Anguko la watetezi laja

Anguko la watetezi laja

Changamoto za kumtukana Rais wa Nchi ndio kipimo cha Uongozi bora!? Be serious even for a second!
Trump kiongozi wa so called "the free world" kutwa akiguswa anatokwa mapovu na kufukuza watu kazi hovyo hovyo. Juzi kati Jim Acosta wa CNN alinyang'anywa access pass ya White house sababu alimuuliza Trump maswali ambayo hayakumpendeza. Je huo haukuwa uamuzi wa kuwafunga watu midomo huko Washington!?
Mjitafakari Wanaharakati!
Mkuu ni wapumbavu tu ndio wanaweza kutokana rais au kiongozi wao, mjinga kamwe hawezi kufanya hivo. hao unao waona ni wapumbavu.UMENIELEWA.

Trump hufukuza tu, bali hapa kwetu tunaona mtu anaempa changamoto rais anapata tabu na misukosuko sana mara nyingine hadi kupotezwa ingawa hatutuhumu kwa ni rais kwa maana ya taasisi wanafanya hivo.

Ila tujnachojiuliza ni kwamba kwanini hayo hutokea wakati rais anapewa changamoto.

Kuna njia nyingi za kushughulikia hayo bila kuonesha kama unakandamiza demokrasia.
 
Yeremia 51:6 kimbieni kutoka Babiloni, kimbieni ili mwokoe uhai wenu. Msiangamie kwa sababu ya kosa Lake.
Kwa maana ni wakati wa kisasi cha Yehova.. Atamlipa kulingana na matendo yake.
Ufunuo 18:2 naye akasema kwa sauti yenye nguvu: "Ameanguka! Babiloni Mkubwa ameanguka naye amekuwa makao ya roho waovu na mahali pa kuvizia pa kila roho mchafu....
 
Kwani sheria mpya ya mafao si inaweza rudi bungeni..kwani ndio msaafu kwamba haibadiliki?? Kama mnalilia kubadilishwa katiba itashindikana sheria ya mafao..?
Hao wageni waliokuwa wanatukana serikali wamepewa nafasi purposely kuonyesha watanzania kuwa mambo ambayo upinzani huyapigia kelele je wakipewa nafasi wanaweza..kwa maana nyingine kushindwa kwa hawa jamaa ni kushindwa kwa upinzani..
Unaota mchana kweupe, mtu anaunga mkono juhudi za mwenyekiti wa chama halafu matokeo mabaya yahusishe upinzani, wapi na wapi.
 
Kwahiyo umeona huo ndio mfano, vp kufumuliwa marinda bako kukoje

Changamoto za kumtukana Rais wa Nchi ndio kipimo cha Uongozi bora!? Be serious even for a second!
Trump kiongozi wa so called "the free world" kutwa akiguswa anatokwa mapovu na kufukuza watu kazi hovyo hovyo. Juzi kati Jim Acosta wa CNN alinyang'anywa access pass ya White house sababu alimuuliza Trump maswali ambayo hayakumpendeza. Je huo haukuwa uamuzi wa kuwafunga watu midomo huko Washington!?
Mjitafakari Wanaharakati!
 
Tumeshuhudia baadhi ya wadau kutoka mitandao ya kijamii mfano Jamii forums waliokuwa wakipigana kufa na kupona kuitetea serikali ya awamu ya tano wakianza kutundika daluga.

Watetezi hao waliojinasibu kuwa ni Kijani lialia huwaambii kitu kuhusu bwana yule na serikali yake sasa akili zimeanza kuwarudi huku tayari wakiwa hawawezi kumdhibiti tena bwana yule.

Sababu kubwa za hawa watetezi wa yule bwana kutundika daluga ni nyingi kutokana na trend ya hali halisi ya mambo mapya yanayolipuka kila siku ambayo mtanzania yeyote hawezi achwa kuguswa na jambo lolote.

Hizi ni sababu chache kwanini wengi watachomoka kwa kasi kulipisha kundi linalotumika kutetea ushindi kwa kutumia virungu na moshi wa kuwasha.

1. Sheria mpya ya mafao ya wastaafu
Hapa sio siri tutegemee watu wengi kama sio kujionyesha waziwazi basi watakaa kimya, hakuna ubishi kuwa chama cha bwana mkubwa kinapata sapoti kutoka kwa watu waliozaliwa muda mrefu yaani 1970 kurudi chini ambao wengi wao ndo wapo katika muda/ wanakaribia kustaafu sasa hapa wameguswa na kugundua kuwa walichokua wanakitetea kimewatia umaskini.

