Apple imetoa mfumo mpya wa iOS 16.0.2 kwa watumiaji wa iPhone 8 mpaka iPhone 14 zote; ili kurekebisha matatizo ya Kamera za iPhone 14 Pro na iPhone 14 Pro Max.
Siku chache zilizopita baadhi ya watumiaji walikuwa wanalalamika kamera ya iPhone 14 Pro ilikuwa inatikisika na kutoa kelele kwa ndani. Matatizo hayo yalikuwa yanatokea pale mtu akitaka kurekodi picha au video kwa kutumia app za Snapchat, Instagram na TikTok.
Apple imefix matatizo hayo na imesisitiza watumiaji wote wa iPhone 14 kuweka update hii ili kusaidia Stabilizer ya kamera ya iPhone isiharibike.
๐ ๐ฎ๐๐ฎ๐๐ถ๐๐ผ ๐บ๐ฒ๐ป๐ด๐ถ๐ป๐ฒ ๐ฎ๐บ๐ฏ๐ฎ๐๐ผ ๐๐ฎ๐บ๐ฒ๐ฟ๐ฒ๐ธ๐ฒ๐ฏ๐ถ๐๐ต๐๐ฎ ๐ธ๐๐ฎ ๐๐ถ๐บ๐ ๐ป๐๐ถ๐ป๐ด๐ถ๐ป๐ฒ ๐ฎ๐บ๐ฏ๐ฎ๐๐ผ ๐๐ถ๐ผ ๐ถ๐ฃ๐ต๐ผ๐ป๐ฒ ๐ญ๐ฐ:
1๏ธโฃ Simu kuonyesha rangi nyeusi kwa muda mrefu; baada ya kufungua simu kwa mara ya kwanza
2๏ธโฃ Ujumbe wa Copy and Paste ulikuwa unajitoa kabla mtu hajafanya maamuzi
3๏ธโฃ Kuna baadhi ya iPhone 14 zilikuwa hazitoi mlio baada ya kuwasha simu