Anayefahamu wilaya ya KALAMBO-RUKWA

Anayefahamu wilaya ya KALAMBO-RUKWA

apologize

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2015
Posts
709
Reaction score
570
Habari wakuu, Kuna ndugu yangu kapangiwa huko kikazi naomba kujua mambo haya.
Gharama za usafiri kutoka Dar mpaka Kalambo na unapanda magari yanayoenda wapi?

Hali ya mazingira ikoje hasa kwa miundo mbinu kama maji na umeme

Gharama za gest house zikoje maana hana ndugu wa kufikia

Vyumba vya kupanga gharama zake zikoje?

Na halimashauri kuna umbali gani kutoka bus stand atapotakiwa kuripoti.


Naombeni ushirikiano wenu kwa wenyeji na wote waliopata kuishi au kupita maeneo hayo
 
Dream liner mkuu uliza jiwe, usafiri wa kufika huko, mengine watakwambia washirika
 
Duh! Hizi wilaya nyengine bhana. Yani ndo kwanZa leo nimepata kuisikia hiyo wilaya.
 
kutoka dar mpaka sumbawanga ni Tshs 55,000/= apande New force/golden deer ndo the best, atafika usiku saa 7 mpk saa 8 kuna gest na lodge nyingi ni yeye na mfuko wake kuanzia elfu 10-30. Asubuhi yake atapanda hiace ya kwenda Matai(ndo ilipo halmashauri ya Kalambo) nauli Tshs 2,500/=stand mpk halmashauri sio mbali sana, amwombe msaada konda amshushe halmashauri" mazingira ya kawaida' maji na umeme upo ila inategemea atabaki hapo hapo halmashauri au watampangwa ktk vijiji/kata, gharama kuishi ni za kawaida na vyakula vya kujipikia ni bei cheee.
 
Huyu ndugu yako kama anafanya kazi private na analipwa vizuri mwambie asijaribu kuingia serikalini kwa utawala huu ambapo watumishi wa umma wanaishi kama machokoraaa.....yalinitokea mimi mwaka jana nikaacha kazi sehemu nzuri nikaenda serikalini kilichonitokea sitakuja sahau katika maisha yangu...kufupisha story nilishaachana na kazi ya serikali na nilifanya for six months only
 
kutoka dar mpaka sumbawanga ni Tshs 55,000/= apande New force/golden deer ndo the best, atafika usiku saa 7 mpk saa 8 kuna gest na lodge nyingi ni yeye na mfuko wake kuanzia elfu 10-30. Asubuhi yake atapanda hiace ya kwenda Matai(ndo ilipo halmashauri ya Kalambo) nauli Tshs 2,500/=stand mpk halmashauri sio mbali sana, amwombe msaada konda amshushe halmashauri" mazingira ya kawaida' maji na umeme upo ila inategemea atabaki hapo hapo halmashauri au watampangwa ktk vijiji/kata, gharama kuishi ni za kawaida na vyakula vya kujipikia ni bei cheee.
Shukran mkuu
 
kutoka dar mpaka sumbawanga ni Tshs 55,000/= apande New force/golden deer ndo the best, atafika usiku saa 7 mpk saa 8 kuna gest na lodge nyingi ni yeye na mfuko wake kuanzia elfu 10-30. Asubuhi yake atapanda hiace ya kwenda Matai(ndo ilipo halmashauri ya Kalambo) nauli Tshs 2,500/=stand mpk halmashauri sio mbali sana, amwombe msaada konda amshushe halmashauri" mazingira ya kawaida' maji na umeme upo ila inategemea atabaki hapo hapo halmashauri au watampangwa ktk vijiji/kata, gharama kuishi ni za kawaida na vyakula vya kujipikia ni bei cheee.
Ha ha ha ha wee lelo 1 kwamba anafika saa 7 au 8 usiku
 
Huyo ndugu yako ni CO, MD, LAB-TEC ama nurse mkuu? Kwa ujumla Kalambo ni kuzuri, niwekee namba yake ya sim PM kuna watu wako kule wanaweza mpokea
 
Hana alternative huyo jamaa yako ? Hawezi kuuza hata kitimoto ? Wachawi wa huko noma. Unalala ndani unaamka uko nje na umelowalowa sehemu fulani fulani
 
Watumishi wengi wa kule wanakaa sumbawanga mjini maana kule ndo kumeanza kendelea inshort bado ni mji mdogo sana
 
Back
Top Bottom