Artificial intelligence
JF-Expert Member
- Jan 28, 2021
- 1,262
- 2,191
SEHEMU YA KWANZA.
Ukweli uliofichwa, unaopatikana kwenye vipande vya mawe vyenye jumbe kutoka sumerians, Babylonians, Akkadians.
Ukizungumzia kuhusu watu wa kale, maisha ya kale na viumbe waliofika duniani kutoka sayari nyingine huwezi kuwasahau annunaki. Historia kutoka katika summerian culture inaeleza kwamba, Annunaki waliabudiwa na walihusika katika kuhukumu mema na mabaya, gods and goddesses waliokuja duniani kumtengeneza mtu (modern man) kutoka kwenye ulimwengu mwingine, ambao unasemekana ni sayari ya Nibiru (sumerian God & Goddesses -the Annunaki, 2016).
Annunaki walitawala maisha na mifumo ya imani ya watu wa kale waliojulikana kama Mesopotamia, lakini ambao kwa sasa wanajulikana kama Tigris-Euphrates river system. Je walikuwa Mungu? hili suala ambalo linazua mkanganyiko kwenye hii saga.
Zecharia Sitchin, muhandishi na mtafiti na mtafsiri maandishi ya kale na msomi kutoka chuo kikuu cha London, anasema hawakuwa Mungu, japo walichukuliwa na kuabudiwa kama Mungu. Baada ya kufanya tafiti nyingi za maandiko ya kale aliitimisha kwa kusema kwamba, hawakuwahi kuwa Mungu, bali viumbe wa ajabu wenye nguvu waliokuja duniani kutoka sayari ya mbali Nibiru inayopatikana kwwnye mfumo wa sayari, ambayo uikaribia dunia kila baada ya miaka 3,500 ikiwa kwenye muhimili wake.
Creation of Human Race
Kutokana na ushahidi uliopatikana kutoka kwenye maandiko ya kale, inasemekana zaidi ya mamia ya maelfu ya miaka iliyopita walikuja viumbe waliofanana na Annunaki kwenye sayari ya dunia- Enki na Enlil, ambao walikuwa watoto wa Annunaki, katika kipindi hicho Anu alikuwa bado anaishi hadi millennia karibu na kuzaliwa kwa Jesus Christ.
Viumbe hao walikuwa na ujuzu mkubwa katika genetic manipulation, hivyo kwa kutumia ujuzi huu walifanya majaribio mengi (proto-human) ya kumtengeneza binadamu wa sasa(modern man) kwa kutimia teknolojia ya human cloning. Kivipi?, ntaelezea mbeleni.
Hebu turudi kwanza kwenye biblia na historia ya kuumbwa kwa mwanadamu. Historia ya Biblia ya uumbaji inatueleza kwamba, mwanaume na mwanamke hawakuumbwa kwa wakati mmoja, bali mwanamke alitolewa kwenye ubavu wa mwanaume (Adam), Adam akiwa mtu wa kwanza kuumbwa hapa duniani kutokana na maandiko ya Biblia, Kwahiyo Adam ndiyo mwanadamu wa kwanza kutokana na maandiko matakatifu ya Biblia takatifu. Je mwanamke alitolewaje kwenye ubavu wa mwanaume? (hapa imani ndiyo inatuongoza tuliache kwanza lilivyo).
THE CREATION OF MAN
Ushahidi wa kwanza kabisa, uliotafsiriwa na sumerians unaonyesha ya kwamba mtu (binadamu wa sasa) alitengenezwa/kuumbwa na Nefilim. Ushahidi huu umezua mkanganyiko kuhusu theory of evolution na Judeo-Christian tenets ambayo imeegemea kwenye Biblia, lakini ukweli ni kwamba ujumbe uliopatikana kutoka Sumerian texts, ndiyo unaoweza kudhibitisha hizo nadharia mbili.
Ukisoma kutoka epic of creation ya sumerians, imeelezwa kwamba uwepo wa mtu, ulitokana na uwepo wa Nefilim zama hizo, ambapo matukio mbali mbali yalirekodiwa, ,mfano tukio la Enlil na Ninlil, tukio lililotukia kabla hata ya uumbaji wa mtu, wakati ambao kwenye Nippur waliishi gods tu, vile vile maandishi haya yanaelezea kuumbwa kwa dunia na maendeleo ya mimea na maisha ya wanyama, hii inaweza kudhibitisha theories za mabadiliko (evolution) za sasa.
