ManiTek TV
JF-Expert Member
- Jun 3, 2011
- 410
- 159
[h=1]APPLE WAZIMA KELELE ZA WAPINZANI NA IOS 8.0.2[/h]
Apple wametimiza ahadi ya kutokulala mpaka kieleweke kuhusu iOS. Siku ya leo wametoa iOS 8.0.2 ambayo itasuluhisha matatizo kadhaa baada ya jaribio la kurekebisha tatizo hilo kufeli vibaya mno walipotoa iOS 8.0.1 kwa kuongeza bugs, bugs ambao hupelekea simu kupoteza mtandao na pia kisoma alama za vidole kwenye kifungo cha mwanzo (home button) kutofanya kazi kabisa.
iOS 8.0.2 inaonekana kuwa tweak ndogo tu kwani faili hilo lina ukubwa wa 64.1 mb kwenye iPad Mini, 64.7 mb kwenye iPhone 5 na 72.2 mb kwenye iPhone 6 Plus. Hivyo huchukua muda mfupi kupakua na ku-install bali pia. Apple wametangaza kuwa simu na tablet ambazo zimewekewa iOS 8.0.1 zitatengenea mara tu zitakapowekea toleo hili la 8.0.2
Mafanikio ya kuboresha iOS yataleta faraja kubwa kwa Apple hasa baada ya wadau mbali mbali kuanza kupinga suala la kupinda kwa iPhone 6 Plus baada ya kukaliwa, wadau wa BBC Technology pamoja na kuikalia mara kadhaa pia wamefanya zoezi la kuiweka mfuko wa nyuma iPhone 6 Plus siku nzima. Simu hiyo imetumika katika shughuli za kawaida za kikazi na kimaisha na kutoa taarifa kwamba iPhone 6 Plus haikupinda wala kuathirika chochote.
Pia wadau wa Mac Romours nao wamefanya zoezi kama hilo bila ya iPhone kupinda. Pia Mac Romours pamoja na kukiri kwamba utakapoikalia kwa nguvu upo uwezekano wa kupinda kwa simu pia wameainisha kuwa fableti mbali mbali zinazopinda baada ya kukaliwa.
Kampuni mbali mbali za upinzani ikiwemo Nokia, LG na Samsung wamekuwa wakimimina mfululizo wa twitter na kuishikia bango kashfa ya kupinda kwa iPhone 6 Plus huku LG wakiongoza kutumia hashtag ya bendgate (#Bendgate).
Usiku wa leo tutaifanyia majaribio kadhaa app ya Health iliyokusudiwa kurekebisha na kuripoti hali yake, pamoja na kujaribu kuchunguza iwapo toleo hilo lina matatizo yoyote mengine mapya. Usiache kutembelea Gajetek kwa makala hiyo itayafuata hivi karibu itakayozungumzia suala hilo.
Chanzo: gajetek habari
-
Mwandishi Wetu
Apple wametimiza ahadi ya kutokulala mpaka kieleweke kuhusu iOS. Siku ya leo wametoa iOS 8.0.2 ambayo itasuluhisha matatizo kadhaa baada ya jaribio la kurekebisha tatizo hilo kufeli vibaya mno walipotoa iOS 8.0.1 kwa kuongeza bugs, bugs ambao hupelekea simu kupoteza mtandao na pia kisoma alama za vidole kwenye kifungo cha mwanzo (home button) kutofanya kazi kabisa.
iOS 8.0.2 inaonekana kuwa tweak ndogo tu kwani faili hilo lina ukubwa wa 64.1 mb kwenye iPad Mini, 64.7 mb kwenye iPhone 5 na 72.2 mb kwenye iPhone 6 Plus. Hivyo huchukua muda mfupi kupakua na ku-install bali pia. Apple wametangaza kuwa simu na tablet ambazo zimewekewa iOS 8.0.1 zitatengenea mara tu zitakapowekea toleo hili la 8.0.2
Mafanikio ya kuboresha iOS yataleta faraja kubwa kwa Apple hasa baada ya wadau mbali mbali kuanza kupinga suala la kupinda kwa iPhone 6 Plus baada ya kukaliwa, wadau wa BBC Technology pamoja na kuikalia mara kadhaa pia wamefanya zoezi la kuiweka mfuko wa nyuma iPhone 6 Plus siku nzima. Simu hiyo imetumika katika shughuli za kawaida za kikazi na kimaisha na kutoa taarifa kwamba iPhone 6 Plus haikupinda wala kuathirika chochote.
Pia wadau wa Mac Romours nao wamefanya zoezi kama hilo bila ya iPhone kupinda. Pia Mac Romours pamoja na kukiri kwamba utakapoikalia kwa nguvu upo uwezekano wa kupinda kwa simu pia wameainisha kuwa fableti mbali mbali zinazopinda baada ya kukaliwa.
Kampuni mbali mbali za upinzani ikiwemo Nokia, LG na Samsung wamekuwa wakimimina mfululizo wa twitter na kuishikia bango kashfa ya kupinda kwa iPhone 6 Plus huku LG wakiongoza kutumia hashtag ya bendgate (#Bendgate).
Usiku wa leo tutaifanyia majaribio kadhaa app ya Health iliyokusudiwa kurekebisha na kuripoti hali yake, pamoja na kujaribu kuchunguza iwapo toleo hilo lina matatizo yoyote mengine mapya. Usiache kutembelea Gajetek kwa makala hiyo itayafuata hivi karibu itakayozungumzia suala hilo.
Chanzo: gajetek habari