Mfukutuzi
JF-Expert Member
- Feb 15, 2015
- 239
- 175
Ni suala lisilo na ubishi kuwa CCM, bila hata kuwataja wapinzani, itajiua yenyewe pale tu litakapotangazwa jina la mgombea wa Urais Julai 12, na hii inatokana na sababu kuu tatu;
1. Makundi: Hakuna asiyejua kuwa CCM sasa kimekuwa ni chama cha makundi makubwa, makundi hatari yenye ajenda binafsi kupitia mgombea. Nakuhakikishia hakuna kundi litakubaliana kirahisi na mgombea kutoka kundi tofauti, tofauti na makundi ya nyuma ya kuzuka na kupotea, makundi ya sasa ni makundi hatari na yamedhamiria, mfano, lipo kundi linaitwa kundi la Safari ya Matumaini, kundi hili ukiliangalia limebeba watu wenye nafasi kubwa ktk chama na wadhamini wakubwa wa chama, hawa ni watu waliojihakikishia hivyo hawako tayari kumwona mgombea wao anapoteza kwa sababu kupoteza kwake ni kupotea kwa nafasi zao, kama tunavyojua CCM sasa ni chama cha visasi.
Hivyo makundi haya kwa kuwa haliachwa yakachanua yakastawi, hakuna shaka chama kinahaha kuyatuliza lakini haiwezekani kwa sababu kila mmoja anaongea lake, hii ni sindano namba moja ya sumu itakayowaua taratibu toka Julai hadi Oktoba inafika
2. Utanganyika na Uzanzibar: Ili kuwaengua wagombea wenye nguvu watalazimika kutumia sera kama ile iliyomng'oa SITTA kwenye uSpika kwa kusema wanahitaji Mwanamke, katika hili tunajua kabisa watasema ni zamu ya "Mzanzibar", na dalili imeshajionyesha kwamba mfumo umejielekeza kwa mwanachama mchanga Jaji AGUSTINO RAMADHANI ambaye bila kujali kadi yake ya uanachama ni ya mwaka gani, bila kujali anakijua chama kwa kiasi gani mpaka awe Mwenyekiti wa chama watalazimika kumweka kwa sababu wengine wana mizigo ya kashfa hivyo muda hautatosha kwa chama kuanza kuwasafisha, vile vile ni faida kwao kwa Zanzibar na Bara kwa sababu za mchanganyiko wa Dini, yaani Ukristo-Uislamu. Sasa kwa jinsi tu hali ilivyo, wale wa Tanganyika hawataki kuongozwa na wachache, huu nao ni mtifuano mwingine ndani ya chama
3. Uroho wa madaraka: Katika historia ya Afrika na Dunia, CCM imevunja rekodi kwa kutoa wagombea wengi nafasi nyeti kama hii ya uRais, wanajitetea eti ni kukua kwa Demokrasia wakati sababu ni tatu tu; Moja ni kutengeneza jina ili kuonekana na kiongozi ajaye, pili ni jinsi Nchi ilivyoendeshwa kwa miaka hii kumi na mtangulizi wao, hivyo kila mmoja anajiuliza "kama hata huyu kaweza mimi nitashindwaje?", hili ni tusi kubwa. Sababu ya tatu kubwa, ni Uroho wa Madaraka, kama tunavyojua kwa sasa Uongozi sio utumishi tena bali ni Biashara, basi kila mmoja ana hamu ya kufika Ikulu, kila mmoja anatamani kuwa Rais kwa sababu kama Mbunge tu mbali na Mshahara mnono analipwa kiinua mgongo cha Mil.238 vipi kwa Rais?