Sumerians texts zinaeleza kwamba, wakati ambapo Nefilim alikuja duniani kwa mara ya kwanza, sanaa ya kupanda mbegu za mazao, matunda na ufugaji wa wanyama ulikuwa bado haujaanza duniani. Vile vile Biblia inasema hivyo, kuhusu kuumba mtu kwa siku 6. Kitabu cha Genesis kimegusia hatua za kwanza za mabadiliko (earlier evolution stage):
No plant of the cleared field was yet on the earth,
No herb that is planted had yet been grown,
And Man was not yet there to work the soil.
Lakini vile vile Sumerians texts zote zinaeleza kwamba Miungu ilimtengeneza mtu ili afanye kazi yao. Creation of epic imelithibitisha hilo (Nukuu zote nitaziambatanisha zilivyo kwenye vitabu bila kuzitafsiri ili nisipindishe maana kwa msomaji):
I will produce a lowly primitive,
Man shall be his name.
I will create a primitive worker ,
He will be charged with the service of the gods,
that they might have their ease.
Neno mtu(man) limetokana na lugha ya Sumerians na Akkadians, ambalo lilitokana na maneno lulu (primitive ), lulu amelu (primitive worker), an awilum (laborer).
Turudi kwenye biblia, baada ya Mungu kumuumba mwanadamu, akampa bustani ya Eden aitunze na kuitawala dunia na vyote vilivyomo, lakini Adam na Eve wakamkosea Mungu kwa kula tunda la mti wa ufahamu. Mungu akasema tazama, mtu amekuwa mmoja wetu, kufahamu mema na maovu. Je huyo Mungu alikuwa anamwambia nani?, na Mungu anayezungumziwa hapa katika Sumerians ni Elohim (Annunaki).
Agano la kale limeweka wazi ya kwamba mtu hakuwa Mungu wala hakutoka mbinguni. Mtu wa kwanza aliitwa Adam kwa sababu aliumbwa kwa "adama" ambayo ina maana ya udongo wa dunia (mtu akifa tunasema ametoka mavumbini, amerudi mavumbini).
Adam aliumbwa katika picha na ufanano wa Muumba (Mungu), kuumbwa kwa ufanano huo, hakuachi wasiwasi wowote ya kwamba Mtu alifanana na Mungu kimwili, kimuonekano wa nje na ndani. Je mtu angewezaje kufanana na muumba wake? Mtu alitengenezwaje? (Majibu utayapata mbeleni).
Mnamo mwaka 1859 Charles Darwin alichapisha utafiti wake kuhusu evolution "On the Origin of Species by Means of Natural Selection, or the Preservation of Favoured Races in the Struggle for Life". Darwin kutokana na utafiti wake huo, alihitimisha kwa kusema kwamba, viumbe hai wote akiwemo mwanadamu ni matokeo ya mabadiliko(evolution by natural selection). Mwanzoni kanisa lilikuja juu kwa kumpinga lakini badae kadri wanasayansi na watafiti walivyozidi kutoa machapisho yao, kanisa likakubaliana.
Lakini je tumetokana na apes, kama ni hivyo mbona wa sasa hawabadiliki. Evolution kwa ujumla inaweza kuelezea matukio yaliyosababisha mabadiliko ya maisha na aina mbali mbali za maisha zilizokuwepo duniani, kuanzia kwenye kuumbwa kwa mtu, lakini evolution haiwezi kuelezea kuhusu uwepo wa binadamu wa sasa (modern man/Homo sapiens) na haina udhibitisho wowote wa kuonyesha jinsi mabadiliko ya ghafla kutoka Homo erectus kwenda Homo sapiens yalivyotokea.
Hominid ya genus Homo ni matokea ya evolution, lakini Homo sapiens ni matokea ya tukio la mabadiliko na mapinduzi ya haraka sana. Homo sapiens(binadamu wa sasa), ilitokea miaka 300,000 iliyopita, muda ambao ni wa karibu sana.
Watafiti na wanasayansi hawana maelezo ya nini kilitokea, kupelekea mabadiliko ya ghafla hivyo na kutokea kwa binadamu wa sasa, lakini jumbe kutoka sumerians na Babylonian zimeelezea. Agano la kale pia limeelezea.
Homo sapiens-modern man-aliletwa na miungu wa kale (ancient gods).
Aliletwa kivipi? na wapi?. Endelea kufuatilia hapa hapa.
N.B. Andiko hili linaweza lisiishe karibuni kwa sababu nataka niweke kila aina ya ushahidi ili kudhibitisha ukweli huu.