2. Wageni kupewa nguvu katika chama
Hakuna kitu kinauma kama kumtusi mtu mtandaoni baada ya muda mfupi anaapishwa na kuwa Naibu Waziri inatia hasira maana inakufanya uonekane kigeugeu maana kutoka kumuita mtu "anayetumika na mabeberu" hadi kumuita muheshimiwa.
Hii inawapa simanzi wadau wengi mtandaoni.

3. Songesha point nyingine hapo chini.........
.......
.......
Mbona Hauwataji Hao Watu?
 
10 Usiogope mambo yatakayokupata; tazama, huyo Ibilisi atawatupa baadhi yenu gerezani ili mjaribiwe, nanyi mtakuwa na dhiki siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima.
Ufunuo wa Yohana 2:10
 
Zigo la misumari halibebeki, wamechoka kudeki mikojo ya bwana yule chini.wanadeki anakojoa wanadeki anachafua.
 
Akina Barbarosa, Kipara Kipya, Cocochanel, Britanica,Lakisipesa na wenzao tayari wameshakiri kuchoka.

Bado kuna maroboti matatu dada ISIS, dada Dokta Love na Mgonjwa Mtambuka wao dawa ndio inaanza kupenya kwenye mfupa.
Nimeshangaa sana ingizo jipya Kipara kipya naye kacheua ! Hakika shetani hana rafiki .
 
WARUMI 13;

1Kila mtu anapaswa kuwatii wenye mamlaka katika serikali; maana mamlaka yote hutoka kwa Mungu; nao wenye mamlaka wamewekwa na Mungu. 2Anayepinga mamlaka ya viongozi anapinga agizo la Mungu; nao wafanyao hivyo wanajiletea hukumu wenyewe, 3Maana, watawala hawasababishi hofu kwa watu wema, ila kwa watu wabaya. Basi, wataka usimwogope mtu mwenye mamlaka? Fanya mema naye atakusifu; 4maana yeye ni mtumishi wa Mungu anayefanya kazi kwa faida yako. Lakini ukifanya mabaya, basi, huna budi kumwogopa, maana anao kweli uwezo wa kutoa adhabu. Yeye ni mtumishi wa Mungu na huitekeleza ghadhabu ya Mungu kwao watendao maovu. 5Kwa hiyo ni lazima kuwatii wenye mamlaka, si tu kwa sababu ya kuogopa ghadhabu ya Mungu, bali pia kwa sababu dhamiri inadai hivyo. 6Kwa sababu hiyohiyo ninyi hulipa kodi; maana viongozi hao humtumikia Mungu ikiwa wanatimiza wajibu wao. 7Mpeni kila mtu haki yake; mtu wa ushuru, ushuru; wa kodi, kodi; na astahiliye heshima, heshima.
8Msiwe na deni kwa mtu yeyote, isipokuwa tu deni la kupendana. Ampendaye jirani yake ameitekeleza Sheria. 9Maana, amri hizi: "Usizini; Usiue; Usitamani;" na nyingine zote, zimo katika amri hii moja: "Mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe." 10Ampendaye jirani yake hamtendei vibaya. Basi, kwa mapendo Sheria yote hutimizwa.

11Zaidi ya hayo, ninyi mnajua tumo katika wakati gani: sasa ndio wakati wa kuamka usingizini; naam, wokovu wetu u karibu zaidi sasa kuliko wakati ule tulipoanza kuamini. 12Usiku unakwisha na mchana unakaribia. Basi, tutupilie mbali mambo yote ya giza, tukajitwalie silaha za mwanga. 13Mwenendo wetu uwe wa adabu kama inavyostahili wakati wa mchana; tusiwe na ulafi na ulevi, uchafu na uasherati, ugomvi na wivu. 14Bwana Yesu Kristo awe vazi lenu; msishughulikie tena tamaa zenu za maumbile na kuziridhisha.
Andiko hawakuandikiwa wenye mamlaka ya kupitia mlango wa nyuma. Ni mamlaka ambayo Mungu mwenyewe anajua wana uhalali.

Na ushahidi upo wazi tunashuhudia laana katika nchi yetu ambayo haijawahi kutokea. Kuna fitina chuki faraka zisizo na mfano. Hii inathibitishwa na andiko kuwa mtawala akiwa batili nchi inalaaniwa.

Je si kweli kuwa heri jana kuliko leo?
 
Back
Top Bottom