Nimekuwa nikipitia website mbali mbali zinazotoa matangazo hapa TZ, kuna ubabaishaji mkubwa sana. Kuna tangazo la apartment hizi hizi za Ilala mchikichini, sijui ni wewe mwenye hilo tangazo au ni mtu mwingine, kama ni wewe basi jirekebishe, otherwise utakuwa unachanganya wateja wako.
1. December 15, 2014. Tangazo liliingia kupatana.com likionyesha apartment inakodishwa kwa $450/=
Mchikichini Resident | Dar es Salaam | Kupatana
2. January 5, 2015. Tangazo liliingizwa tena kupatana.com, mara hii kodi kwa mwezi ni Sh. 800,000/=
APARTMENT FOR RENT | Dar es Salaam | Kupatana
3. January 12, 2015. Tangazo likaingizwa kwa mara ya tatu kupatana.com, kodi ikisomeka Tsh 100,000,000/=
NHC Mchikichini apartment | Dar es Salaam | Kupatana
4. January 13, 2015. Tangazo liliingizwa kwa mara ya nne kupatana.com, kodi ikiwa Tsh 1,000,000/=
APARTMENT FOR RENT | Dar es Salaam | Kupatana
5. February 25, 2015. Tangazo liliingizwa kwa mara ya tano kupatana.com, kodi ikiwa $ 1,000/=
3bdrm for Rent at Ilala, Mchikichini, Dar es salaam | Dar es ...
Kutokana na namba moja ya simu kutumika mara zote tangazo linapotolewa, inaonyesha tangazo ni la mtu mmoja, leo hii lipo jamiiforums bei ikiwa tsh 1.4million.
Je leo hii nikikupigia simu nikahitaji hiyo apartment kwa Tsh. 800,000/= kwa mwezi kama ulivyoeleza hapo nyuma utakubali?
Jipange mkuu, unapoteza wateja.