Ukweli uliofichwa, unaopatikana kwenye vipande vya mawe vyenye jumbe kutoka sumerians, Babylonians, Akkadians.
Ukizungumzia kuhusu watu wa kale, maisha ya kale na viumbe waliofika duniani kutoka sayari nyingine huwezi kuwasahau annunaki. Historia kutoka katika summerian culture inaeleza kwamba, Annunaki waliabudiwa na walihusika katika kuhukumu mema na mabaya, gods and goddesses waliokuja duniani kumtengeneza mtu (modern man) kutoka kwenye ulimwengu mwingine, ambao unasemekana ni sayari ya Nibiru (sumerian God & Goddesses -the Annunaki, 2016).
Annunaki walitawala maisha na mifumo ya imani ya watu wa kale waliojulikana kama Mesopotamia, lakini ambao kwa sasa wanajulikana kama Tigris-Euphrates river system. Je walikuwa Mungu? hili suala ambalo linazua mkanganyiko kwenye hii saga.
Zecharia Sitchin, muhandishi na mtafiti na mtafsiri maandishi ya kale na msomi kutoka chuo kikuu cha London, anasema hawakuwa Mungu, japo walichukuliwa na kuabudiwa kama Mungu. Baada ya kufanya tafiti nyingi za maandiko ya kale aliitimisha kwa kusema kwamba, hawakuwahi kuwa Mungu, bali viumbe wa ajabu wenye nguvu waliokuja duniani kutoka sayari ya mbali Nibiru inayopatikana kwwnye mfumo wa sayari, ambayo uikaribia dunia kila baada ya miaka 3,500 ikiwa kwenye muhimili wake.
Creation of Human Race
Kutokana na ushahidi uliopatikana kutoka kwenye maandiko ya kale, inasemekana zaidi ya mamia ya maelfu ya miaka iliyopita walikuja viumbe waliofanana na Annunaki kwenye sayari ya dunia- Enki na Enlil, ambao walikuwa watoto wa Annunaki, katika kipindi hicho Anu alikuwa bado anaishi hadi millennia karibu na kuzaliwa kwa Jesus Christ.
Viumbe hao walikuwa na ujuzu mkubwa katika genetic manipulation, hivyo kwa kutumia ujuzi huu walifanya majaribio mengi (proto-human) ya kumtengeneza binadamu wa sasa(modern man) kwa kutimia teknolojia ya human cloning. Kivipi?, ntaelezea mbeleni.
Hebu turudi kwanza kwenye biblia na historia ya kuumbwa kwa mwanadamu. Historia ya Biblia ya uumbaji inatueleza kwamba, mwanaume na mwanamke hawakuumbwa kwa wakati mmoja, bali mwanamke alitolewa kwenye ubavu wa mwanaume (Adam), Adam akiwa mtu wa kwanza kuumbwa hapa duniani kutokana na maandiko ya Biblia, Kwahiyo Adam ndiyo mwanadamu wa kwanza kutokana na maandiko matakatifu ya Biblia takatifu. Je mwanamke alitolewaje kwenye ubavu wa mwanaume? (hapa imani ndiyo inatuongoza tuliache kwanza lilivyo).
THE CREATION OF MAN
Ushahidi wa kwanza kabisa, uliotafsiriwa na sumerians unaonyesha ya kwamba mtu (binadamu wa sasa) alitengenezwa/kuumbwa na Nefilim. Ushahidi huu umezua mkanganyiko kuhusu theory of evolution na Judeo-Christian tenets ambayo imeegemea kwenye Biblia, lakini ukweli ni kwamba ujumbe uliopatikana kutoka Sumerian texts, ndiyo unaoweza kudhibitisha hizo nadharia mbili.
Ukisoma kutoka epic of creation ya sumerians, imeelezwa kwamba uwepo wa mtu, ulitokana na uwepo wa Nefilim zama hizo, ambapo matukio mbali mbali yalirekodiwa, ,mfano tukio la Enlil na Ninlil, tukio lililotukia kabla hata ya uumbaji wa mtu, wakati ambao kwenye Nippur waliishi gods tu, vile vile maandishi haya yanaelezea kuumbwa kwa dunia na maendeleo ya mimea na maisha ya wanyama, hii inaweza kudhibitisha theories za mabadiliko (evolution) za sasa.
