Anayosema Muhammad (S.W.A) ni kweli

Mhafidhina07

JF-Expert Member
Aug 1, 2014
2,556
2,994
Amani iwe juu yenu.

Nianze kwa kunukuu kutoka sura ya NNAJIM(nyota) aya ya kwanza inasema"hakuna anachosema muhammad isipokuwa wahyi" ni kwamba wengi wanamzushia uchawi na kumwambia mtunga mashairi ila mungu anawaambie wote wanaokebehi kuwa yeye ndiye anaongea kupitia mtume wake.

Wengine wanamwita au kuita uislamu dini ya kichawi kwa uzushi wa kusema wanatumiliwa majini wazuri wakati ni uongo na hata mungu amewaonya binadamu wanaofanya uchawi kwa kuiga/kumzushia maisha ya mtume suleimani kuwa alitumia majini.

Surat Baqara 102 "wapo wanaotenda uchawi na kukufuru kwa kumzushia nabii suleimani ila uchawi huo umetoka kweny mji wa babeli kutoka kwa haruta na maruti.na hawafunz watu mpk kuwaambia hakika yetu sisi ni mtihani,wanafunza watu uchawi na kufarakanisha.
 
Je, ni kweli kuwa majini ni waislamu?

Na ni kwa nini majini yana majina ya kiislamu?
 
Je, ni kweli kuwa majini ni waislamu?
Na ni kwa nini majini yana majina ya kiislamu?
surat jinni aya ya kwanza"hakika imefunuliwa kundi la majini kuwa wamesikia quran yenye uongofu",basi tumeiamini na hatutomshirikisha mungu na viumbe wengine,wapo watu wa kiume wanaomba ulinzi kwa majini lakin hawapati lolote zaidi ya dhambi." hatukata
 
jini kiumbe ila anapoingilia mfumo wa maisha ya kibinadamu anakuwa pepo(shetani) masheikh mnaokutana nao uchochoroni ni njaa ni sawa na manabii wanaotumia nguv za giza.
 
Amani iwe juu yenu.nianze kwa kunukuu kutoka sura ya NNAJIM(nyota) aya ya kwanza inasema"hakuna anachosema muhammad isipokuwa wahyi" ...
Achana na hizo hadithi zisizo na kichwa wala miguu. Hakuna cha mungu wala nini. Hizo zote ni ngonjera ziliandikwa na watu hawajaenda hata darasa la pili.

Achana na hizo mambo hazina ukweli wowote.
 
"hakuna anachosema muhammad isipokuwa wahyi"
Tumia akili ya kawaida, Mungu hawezi kumtuma mwanadamu atamke haya maneno, huyu ni binaadamu mwenye hasira,chuki,jazba,visasi, hasadi,roho mbaya! Narudia tena tumia akili!


(47:4 QURAN)

Surah Muhammad



فَإِذَا لَقِيتُمُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فَضَرۡبَ ٱلرِّقَابِ حَتَّىٰٓ إِذَآ أَثۡخَنتُمُوهُمۡ فَشُدُّواْ ٱلۡوَثَاقَ فَإِمَّا مَنَّۢا بَعۡدُ وَإِمَّا فِدَآءً حَتَّىٰ تَضَعَ ٱلۡحَرۡبُ أَوۡزَارَهَاۚ ذَٰلِكَۖ وَلَوۡ يَشَآءُ ٱللَّهُ لَٱنتَصَرَ مِنۡهُمۡ وَلَٰكِن لِّيَبۡلُوَاْ بَعۡضَكُم بِبَعۡضٖۗ وَٱلَّذِينَ قُتِلُواْ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ فَلَن يُضِلَّ أَعۡمَٰلَهُمۡ



4. Basi mnapo wakuta walio kufuru wapigeni shingoni mwao, mpaka mkiwadhoofisha wafungeni pingu. Tena waachilieni kwa hisani au wajikomboe, mpaka vita vipoe. Ndio hivyo. Na lau angeli taka Mwenyezi Mungu angeli washinda mwenyewe, lakini haya ni kwa sababu akutieni mitihani nyinyi kwa nyinyi. Na walio uliwa katika njia ya Mwenyezi Mungu hatazipoteza a´mali zao.
 
Je, ni kweli kuwa majini ni waislamu?

Na ni kwa nini majini yana majina ya kiislamu?
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

1. Sema: Imefunuliwa kwangu ya kuwa kundi moja la majini lilisikiliza, na likasema: Hakika sisi tumeisikia Qur'ani ya ajabu!

