Angry Rafael Benitez says he will leave Chelsea in May 2013

Angry Rafael Benitez says he will leave Chelsea in May 2013

Rafa Benitez wakati anafundisha Liverpool mbona alikuwa anapendwa ingawa alikuwa ni Mspanish,hizo media hazikuwepo?

Mkuu, hivi unazifahamu media za Waingereza kwa undani zilivyo au na wewe ni mmoja kati ya wale ambao wameisha uvaa mkenge wa hizi media.

Hivi huwa unafuatilia Press conference za ijumaa au talk sport radio kabla ya mechi za jumamosi kuelewa kwa undani kilichoko nyuma ya media nyingi za hapa kwa kila Manager.

Nimekwambia sumu aliyoinywa Benitez ni kuzi accuse media kama zinakuwa bias (kitu ambacho ni kweli) huku akitoa mfano wa Sir Alex Furguson.


Unakumbuka uhasama wa Benitez na Mourinho (Liverpool Vs Chelsea ) hasa baada ya Liverpool kuwatoa Chelsea kwenye Champs League baada ya goli la utata la Luis Garcia ambalo Mourinho alisema sio halali.

Ugomvi wa SAF na Benitez haujaanza leo ulikuwepo tangu kipindi Benitez akiwa Liverpool tena bora hata sasa hivi haujaonekana,unataka kutuambia Liverpool walimfukuza sababu ya ugomvi wake na SAF?

Media za Uingereza huwa zinatafuta kwanza mahari pa kuanzia ndiyo maana kwa mtu asiyezifahamu anaweza usijue picha nzima ikoje. This people are cunning na kwa kufanya hivi, huwa wanawaokota wapenzi au washabiki wengi sana.

Kama wachezaji wanaohama timu moja kwenda nyingine wanazomewa(ACole,Nasri,Parker,Tores),unategemea kwa makocha ndio itakuwa kinyume? David Moyes akihamia Liverpool mashabiki wa Everton hawatamzomea?

Kweli wewe huelewi. Ngoja nikupe mfano hai wa media za waingereza zinavyosaidia Manager ambaye ni Mwingereza. Kama una kumbukumbu, mwaka 2004 Harry Redknapp alihama kutoka Portsmouth kwenda Southampton timu ambayo ni wapinzani wakubwa. Washabiki na wapenzi wa Portsmouth waliamua kumzomea kila mechi na wengine wakatengeneza placard lakini kwa vile media zinampenda, Media nyingi za Kiingereza zilianza kuwalaaumu hao mashabiki na wapenzi kwa kitendo chao cha kumuita Harry majina kama Judas, Scummer and Rot in hell. watu walikuwa discouraged na media kufanya hivyo, matokeo yake kelele hizo zikawa hazina nguvu yoyote ile. Hizi ndizo media za Waingereza.

Huwezi kusikia media zinawasimanga watu wanaomzomea Benitez, badala yake zinachagiza vitendo vyao. Hii ndiyo tofauti ya media za hapa UK.
 
Mourinho,

Mashabiki wa Chelsea wanakulilia wewe kwa sababu kuna uwezekano wa wewe kuwa available mwisho wa msimu

Akichukua tu kombe la Champions League na Madrid kuna uwezekano mkubwa wa kurudi "nyumbani" but you never know!
 
Last edited by a moderator:
"They could be playing Europa League again next season and not the Champions league" : BENITEZ

Hiyo statement ni nzito sana kutolewa na kocha anayepigania kuqualify for champions league spot.

May be something will happen sooner than later, halafu the next game for Blues is Vs West Brom, na kipigo hapo yanaweza kumkuta ya AVB na RDM.
 
  • Thanks
Reactions: EMT
You do not know what you are talking about man!
RAFA OUT!

I do know, the fans are disgraceful..all Rafa wants is the fans getting behind the team and supporting it, but the fans are too hateful to admit that.
 
Chelsea doesnt deserve Rafa.

Rafa is a honest fellow who deserves utmost respect from Chelsea fans.

Move on Rafa..God be with you.

From the fans point of view alichosema Rafa dhidi ya Chelsea wakati akiwa Liverpool, ha-deserve kuwa manager wa Chelsea.
 
I'm sorry for him, Once the media in England start gang up on Football Manager (Foreign). No chance, will have to go. Interesting, they can't find any better English Football Manager.
The Media are warming up for Arsene Wenger as well, but the man is embeded to the club body and some section of club member and supporter.

Kwa suala la Rafa sidhani kama ni media, bali ni mashabiki wengi ndiyo hawamtaki.

Lakini amepata fundisho. If you want to manage more than one team in future, then don't say bad things about other teams.

Hata kama ingekuwa Everton au Manchester United, sidhani kama mashabiki wao wangekaa kimya.
 
Kosa lake kuu ni pale alipolalamika kama Sir Alex Furguson is UNTOUCHABLE na anapata special treatment kwenye media kwa vile waandishi wengi wanamgwaya. Maneno haya yalikuwa ndiyo sumu kwake hasa ikichukuliwa yeye ni foreigner. Huu ndiyo ukweli.

Hilo lilikuwa kosa lake dhidi ya Man Utd lakini siyo Chelsea. Bifu ya mashabiki wa Chelsea dhidi ya Rafa haihusiani kabisa na aliyosema Rafa juu ya Fergie.

Wakati akiwa Liverpool alisema wazi kuwa he would never manage Chelsea and criticised Chelsea fans saying that they needed plastic flags to get behind their team.

What goes around, comes around. Angewaomba msamaha labda wangemkubali. Lakini yeye kajifanya kichwa ngumu.
 
Mie naongea Kama Mshabiki wa Liverpoolfc, Naanza kwa kutolewa kwake Rafael Benitez na Tabia ya Benitez kwa wachezaji kwa Maoni yangu lakini.

1. Benitez kufukuzwa LFC sio kwa kufanya vibaya LFC alifukuzwa kumbuka na Tom Hicks na Gillet ambao Benitez na hao watu walikuwa hawaelewani na ni Mashabiki wachache sana na hao Gillet na Hicks ndio chanzo cha uharibifu wamambo mengi hapo LFC walitaka Benitez atolewe na pia Media ilichangia ila sio sana na kwa Maoni yangu Benitez anapofaa ni LFC na MAshabiki asilimia kubwa wapo tayari Benitez kurudi Liverpoolfc. Uharibifu aliofanya Benitez LFC ni mdogo sana maybe kuuza Alonso na pia anatabia ya ku act kama Mwalimu Mkuu wa Shule akiweza kujirekebisha hilo ok Wachezaji wasikuhizi pesa zinawapa kiburi.

2.Benitez na Chelsea sasa Na MAshabiki wa Chelsea - Benitez alijuwa wazi Chelsea Fan hawatompenda na alijuwa wazi atakaa mwaka tu pale pesa ndio aliyoifata alikuwa nje ya game muda mwingi. Mashabiki wa Chelsea toka kufika walimchukia sababu ile Rival ya Morinho to Liverpool na Benitez to Chelsea na mitoano ile ya CL na FA mie nashangaa Chelsea Fan mbona hata Valencia alimtoa Liverpool mara 2 na Benitez alipokewa? Chelsea Fan wanasema wao wanalipa pesa Je Abromovich hawapi hiyo pesa bila Abromovich Chelsea ingekuwa wapi? na kama kweli mna power Fan wa Chelsea mtukuneni Abromovich basi.

3. Chelsea na De Matteo ni kweli De Matteo kila mtu hawezi kukataa kwamba hakutakiwa kufukuzwa watu humsifia kwamba ameshinda FA na CL kwa muda mfupi je hapo hamuoni kama Tatizo ni Player Power Chelsea? mtu miezi 3 umeshinda CL na FA kweli? ndio Best Manager na ile miezi ya nyuma vipi AVB asisifiwe kazi yake? tatizo linaonekana Jeuri ni Players na Abromovich hakuliona hilo alitakiwa alijue kwamba ok Player tatizo ila kwa De Matteo wametulia sababu wanampenda abaki, Chelsea timu bwana sio mbovu sababu ya Manager Chelsea wachezaji ni wajeuri kama mtu hawampendi na game haiendi chunguzeni Manager wote mtaona timu sio ndio hivyo hivyo? basi akae Terry Care Taker ishinde game 3 tizameni sifa kutoka Media na Fan na Player namna watavyocheza.

