Nina rafiki yangu ambaye tumeshibana saana kwa kauli nyingine sio rafiki tena ni ndugu kabisa.
Huyo rafiki yangu baba yake ni mgonjwa saana anaumwa sana. Tulikwenda naye hospitali wakasema anahitaji kufanyiwa upasuaji tumboni mwake na hili afanyewe hivo kuna pesa fulani ambazo wanaomba hili apate kutibiwa.
Sasa kuna pesa ambazo nilipewa na familia yangu baada ya dada zangu kuolewa wazazi wakaona zile pesa tufanye nazo biashara wakanipa mimi kama mtoto wao wa kiume. Na kwenye plan yangu ya biashara nilikuwa nipo na huyu ndugu yangu (rafiki) tulikuwa tuna panga wote.
Sasa baada ya baba yake kuumwa hizo pesa anaomba eti ni msaidie hili amtibishe baba yake najaribu kumwambia nitampa nusu kwa bahati mbaya nusu nyingine hana kwa hiyo anaomba pesa zangu eti Mungu atanilipa utu wa mtu ni muhimu kuliko pesa. Na kweli mzee wake ni mgonjwa saana na asipo tibiwa mapema ni Mungu tu
Mimi na shindwa na la kufanya kabisa
Yaani sijui nikimpa wazazi nitawapa taarifa gani au nitapata wapi tena pesa zingine. Nahisi na changanikiwa kabisa
Naona sina bahati kabisa.
Sijui naombeni ushauri