2. Inaongoza kwenye uwongofu, kwa hivyo tumeiamini, wala hatutamshirikisha yeyote na Mola wetu Mlezi.

3. Na kwa hakika utukufu wa Mola wetu Mlezi umetukuka kabisa; hana mke wala mwana.

4. Na kwa hakika wapumbavu miongoni mwetu walikuwa wakisema uwongo ulio pindukia mipaka juu ya Mwenyezi Mungu.

5. Nasi tulidhani kuwa watu na majini hawamzulii uwongo Mwenyezi Mungu.

6. Na hakika walikuwako wanaume katika watu walio kuwa wakitafuta kujikinga kwa wanaume wa kijini; kwa hivyo wakawazidisha madhambi.

7. Na kwa hakika wao walidhani, kama mlivyo dhani nyinyi, ya kuwa Mwenyezi Mungu hatamleta Mtume.

8. Nasi tulizigusa mbingu, na tukaziona zimejaa walinzi wenye nguvu na vimondo.

9. Na hakika tulikuwa tukikaa humo katika baadhi ya makao ili kusikiliza; lakini sasa anaye taka kusikiliza atakuta kimondo kinamvizia!

10. Nasi hatujui kama wanatakiwa shari wale wanao kaa kwenye ardhi au Mola wao Mlezi anawatakia uwongofu.

11. Na hakika katika sisi wamo walio wema, na wengine wetu ni kinyume na hivyo. Tumekuwa njia mbali mbali.

12. Nasi tulijua kuwa hatutomshinda Mwenyezi Mungu duniani, wala hatuwezi kumponyoka kwa kukimbia.

13. Nasi tulipo usikia uwongofu tuliuamini. Basi mwenye kumuamini Mola wake Mlezi basi haogopi kupunjwa wala kudhulumiwa.

14. Na hakika wamo katika sisi Waislamu, na wamo kati yetu wanao acha haki. Basi walio silimu, hao ndio walio tafuta uwongofu.

15. Na ama wanao acha haki, hao watakuwa kuni za Jahannamu.

16. Na lau kama wangeli simama sawasawa juu ya njia tungeli wanywesha maji kwa wingi,

17. Ili tuwajaribu kwa hayo. Na anaye puuza kumkumbuka Mola wake Mlezi atamsukuma kwenye adhabu ngumu.

18. Na hakika misikiti ni ya Mwenyezi Mungu, basi msimuabudu yeyote pamoja na Mwenyezi Mungu.

19. Na hakika Mja wa Mwenyezi Mungu alipo simama kumwomba, wao walikuwa karibu kumzonga!

20. Sema: Hakika mimi namwomba Mola wangu Mlezi, wala simshirikishi Yeye na yeyote.

21. Sema: Mimi sina mamlaka ya kukudhuruni wala kukuongozeni.

22. Sema: Hakika hapana yeyote awezae kunilinda na Mwenyezi Mungu, wala sitapata pa kukimbilia isipo kuwa kwake Yeye tu.

23. Ila nifikishe Ujumbe utokao kwa Mwenyezi Mungu na risala zake. Na wenye kumuasi Mwenyezi Mungu na Mtume wake, basi hakika hao watapata Moto wa Jahannamu wadumu humo milele.

24. Hata watakapo yaona wanayo ahidiwa, ndipo watakapo jua ni nani mwenye msaidizi dhaifu, na mchache wa idadi.

25. Sema: Sijui kama yapo karibu hayo mnayo ahidiwa, au Mola wangu Mlezi atayawekea muda mrefu.

26. Yeye ndiye Mwenye kujua ya siri, wala hamdhihirishii yeyote siri yake,

27. Isipo kuwa Mtume wake aliye mridhia. Naye huyo humwekea walinzi mbele yake na nyuma yake.

28. Ili Yeye ajue kwamba wao wamefikisha ujumbe wa Mola wao Mlezi, na Yeye anayajua vyema yote walio nayo, na amedhibiti idadi ya kila kitu.
 
Amani iwe juu yenu.

Nianze kwa kunukuu kutoka sura ya NNAJIM(nyota) aya ya kwanza inasema"hakuna anachosema muhammad isipokuwa wahyi" ni kwamba wengi wanamzushia uchawi na kumwambia mtunga mashairi ila mungu anawaambie wote wanaokebehi kuwa yeye ndiye anaongea kupitia mtume wake.

Wengine wanamwita au kuita uislamu dini ya kichawi kwa uzushi wa kusema wanatumiliwa majini wazuri wakati ni uongo na hata mungu amewaonya binadamu wanaofanya uchawi kwa kuiga/kumzushia maisha ya mtume suleimani kuwa alitumia majini.

Surat Baqara 102 "wapo wanaotenda uchawi na kukufuru kwa kumzushia nabii suleimani ila uchawi huo umetoka kweny mji wa babeli kutoka kwa haruta na maruti.na hawafunz watu mpk kuwaambia hakika yetu sisi ni mtihani,wanafunza watu uchawi na kufarakanisha.
Kwani tatizo nini, shida nini hasa?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom