Arusha: A libarated zone.

bendaki

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2013
Posts
952
Reaction score
346
Uchaguzi uliokwisha wa madawani ktk kata 27 umeleta jambo mhimu kwa CDM ktk uhai wake kuliko wakati wowote hapo awali. Jiji la Arusha kuanzia jana chama tawala ni CDM na CCM ni wapinzani, hili hawakulitarajia hivi karibuni. Huu ndio utamu wa ngoma ambao huwa ni lele. Ktk uwanja wa mapambono huwa muhimu kupata uwanja ulio kombolewa ili jeshi lako lipate point of application. CDM wana haki kufurahia. Ni ishara tosha kuwa karibuni Tanzania inakombolewa.
 
CDM fellow comrades we give you big up mmetisha wakuu safi sana makamanda namaliza kwa kusema if we need to live as liberals we need to make sure as intellects we r running as fast as possible in the realm of impossibilities to liberate our country
 
Lakini usisahau, "ILIBIDI KUPAMBANA HADI DAMU KUMWAGIKA!" Poleni sana Wana Arusha. Mipigwa lakini mlisonga mbele. Wengine wenu walitiwa gerezani lakini mlisonga mbele. Mlipigwa mabomu na risasi lakini hamkukata tamaa! Mlizika ndugu zenu waliouwawa lakini mkasonga mbele. Kuna kitu kikubwa cha kujifunza na kujivunia kutoka kwenu. Nawashauri neno moja tu, Kupata ni kitu kingine na kutunza ni kitu kingine! Shikeni sana mlicho nacho sasa mtu mwingine asije kuwanyang'anya taji yenu. Kamanda Lema, "I SALUTE YOU!"
 
Ni pigo kubwa kwa maccm ilhal wengine wakijifariji kwa kuanzisha nyuzi za kijuha bila ya kuangalia ukweli.Uchaguzi huu ulikuwa tanuri la moto kwa chadema huku ccm ikiwa ni kuni kavu waliotumia hila chungu nzima kuanzia kuwanyima watu haki yao ya kupiga kura,ubabe,nondo,mapanga na kila aina ya hujuma hadi kutumia policcm lakini chadema yazidi kung'ara kila kona ya nchi kwani imeweza kuikaba ccm kila kona na hatimae kuwapora jiji la kitalii kwa jasho,damu na hata vifo vingi tu.Kilichonifurahisha zaidi ktk uchaguzi huu ni kuona gari ya jeshi ikiwa na askari pamoja na mashabiki wa timu yao ya mpira walivyowapa sapoti makamanda waliokuwa wanalinda kura kwa kuwashangilia kupita maelezo hadi magamba na policcm wakanywea."VIVA CHADEMA VIVA".
 
Kuna watu humu huwa wanataka kutuaminisha kuwa watu wa Dar es Salaam (au tuseme Pwani) ndio walioongoza mapambano ya kuleta Uhuru wa Tanganyika "halafu baadae wakamkaribisha tu Nyerere ila baadae akawageuka na kuleta mfumo Kristo". Swali ni kuwa mbona kama ndio hivyo mbona leo ndio wanaopigia kura wakoloni weusi kwa kupewa sahani za ubwabwa na kofia? Sehemu za Pwani ni moja kati ya sehemu maskini kabisa nchi hii, au kwao huo ndio utajiri?

Wasichojua kuwa hata kabla ya TAA au TANU Wameru walimtuma mtu wao UNO (akiitwa Kaaya kama sikosei) kudai Uhuru wa Wameru. Arusha ni huru tangu zamani, na ndipo ukombozi wa pili ulipoanzia. Wengine watafatia tu (ila mwisho itakuwa ni Dar es Salaam - ambako wababaishaji wamejaa na ndio unaowasikia kila siku wakisema "Arusha mji mgumu kuishi").
 
ulichokiongea Ndugu yangu nakuunga mkono mia kwa mia uchaguzi huu chadema wameonewa sana kila pembe kwa nguvu zote,hujuma za kila aina iliitaji kujitolea kifo ili chedema ishinde kwa bahati mbaya majimbo mengi hayajapata ujasiri wa kulinda kura kwa garama ya kifo ili linawezekana tu,Arusha wakiongozwa na Mbuge wao,lakini itakapofikia hata majimbo kumi tu ya mfano wa Arusha tutashinda, katika uchaguzi wa Kalenga likiboreshwa dafutari la wapiga kura na wakipatikana majasiri wa kulinda kura kama Arusha tutashinda,lakini kwa kuwa tume ni kwa ajili ya ccm hawatokubali hilo
 
Acha niseme ukwl tu ss wanaarusha tumepambana ile mbaya, mm ni moja wapo kati ya vijana waliokuwa wanalinda kura ktk shule ya msingi sombetin, nilikutana na vikwazo vingi sn mpaka nilitishia na policcm watanipiga risasi, but cha kushangaza sana ss wanachadema tukaqa tunafukunzwa ccm wakawa eneo la tukiwa wakilete watu wao na magar na kuwapa pesa hilo tukawa tumeliona tukajikusanya kama makamanda 10 hiv tukaenda kwa policcm na kuwaambia kama hawatazuia hawa ccm kuelekeza watu jins ya kupiga kura patawaka mda si mrefu maana makamanda tulianza kuitana, tulipigwa tulinyanyaswa ila hatukata tamaa, tulilinda kura mpaka kikaeleweka, japokuwa ccm walinunua shahada za wapiga kura wengi sn, ktk watu 24000 wanaenda kupiga kura watu 4000 na ushee?
Ccm walikuwa na uhakika wa kushinda sombetin kwasababu walinunua shahada za wapiga kura, ila kiukwl makanda tulipambana sn na ile policcm kumpiga mbunge wetu ni moja kt ya mipango waliyo panga wao wampig mbunge halafu wanachadema tuanzishe vurugu wao waibe kura, ila ss tulitambua hilo tukawa wapole, sasa matokeo yalipotoka tulishangilia arusha nzima!!!
 
Kama Halmashauri ni yenu sasa acheni kuongelea habari za ushindi hadi leo...pangeni sasa mipango ya kulibadilisha jiii la Arusha ili muonyeshe utofauti.
Mna advantage ya Mbunge na mnaongoza halmashauri , hamtakuwa na utetezi wa uzembe wowote.
Ifikie mahali lele ziishe.
 

Umesema vema mkubwa!
 

Huu ndo ukweli mkuu..hapa ushabiki ukae kando... utetezi wowote....uzembe wowote hauna nafasi. Uchaguzi umekwisha diwani fanya kazi...Sombetini ina mambo mengi. Idara ya hali ya hewa imetoa taarifa kuhusu mvua nyingi ...kuna maeneo kwenye kata wananchi watakufa kama mifereji ya maji haitatengenezwa..anza kazi Bananga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…