Black listed
Senior Member
- Apr 6, 2023
- 181
- 260
Unataka kusema nini!??Kibiolojia, kuna makundi makuu mawili ya viumbe hai hapa duniani. Kundi la kwanza linaitwa mamalia (animalia), na la pili ni mimea (plantae).
Kwenye kila kundi bado kuna mgawanyiko (classification). Kundi la mamalia tupo sisi binadamu na wanyama (hayawani).
Kuna sifa zinazotofautisha kati ya viumbe hawa wawili (binadamu na wanyama). Sifa hizo ni namna ya kutembea, aina ya vyakula tulavyo, nk. Lakini sifa kuu inayotufautisha wanadamu na wanyama ni akili na utashi (ustaarabu).
Ni kutokana na akili na utashi, maisha ya wanadamu yamejengwa katika misingi itakayomtofautisha na wanyama. Misingi hii ni sheria, mila, tamaduni, nk.
Misingi hii ipo katika ngazi ya taifa, mikoa, wilaya, tarafa, kata, vijiji, ukoo, hadi ngazi ya familia. Na ndio maana mtu akikiuka misingi katika ngazi yoyote huhukumiwa kulingana na ngazi husika.
Watu wengi hutii sheria za ngazi za juu tu, lakini hawatii sheria za ngazi za chini. Labda hii inatokana na uwajibikaji wa mamlaka ya ngazi hizo kuwawajibisha (kuwaadhibu) wale wote wanaoenda kinyume na sheria.
Katika ngazi za familia, na hata ukoo, watu wamekuwa wakikiuka mila, desturi, na utamaduni ambavyo ndio sheria zinazowalinda na kuwatambulisha.
Watu wanaharibu sifa ya familia au ukoo kwa kufanya mambo ambayo wanahisi kwao yana masilahi. Watu wa aina hii, wengi wao ni wabinafsi, na anafanya hivyo ili kuwaonyesha watu kwamba yeye ni wa kipekee, tofauti na familia au ukoo anaokotoka.
Kama kuna jambo jema limetokea ndani ya familia au ukoo wenu, kulitoa jambo hilo nje sio vibaya. Lakini likitokea, kwa bahati mbaya, jambo lisilo jema (labda la kutia aibu familia au ukoo), usilitangaze nje, maana utaharibu sifa ya familia au ukoo, ambako na wewe mwenyewe unatoka.
Utakuta mtu mmoja kutoka katika familia au ukoo fulani ana tatizo na anahitaji msaada kutoka kwa wanandugu. Wewe badala ya kumsaidia unatoka na kwenda kumtangaza vibaya kwa watu wa mbali, kwamba yule jamaa masikini sana, amekuja ameniomba kitu fulani. Unafanya hivyo ili kumharibia sifa yake.
Kuna mambo mengine yanatakiwa kuwa siri ndani ya familia au ukoo; hayatakiwi kutoka nje. Hapo ndipo linakuja suala la mila na desturi. Kila familia na ukoo vina mila tofauti na familia nyingine, japo baadhi zinaingiliana, lakini maadili yatabaki kuwa ndani ya familia na ukoo husika.
Kuna baadhi ya makabila yako makini sana katika suala la kutunza maadili ili kulinda mila, desturi, na tamaduni zao. Baadhi ya mabila haya ni yale ya kaskazini. Makabila haya, mtu akikengeuka, akatoa nje siri za familia au ukoo, atashikwa na kuletwa mbele ya familia au ukoo, atatandikwa fimbo hadhrani, bila kujali umri wake. Akitoka hapo, adabu tele!
Nadhani kila familia au ukoo, vingejiwekea taratibu na sheria za kufuatwa (kuchukuliwa) pindi ikitokea kuna watu wanaharibu mila na desturi, ili kuziepusha na aibu familia na koo husika.
UONGOZI WETU NA HATMA YA TANZANIA.MWALIMU NYERERE ANAMALIZA KWA USHAIRI KWENYE KITABU CHAKE.
UONGOZI WETU NA HATMA YA TANZANIA.
