Andy Lentz, kaimu Balozi wa Marrkani nchini Tanzania

Andy Lentz, kaimu Balozi wa Marrkani nchini Tanzania

Bagamoyo

Platinum Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
29,866
Reaction score
34,022
Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania azungumzia mambo mazito yakiwemo umuhimu wa Vyombo huru vya habari, uchaguzi ni kipimo cha uongozi ..


View: https://m.youtube.com/watch?v=N8LT3kmJJmk

AZAM TV wamlitembelea kaimu balozi Andy Lentz na kubadilishana mawazo kuhusu umuhimu wa vyombo vya habari, na vyombo hivyo pamoja na waandishi wake kulindwa.

Mazungumzo hayo kabla ya uchaguzi kaimu balozi alielezea matumaini yake uchaguzi wa tarehe 29 October 2025, ingawa kaimu balozi alitoa angalizo kuwa kuna historia ya vurugu ktk chaguzi

Watalii wapatao 35,000 kutoka Marekani hutembelea Zanzibar na watalii wao ni miongoni mwa watalii wanaotumia pesa nyingi kama watalii kuliko wengine kutoka nchi zinazoleta watalii wengi Tanzania

Upande wa uwekezaji pia katika maeneo mbalimbali kama Zanzibar, Kilimanjaro na Arusha nilitembelea maeneo hayo na kuonana na makampuni ya Kimarekani yanavyofanya biashara na uwekezaji

Kuhusu taarifa zisizo sahihi (misinformation) na kampeni za taarifa potovu (disinformation) ni changamoto. Hivyo walaji wa habari ikuwemo taarifa za mchakato mzima wa uchaguzi wanategemea taarifa sahihi, taarifa za ukweli, taarifa za kiuchunguzi kutoka vyanzo sahihi kutoka vyombo vya habari ikiwemo vya Tanzania kaimu balozi Andy Lentz anakazia

Kuhusu misaada mbalimbali ya Marekani kupitia kodi za raia wake kwa Tanzania ni vizuri serikali mbili kufanya kazi kwa pamoja kama wadau wanaokubaliana kufanya kazi katika namna inayokubalika kwa pande zote mbili yaani Tanzania na Marekani

Kuhusu machafuko yanayotokea duniani swali alilotupiwa kaimu balozi wa Marekani, kaimu balozi wa Marekani anasema inajihusisha sana kuwezesha pande zinazohusika kuwezesha machafuko, vita na madhila yake yakiisha. Marekani tupo ktk mkakati wa kuwezesha pande zinazohusika iwe Gaza, Mashariki ya Congo, Vita ya Ukraine na Russia kuweza kumaliza vita au machafuko.

Kaimu balozi anaongeza katika machafuko kuna pande mbalimbali zinazochochea hali hiyo ikiwemo serikali na magenge yasiyo ya kiserikali (non State actors) ambavyo huchangia hali ya machafuko, vita na mauaji.
 

Vyombo vya habari Tanzania vilikuwa wapi wakati wa uchaguzi? Na pia kwa sasa vipo wapi ?


View: https://m.youtube.com/watch?v=59U95VIFaSA
Tanzania imefanya uchaguzi tarehe 29 Oktoba 2025 ambao mpaka sasa mengi yamejitokeza na kuzusha maswali.

Mojawapo ni nafasi ya vyombo vya habari. Vilikuwa wapi kuwafahamisha yaliyokuwa yakijiri nchini mwao, vilikuwa wapi kuwaarifu nini cha kufanya katika mazingira yaliyoonekana kuwa ya hatari, vilikuwa wapi kuwapa jukwaa la kusema na kutoa maoni yao?
DW
 
Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania azungumzia mambo mazito yakiwemo umuhimu wa Vyombo huru vya habari, uchaguzi ni kipimo cha uongozi ..


View: https://m.youtube.com/watch?v=N8LT3kmJJmk

Screenshot_20251120-220343~2.png
 

Vyombo vya habari Tanzania vilikuwa wapi wakati wa uchaguzi? Na pia kwa sasa vipo wapi ?


View: https://m.youtube.com/watch?v=59U95VIFaSA
Tanzania imefanya uchaguzi tarehe 29 Oktoba 2025 ambao mpaka sasa mengi yamejitokeza na kuzusha maswali.

Mojawapo ni nafasi ya vyombo vya habari. Vilikuwa wapi kuwafahamisha yaliyokuwa yakijiri nchini mwao, vilikuwa wapi kuwaarifu nini cha kufanya katika mazingira yaliyoonekana kuwa ya hatari, vilikuwa wapi kuwapa jukwaa la kusema na kutoa maoni yao?
DW

wakati mwingine tumieni akili hata hiyo kdg..mnarudia rudia kutaja vyombo vya habari tanzania, HAKUNA VYOMBO VYA HABARI TANZANIA..kuna waigizaji wa vyombo vya habri..achaneni nao, wa nini....?
 
wakati mwingine tumieni akili hata hiyo kdg..mnarudia rudia kutaja vyombo vya habari tanzania, HAKUNA VYOMBO VYA HABARI TANZANIA..kuna waigizaji wa vyombo vya habri..achaneni nao, wa nini....?

Vyombo vyote ikiwemo TBC, AZAM, JAMBO TV, MILLARD AYO, CROWN MEDIA n.k vimekuwa taasisi 'chawa', zinafumbia macho kuchambua, kuchunguza au kutoa taarifa wanazofikiri serikali dhalimu ya Tanzania haitaki zijadiliwe, ziulizwe au hata kujengea uwezo raia kupata habari za ukweli.
 
Back
Top Bottom