Kama nina uwezo wa kutoa 1.4 kwa mwezi yanini si bora niendelee kukaa mabonde kuinama hiyo pesa nitumie kumalizia nyumba yangu
Hiyo ni nyumba inapatikana Kwa owner mimi nimeongea naye, bei Za nyumba Dar ziko juu, kwanza ungeanza Na swali je kumiki apartment kama hiyo maeneo hayo inaghalamu kiasi gani? Kwa hela ninayopangishia it will take 25yrs kurudisha investment Kwenye hiyo property sasa hapo hakuna FAIRNESS kivipi? Watu mnawasakama wenye nyumba mnasahau bei Za viwanja Na ujenzi zilivyo juu. Hakuna faida inayopatikana Kwenye apartment for the next 25yrs Kwa bei ya 1.4mil Kwa Mwezi ndio maana hapo hapo Kwenye hizo apartment kuna wengine wanapangisha Kwa $1000,
Ningeshauri tuwe wakweli Na tufanye research ya mambo kabla ya kupost tu vitu visivyo eleweka, it is shame wabongo tunapenda kuongea kiwivu wivu hivi, kisha tunalia mendeleo hakuna wakati ukiona mtu ana Mradi halali kinachofanyika ni kufanya majungu, huna facts zozote,
Jamani waliomua kujikwamua kiuchumi Kwa njia halali mwahache, inakasirisha kuona biashara halali zinapigwa vita, mnataka kila mtu awe fisadi
Binafsi nilifanya sana juhudi kununua hizo apartment ila nilishindwa Kwenye mchakato, ndio maana nimezifuatilia sana niweze kupanga kutokana Na ukaribu wake Kwenda kazini kwangu, ebu piga mahesabu una mkutano Na mtu saa 1800 mjini Na unakaa airport inakuchukua muda ili ufike mjini Kwa Siku Za Kazi ?
Hizi sio nyumba Za watu Wa chini tuwe tunaangalia mambo Kwa upana wake , ila hiyo 1.4 Kwa Mwezi naona fair japo sina kiasi Na ndio maana nimemtafuta mpaka owner, siwe weka chuki Kwenye biashara ya mtu wakati najua Naye ametumia pesa