Anzeni vikao vya Send-off wanajamvi

Anzeni vikao vya Send-off wanajamvi

martinezstavo

JF-Expert Member
Joined
Jun 30, 2020
Posts
735
Reaction score
1,560
Kama kunasiku nina furaha basi ni leo. Wiki kadhaa nyuma nilileta Uzi kuhusu mwanamke niliyempa ujauzito kwa kudhani kuwa namkomoa baadae aliniganda mpaka nkawa nakosa Raha kwa kuwa sikumpenda na nilidate naye ili kulipa kisasI lakini leo nimepata kuamini kuwa unaweza fanya jambo baya likaleta matokeo ambayo hujayatarajia kabisa (Baya lisilokuzulu ni Jema lisilo na faida)

Nilipoleta uzi hapa watu walinijia juu wakanipasha, wakanishauri, nikashaulika. Kwanza kabisa niliamua kujifunza kusamehe maana hapo mwanzo nilikuwa naamimi ukinikosea kwa jambo lolote lazima nilipe kisasi, kisasi ilikuwa ndo njia pekee ya kutoa sumu ndani yangu.

Pili nikaanza kumrudishia heshima kama mwanamke aliyenibebea kiumbe changu. Tatu nikaazimia kumtambulisha kwetu jambo ambalo lilifanikiwa kwa 70%

Tukio lililotokea leo ndo limenisukuma kuandika huu uzi niwashukuru lakini pia niwaalike kwenye ndoa tukufu ambayo soon itapagwa tarehe ambayo itakuwa kabla ya delivery. Nisiseme mengi ila leo nimetoka ukweni nimepokelewa kama Lissu alipowasili Julius Nyerere Airport.

Ova

Pia soma: Ananiganda sana mpaka sina raha
 
Inapendeza kiongozi, Mimi bado kwanza naufanyisha moyo wangu mazoezi ukomaekomae kwanza sometimes maamuzi yake yakibwege sana
 
Hii ndio jamii forum,mtu unaweza kuchota maarifa kibao toka hapa,hapa hutakosa Neno lililotimia. Na Wewe ndio mwanaume halisi,unaeweza kujifunza,kujirekebisha na kusonga mbele kishujaa kabisa ukijiamini. Hongera kwako kijana
 
Back
Top Bottom