EPL Ma MAnager ni Sir Alex na United heshima kwa mashabiki wao heshima kwa player na Arsene Wenger HEshima anakuwa nazo kwa Player na Mashabiki pia Benitez alikuwa ni LFC tu hivyohivyo tatizo aliondoshwa mapema na chuki zao Hicks and Gillet ila wangepigwa chini Hicks na Gillet Benitez bado yupo LFC basi ingekuwa mbali. Chelsea Fan kila mtu anawajua hawana tofauti na Owner bora huyo mwenye timu anawatakia mafanikio. Scolari aliyesema hayo Player ndio chanzo cha mafanikio mabovu. Benitez tatizo lake kwenye kupenda kubadilisha wachezaji tu kila game akitaka afanikiwe arudi kwao Spain au kama kuwa England basi LFC wamrudishe.
 
"They could be playing Europa League again next season and not the Champions league" : BENITEZ

Hiyo statement ni nzito sana kutolewa na kocha anayepigania kuqualify for champions league spot.

May be something will happen sooner than later, halafu the next game for Blues is Vs West Brom, na kipigo hapo yanaweza kumkuta ya AVB na RDM.

Baada ya rant yake ya jana kuna some breaking news kuwa amesema ana uhusiano mzuri na Abramovich.

Chelsea interim boss Rafael Benitez has told BBC Sport he has an "excellent" relationship with owner Roman Abramovich and he will be at the club until the end of the season: BBC Sport - Rafael Benitez wants to stay at Chelsea until end of the season

Nafikiri ni baada ya bodi ya Chelsea kukaa leo na kumwambia apooze alichosema jana?

Otherwise, kwa aliyosema jana tuu, he deserved the sack hata kabla ya May.
 
Mm mpaka sasa sijaona alichofanya, bora aondoke tu.

Sent using wireless by wire
 
I do know, the fans are disgraceful..all Rafa wants is the fans getting behind the team and supporting it, but the fans are too hateful to admit that.

How could the fans get behind him whilst he told them when he was at Liverpool that he will never manage Chalsea and further that they should carry plastic flags to support their team?

Si alisema hatakaa aifundishe Chelsea? What is he doing now? The fans has a valid case here.

Angekuwa wa maana angewaomba msamaha, mambo yaishe.

Why for him "Sorry Seems to Be the Hardest Word" to say?

Badala yake he wants to take them for granted.

 
Last edited by a moderator:
How could the fans get behind him whilst he told them when he was at Liverpool that he will never manage Chalsea and further that they should carry plastic flags to support their team?

Si alisema hatakaa aifundishe Chelsea? What is he doing now? The fans has a valid case here.

Angekuwa wa maana angewaomba msamaha, mambo yaishe.

Why for him "Sorry Seems to Be the Hardest Word" to say?

Badala yake he wants to take them for granted.

Mkuu "MONEY TALK" na anajuwa hatokuwa muda mrefu ndomana naye anafanya ujeuri ila Chelsea Kama nilivyosema Manager pale ni Morinho hata aje nani pale ni ngumu ukitaka kujuwa wachezaji wa Chelsea ni jeuri kwa mtu kama Scolari tu AVB alifanyiwa fitina na wachezaji kama kipindi cha Scolari kutolewa ndio kina Drogba kina Lampard kina Terry wakaanza kujikamua sioni Benitez kumaliza May na kama Chelsea hawajamrudisha Morinho basi hata aje nani mambo yatazidi kuwa mabaya. na Benitez kashayajua ndomana naye anawatemea mate Chelsea kwa makusudi yeye hajali anapokea pesa yake basi.
 
2.Benitez na Chelsea sasa Na MAshabiki wa Chelsea - Benitez alijuwa wazi Chelsea Fan hawatompenda na alijuwa wazi atakaa mwaka tu pale pesa ndio aliyoifata alikuwa nje ya game muda mwingi. Mashabiki wa Chelsea toka kufika walimchukia sababu ile Rival ya Morinho to Liverpool na Benitez to Chelsea na mitoano ile ya CL na FA mie nashangaa Chelsea Fan mbona hata Valencia alimtoa Liverpool mara 2 na Benitez alipokewa? Chelsea Fan wanasema wao wanalipa pesa Je Abromovich hawapi hiyo pesa bila Abromovich Chelsea ingekuwa wapi? na kama kweli mna power Fan wa Chelsea mtukuneni Abromovich basi.

Rival kati ya Liverpool na Chelsea ilianza kwa sababu ya Rafa na Mourinho. Kabla ya hapo kulikuwa hakuna rival yoyote.