Sumerians texts zinaeleza kwamba, wakati ambapo Nefilim alikuja duniani kwa mara ya kwanza, sanaa ya kupanda mbegu za mazao, matunda na ufugaji wa wanyama ulikuwa bado haujaanza duniani. Vile vile Biblia inasema hivyo, kuhusu kuumba mtu kwa siku 6. Kitabu cha Genesis kimegusia hatua za kwanza za mabadiliko (earlier evolution stage):
No plant of the cleared field was yet on the earth,
No herb that is planted had yet been grown,
And Man was not yet there to work the soil.
Lakini vile vile Sumerians texts zote zinaeleza kwamba Miungu ilimtengeneza mtu ili afanye kazi yao. Creation of epic imelithibitisha hilo (Nukuu zote nitaziambatanisha zilivyo kwenye vitabu bila kuzitafsiri ili nisipindishe maana kwa msomaji):
I will produce a lowly primitive,
Man shall be his name.
I will create a primitive worker ,
He will be charged with the service of the gods,
that they might have their ease.
Neno mtu(man) limetokana na lugha ya Sumerians na Akkadians, ambalo lilitokana na maneno lulu (primitive ), lulu amelu (primitive worker), an awilum (laborer).
Turudi kwenye biblia, baada ya Mungu kumuumba mwanadamu, akampa bustani ya Eden aitunze na kuitawala dunia na vyote vilivyomo, lakini Adam na Eve wakamkosea Mungu kwa kula tunda la mti wa ufahamu. Mungu akasema tazama, mtu amekuwa mmoja wetu, kufahamu mema na maovu. Je huyo Mungu alikuwa anamwambia nani?, na Mungu anayezungumziwa hapa katika Sumerians ni Elohim (Annunaki).
Agano la kale limeweka wazi ya kwamba mtu hakuwa Mungu wala hakutoka mbinguni. Mtu wa kwanza aliitwa Adam kwa sababu aliumbwa kwa "adama" ambayo ina maana ya udongo wa dunia (mtu akifa tunasema ametoka mavumbini, amerudi mavumbini).
Adam aliumbwa katika picha na ufanano wa Muumba (Mungu), kuumbwa kwa ufanano huo, hakuachi wasiwasi wowote ya kwamba Mtu alifanana na Mungu kimwili, kimuonekano wa nje na ndani. Je mtu angewezaje kufanana na muumba wake? Mtu alitengenezwaje? (Majibu utayapata mbeleni).
Mnamo mwaka 1859 Charles Darwin alichapisha utafiti wake kuhusu evolution "On the Origin of Species by Means of Natural Selection, or the Preservation of Favoured Races in the Struggle for Life". Darwin kutokana na utafiti wake huo, alihitimisha kwa kusema kwamba, viumbe hai wote akiwemo mwanadamu ni matokeo ya mabadiliko(evolution by natural selection). Mwanzoni kanisa lilikuja juu kwa kumpinga lakini badae kadri wanasayansi na watafiti walivyozidi kutoa machapisho yao, kanisa likakubaliana.
Lakini je tumetokana na apes, kama ni hivyo mbona wa sasa hawabadiliki. Evolution kwa ujumla inaweza kuelezea matukio yaliyosababisha mabadiliko ya maisha na aina mbali mbali za maisha zilizokuwepo duniani, kuanzia kwenye kuumbwa kwa mtu, lakini evolution haiwezi kuelezea kuhusu uwepo wa binadamu wa sasa (modern man/Homo sapiens) na haina udhibitisho wowote wa kuonyesha jinsi mabadiliko ya ghafla kutoka Homo erectus kwenda Homo sapiens yalivyotokea.
Hominid ya genus Homo ni matokea ya evolution, lakini Homo sapiens ni matokea ya tukio la mabadiliko na mapinduzi ya haraka sana. Homo sapiens(binadamu wa sasa), ilitokea miaka 300,000 iliyopita, muda ambao ni wa karibu sana.
Watafiti na wanasayansi hawana maelezo ya nini kilitokea, kupelekea mabadiliko ya ghafla hivyo na kutokea kwa binadamu wa sasa, lakini jumbe kutoka sumerians na Babylonian zimeelezea. Agano la kale pia limeelezea.
Homo sapiens-modern man-aliletwa na miungu wa kale (ancient gods).
Aliletwa kivipi? na wapi?. Endelea kufuatilia hapa hapa.
N.B. Andiko hili linaweza lisiishe karibuni kwa sababu nataka niweke kila aina ya ushahidi ili kudhibitisha ukweli huu.