Ardhi ya Tanzania yazidi kuumiza wanachama EAC

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,315
33,111
Keneth Goliama
MVUTANO kuhusu suala la ardhi umeibuka jana katika mkutano wa wataalamu wa kamati za Serikali Kanda ya Afrika Mashariki uliojadili madini, baadhi ya nchi zimepinga kuingiza ardhi kwenye mambo yanayoshughulikiwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Wakichangia katika mkutano huo kwa nyakati tofauti, wajumbe walisema itakuwa ngumu kwa baadhi ya nchi kuingia kuingiza suala hilo kwenye mambo ya EAC, kwa sababu bado ndani ya nchi hizo kuna migogoro ya ardhi.
Wakati baadhi ya wajumbe wakipinga hilo, wengine kutoka Uganda walisema haiwezekani nchi wanachama kuogopa kuingiza suala hilo kutokana na kuonyesha maendeleo mazuri.

Hata hivyo, wajumbe kutoka nchi ya Kenya walionyesha wasiwasi wa uharaka wa kuingia kuingiza ardhi kwenye masuala ya EAC kutokana na mapigano yanayotokea ndani ya baadhi ya nchi wanachama.

“Itakuwa ajabu kuingiza shirikisho la ardhi katika jumuiya wakati nchi za Rwanda Burundi na Tanzania zikionyesha kuwa na ugomvi wa ardhi na wawekezaji,” alisema Mkuu wa Sera ya Mipango na Ardhi kutoka Ethiopia, Dk John Kangwanja.

Dk Kangwanja alisema kama hatua hiyo itafikia, kuna nchi zinaweza kuathirika kwa kiasi kikubwa kutokana na migogoro ambayo inaendelea kujitokeza baina ya wazawa na wawekezaji.

Wakati suala hilo lilipokuwa likizidi kuzua mvutano kwenye ukumbi, wawakilishi wa Tanzania wakiongozwa na Naibu Waziri wa Fedha, Gregory Teu, walionekana kutochangia chochote huku waziri akiulizwa suala hilo kutoa maelezo alijibu kuwa hana maelezo.

Wachiangiaji hao walisema Sheria ya mwaka 1995 na Sera ya Ardhi ya Tanzania, inapishana kwa kiasi kikubwa kutokana na kupitwa na wakati.Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Ardhi (ARU), Profesa Lucugga Kironde, alisema Tanzania ikikubali kuingiza suala hilo, itarajie kukumbwa na migogoro mikubwa kutokana na nchi nyingi za jumuiya hiyo zinanyemelea baada ya kwao kukumbwa na uhaba.

Profesa Kironde alisema haiwezekani Tanzania ikiingia kwenye shirikisho bila kufanya marekebisho ya sheria ya ardhi, Watanzania wataendelea kuonekana maskini huku wachache kutoka EAC wakinufaika.

“Afrika ina rasilimali za kutosha kila mahali hasa madini,umefika wakati kufuatilia kwa makini sheria ya ardhi ili mikataba ya nchi iweze kunufaisha wazawa kutokana na kumiliki ardhi,” alisema Profesa Kironde

Chanzo. Ardhi ya Tanzania yazidi kuumiza wanachama EAC
 
Back
Top Bottom