This is exactly what he said miaka mitano iliyopita wakati akiwa Liverpool na bado inawauma mashabiki wa chelsea mpaka leo:

"Chelsea is a big club with fantastic players, every manager wants to coach a such a big team,' said the Spaniard. ‘But I would never take that job, in respect for my former team at Liverpool, no matter what. For me there is only club in England, and that's Liverpool." Read more: Rafa Benitez Chelsea manager: I'd never take Stamford Bridge job | Mail Online

Halafu mtu kama huyo leo anataka ku-manage Chelsea whilst to him the only club in England ni Liverpool? Si arudi tuu Anfield?

Tena bado anapendwa pale. Tena pamoja na kufundisha Chelsea anaishi huko huko Liverpool, which makes it difficult to see him in charge at Chelsea.

But the killer was this one.

article-2236795-16265F8D000005DC-347_634x702.jpg
 
benitez_2495723b.jpg Mzeee Mzima ana Smile lol Pesa Mchezo huyu anawafanyia kusudi lol kina Terry hapo wapo wapi?
 
Kwa suala la Rafa sidhani kama ni media, bali ni mashabiki wengi ndiyo hawamtaki.

Lakini amepata fundisho. If you want to manage more than one team in future, then don't say bad things about other teams.

Hata kama ingekuwa Everton au Manchester United, sidhani kama mashabiki wao wangekaa kimya.

Ni kweli alikuwa na tatizo na washabiki wa CFC lakini hii imekuwa amplified na media baada ya kupewa kazi na mpaka leo bado kwenye talk sport radio, press conference na kwenye magazeti kila kinachoongelewa ni maneno aliyosema. Mbona ilitokea kwa manager wengine ( UK) lakini kwa kutokukuzwa na media na radio mambo yalipowa na wakaendelea na kazi.
 
Mkuu "MONEY TALK" na anajuwa hatokuwa muda mrefu ndomana naye anafanya ujeuri ila Chelsea Kama nilivyosema Manager pale ni Morinho hata aje nani pale ni ngumu ukitaka kujuwa wachezaji wa Chelsea ni jeuri kwa mtu kama Scolari tu AVB alifanyiwa fitina na wachezaji kama kipindi cha Scolari kutolewa ndio kina Drogba kina Lampard kina Terry wakaanza kujikamua sioni Benitez kumaliza May na kama Chelsea hawajamrudisha Morinho basi hata aje nani mambo yatazidi kuwa mabaya. na Benitez kashayajua ndomana naye anawatemea mate Chelsea kwa makusudi yeye hajali anapokea pesa yake basi.

Kweli some chelsea senior players ni jeuri na ndiyo maana wanataka kuwa-face out. Ndiyo maana pamoja na media kutaka Lampard aongezewe mkataba, the board seems to phase him out.

Lakini kwa suala la Rafa, it has to do more with the fans. Kutokana aliyoyasema huko nyuma dhidi ya Chelsea and particularly its fans, sidhani kama wangemkubali.

The guy is very stubborn as well. Ukiwa kama Liverpool fan you should know his stubborn more than anyone else.
 
Ni kweli alikuwa na tatizo na washabiki wa CFC lakini hii imekuwa amplified na media baada ya kupewa kazi na mpaka leo bado kwenye talk sport radio, press conference na kwenye magazeti kila kinachoongelewa ni maneno aliyosema. Mbona ilitokea kwa manager wengine ( UK) lakini kwa kutokukuzwa na media na radio mambo yalipowa na wakaendelea na kazi.

Sidhani kama limekuwa amplified na media, bali yeye ndiye ame-amplify suala zima kwenye media.

He started it himself five years ago that he will never manage Chelsea.

Alisema "For me there is only club in England, and that's Liverpool."

Ndiyo maana hata timu nyingine za Uingereza hazikutaka kumwajiri simply because of what he said.

Kwa hiyo, anapokuja kumeneji timu nyingine zaidi ya Liverpool why should the people not be entitled to question him?

Has he changed his stance? Or pamoja na kumanage Chelsea still "For [him] there is only club in England, and that's Liverpool"?

Kwa mameneja wengine hasa wa Kiingereza huwa wanakuwa makini zaidi na wanavyoongea na media.

Mbona watu kama Harry Redknapp hawasemi ovyo ovyo?

Rafa thought "he will never walk alone" but he is now.
 
From the fans point of view alichosema Rafa dhidi ya Chelsea wakati akiwa Liverpool, ha-deserve kuwa manager wa Chelsea.
he is already the manager..that history should be put to rest for the good of the team. Beef baadae, sahivi inabidi wamsupport jamaa.
 
Back
Top Bottom