa spidi na kuovatake kwake hakufai .
Haya kwa mfano mtu unataka kupanda hilo basi , wahudumu wanakwambia mwisho wa gari hilo ni arusha stand na unaamua kupanda ,mkifika arusha wanakwambia wao hawaingiagi stend badala yake wana stand yao maeneo ya seliani na ndiko wataenda kushusha abiria.
Mfano mtu ulikuwa na safari ya kuunganisha ukifika arusha inakubidi ulipie boda boda uende stand kuu na itakubidi ulipie uzito wa mzigo uliobeba kwa hilo basi na itakubidi ulipie gharama ya kuutoa hapo kwenye stand yao hadi stend kuu.
Abiria tunapazaga sauti zetu askali amfuatilii mnasubiriaga mpake majanga yatokee au mnataka yatokee kama Yale ya tukio la ajali la lucky Vincent ndipo mchukue hatua?.
Muwakanye madereva wa hilo basi waache tabia za kutotii sheria za usalama barabarani na wawashushe abiria wao kwa mujibu wa matamko yao wanapowakaribisha kupanda hayo magari na sio kushusha vichochoroni kwani wanawaongezea gharama zisizo za lazima.
Hizi ndizo taarifa za kiinterijensia RTO arusha tunaomba ulifuatilie gari hilo na muda wowote nitapita maeneo ya ofisi zenu kujua kama mmepata hizi taarifa na kuzifanyia kazi.
Wananchi wanawapa taarifa nyie hamzizingatii badala yake mnasubiria ajali zitokee ndipo mnaanza kuchukua hatua.