Ni hili linamfanya kila mmoja atumie mbinu yoyote ile iwe safi au chafu ila tu afike Ikulu, hakuna anayekubali kumpisha mwenzake, hili nalo janga jingine
Ningeweka sababu nyingi za anguko hili ila hizi tatu (ambazo wengi wanaziruka) zinatosha kwa wewe kupata picha ya jinsi Dola hii itakavyoanguka kabla hata ya kufika uchaguzi Oktoba
Mr. ZigZag (#TeamTanzania)
1. Makundi: Hakuna asiyejua kuwa CCM sasa kimekuwa ni chama cha makundi makubwa, makundi hatari yenye ajenda binafsi kupitia mgombea. Nakuhakikishia hakuna kundi litakubaliana kirahisi na mgombea kutoka kundi tofauti, tofauti na makundi ya nyuma ya kuzuka na kupotea, makundi ya sasa ni makundi hatari na yamedhamiria, mfano, lipo kundi linaitwa kundi la Safari ya Matumaini, kundi hili ukiliangalia limebeba watu wenye nafasi kubwa ktk chama na wadhamini wakubwa wa chama, hawa ni watu waliojihakikishia hivyo hawako tayari kumwona mgombea wao anapoteza kwa sababu kupoteza kwake ni kupotea kwa nafasi zao, kama tunavyojua CCM sasa ni chama cha visasi.
Hivyo makundi haya kwa kuwa haliachwa yakachanua yakastawi, hakuna shaka chama kinahaha kuyatuliza lakini haiwezekani kwa sababu kila mmoja anaongea lake, hii ni sindano namba moja ya sumu itakayowaua taratibu toka Julai hadi Oktoba inafika
2. Utanganyika na Uzanzibar: Ili kuwaengua wagombea wenye nguvu watalazimika kutumia sera kama ile iliyomng'oa SITTA kwenye uSpika kwa kusema wanahitaji Mwanamke, katika hili tunajua kabisa watasema ni zamu ya "Mzanzibar", na dalili imeshajionyesha kwamba mfumo umejielekeza kwa mwanachama mchanga Jaji AGUSTINO RAMADHANI ambaye bila kujali kadi yake ya uanachama ni ya mwaka gani, bila kujali anakijua chama kwa kiasi gani mpaka awe Mwenyekiti wa chama watalazimika kumweka kwa sababu wengine wana mizigo ya kashfa hivyo muda hautatosha kwa chama kuanza kuwasafisha, vile vile ni faida kwao kwa Zanzibar na Bara kwa sababu za mchanganyiko wa Dini, yaani Ukristo-Uislamu. Sasa kwa jinsi tu hali ilivyo, wale wa Tanganyika hawataki kuongozwa na wachache, huu nao ni mtifuano mwingine ndani ya chama
3. Uroho wa madaraka: Katika historia ya Afrika na Dunia, CCM imevunja rekodi kwa kutoa wagombea wengi nafasi nyeti kama hii ya uRais, wanajitetea eti ni kukua kwa Demokrasia wakati sababu ni tatu tu; Moja ni kutengeneza jina ili kuonekana na kiongozi ajaye, pili ni jinsi Nchi ilivyoendeshwa kwa miaka hii kumi na mtangulizi wao, hivyo kila mmoja anajiuliza "kama hata huyu kaweza mimi nitashindwaje?", hili ni tusi kubwa. Sababu ya tatu kubwa, ni Uroho wa Madaraka, kama tunavyojua kwa sasa Uongozi sio utumishi tena bali ni Biashara, basi kila mmoja ana hamu ya kufika Ikulu, kila mmoja anatamani kuwa Rais kwa sababu kama Mbunge tu mbali na Mshahara mnono analipwa kiinua mgongo cha Mil.238 vipi kwa Rais?
Ni hili linamfanya kila mmoja atumie mbinu yoyote ile iwe safi au chafu ila tu afike Ikulu, hakuna anayekubali kumpisha mwenzake, hili nalo janga jingine
Ningeweka sababu nyingi za anguko hili ila hizi tatu (ambazo wengi wanaziruka) zinatosha kwa wewe kupata picha ya jinsi Dola hii itakavyoanguka kabla hata ya kufika uchaguzi Oktoba
Mr. ZigZag (#TeamTanzania)