Anne Kilango Malecela ashangazwa na Mkoa wa Kilimanjaro kuwa Pemba ya Tanzania Bara. Adai CHADEMA haitakaa ishike Dola Nchi hii

Wee mama wewe! Heri maneno ya kinywa chako yangekuwa machache.
Mama kumbuka:
Danieli 4:32; .............. Aliye juu ndiye anayemiliki katika ufalme wa wanadamu, naye humpa amtakaye, awaye yote!
Kama una muda mama, soma sura yote ya 4 ya kitabu hicho cha Danieli.

Tena kitabu cha 1Samweli 2:3 kinasema;
Msizidi kunena kwa kutakabari hivyo;Majivuno yasitoke vinywani mwenu;Kwa kuwa BWANA ni Mungu wa maarifa,Na matendo hupimwa na yeye kwa mizani.

Kama haitoshi vile, 1Samweli 2:6 inasema;
BWANA ndiye huinua juu na pia kushusha chini.
Yatafakari haya.
Naomba unisamehe kama nimekukwaza!
 
kauli kama hizi ndio zinafanya wapemba wadai nchi yao
waache na wapemba kili waliwahi kudai Mariale amka baba West kilimanjaro .Halafu hawa wana ccm shida yao ni cdm,,,,hiv wamesahu G55 walikuwepo na kulikuwa na mfumo.wa chama.kimoja...
 
yeye alikuwa kiongozi kwa muda gani na alikuwa ccm ni maendeleo yapi aliyowaletea watu jimboni kwake.atakuwa kasahau tu.
 
Huyu mama aliwahi kuwa waziri au naibu waziri, yy anatoka kilimanjaro wilaya aliyotoka nakatika wilaya zenye maendeleo duni mkoa wa kilimakiaro, lakini ni katika wilaya zenye maendeleo ya juu sanaukilinganisha na wilaya mikoa ya dodoma, tabora, geita, simiyu na katavi
 
Kama upinzani hawawezi kushika dola, Kwanini mnategemea jeshi la police, Kwanini hamtaki tupate tume huru ya uchaguzi, Katiba mpya? Tatizo wabunge wa ccm wanaona watanzania ni mafala. Hakuna sehemu mnayoshinda uchaguzi kihalali. Wizi wa kura ni tabia yenu! siku inakuja nayo haiko mbali Mungu atakapochoka na maigizo yenu hamtaweza kuyasema haya maana wengi wenu mtakua magereza.
 
Yeye sio mungu iwe Leo ama kesho ccm wataondoka tu wameondoka kina Hitler na musolin sembuse hawa wapayukaji
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…