Ole wake Tanzania Tusipoisaidia
Niwezalo nimelifanya kushauri na kuonya nimeonya.
tahadhali nimetoa ushauri na kuonya nimeshatoka kitini zaidi nifanye nini.
Namlilia Jaalia atumulikie njia Tanzania ailinde WAOVU wasiishinde.
Amina Tena Amina Amina Tena amina
UONGOZI WETU NA HATMA YA TANZANIA.
MWALIMU JK NYERERE
NilichokisemaUnataka kusema nini!??
Lini unapepa la bai
Kumbe kuna makundi mangapi ya viumbe hai?HUU NI UONGO NA USHUBWADA,... Hapo kwenye makundi kusema tu kuna animalia na plantae sijasoma uongo uliofuata chini.
Unganisha doti!Lini unapepa la bailogi
Sisi tulisoma makundi kama manne kuna fungi ,animalia ,plantae na bacteria wana jina lao kitaaalimu hao bacteria kama protista..sijajua syllabus yenuKumbe kuna makundi mangapi ya viumbe hai?
Na maadili yanamomonyoka kwa kadiri tunavyosigina mila na tamaduni zetuKama Taifa limeacha mila na destruri zake na kukumbatia tamaduni za wazungu na waarabu unategemea ni nini katika ngazi ya chini
Hizo fungus na bacteria ni makundi madogo ndani ya animaliaSisi tulisoma makundi kama manne kuna fungus ,animalia ,plantae na bacteria wana jina lao kitaaalimu hao bacteria kama proto...sijajua syllabus yenu
Wamegroup maana hazina maana ila zamani tulikuwa tunasoma kingdom 4 ..Hizo fungus na bacteria ni makundi madogo ndani ya animalia
Atafanya upuuzi akiwa nje ya familia au nje ya ukoo......akirudi kundini anashika adabu yake, vinginevyo mboko zitamuhusuPorojo tupu kila jamii ina mila zake na wanafanya huko kweny miji yao ...Maadili yanachangiwa na mazingira mtu hata awe kabila gani akija town anakuja kuharibika.
Hakuna kabila linaloruhusu wanawake wazee kabla ya kuolewa waka kuvaa vinguo vifupi ni nje ya maadilu sasa wwe nenda huko kaskazini ndio utaelewa, watu wanavuta bangi kila kona plus matusi kwao kawaida.
Hivi mkuu hizi reply zako Kuna sehemu umezisave kabisa?MWALIMU NYERERE ANAMALIZA KWA USHAIRI KWENYE KITABU CHAKE.
UONGOZI WETU NA HATMA YA TANZANIA.
Ole wake Tanzania Tusipoisaidia
Niwezalo nimelifanya kushauri na kuonya nimeonya.
tahadhali nimetoa ushauri na kuonya nimeshatoka kitini zaidi nifanye nini.
Namlilia Jaalia atumulikie njia Tanzania ailinde WAOVU wasiishinde.
Amina Tena Amina Amina Tena amina
UONGOZI WETU NA HATMA YA TANZANIA.
MWALIMU JK NYERERE
Nilisoma zamani kidogo, wakati huo syllabus (na vitabu) viliainisha hivyo, hata hivyo ukweli unabaki palepaleSisi tulisoma makundi kama manne kuna fungi ,animalia ,plantae na bacteria wana jina lao kitaaalimu hao bacteria kama protista..sijajua syllabus yenu
Wacha potosha Kama hujui Kingdom zipo tanoHizo fungus na bacteria ni makundi madogo ndani ya animalia
Sawa ndugu, nakubaliana na wewe. Lakini hapo juu nimesema, wakati namjibu Acumen, kuwa, wakati mimi nasoma, kulikuwa na kingdom mbili tu; animalia na plantae.Wacha potosha Kama hujui Kingdom zipo tano
1/Animalia
2/Plantae
3/Monera (Bacterias)
4/Fungi (Fangasi)
5/Protester
So Bacteria na Fungi hawapobkwenye Animalia hizo ni kingdom.