habari ya hapa
JF-Expert Member
- Dec 20, 2012
- 12,789
- 8,753
Mabibi na mabwana nawasalimu kwa jina LA Mungu Muumba mbingu na dunia. Km kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu, huyu baba ana mke na watoto wa tano wa mama tofauti tofauti, mke wake wakwanza alifariki namfaham tumetoka kijiji kimoja huko Muheza, huko nyuma niliwahi kusikia anatoka na binti yake siku amini.
Km mwezi umepita nilifiwa na kaka binamu, nikaenda msibani na yy pia alikuja, mida ya jion tulitoka madada na makaka kunyoosha miguu kundi kubwa tu na yeye akiwapo, tulipita kilabuni tukaweka kituo hapo wapenzi wa mnaz, boa, bia waliagiza wakaanza kunywa na story za hapa na pale, me si mnywaji hivyo nilipewa kaz ya kubeba simu.
Wakati tuko pale mwanae alikuwa akimpigia sana simu, anatoka kidogo wanaongea anarudi, baadae tulirudi msibani, tukakuta mziki wa kwaya tukaanza kucheza na yeye akiwapo simu za watu nyingi nilikuwa nazo na yake pia mwanae akampigia tena nikampa wakati huo kishalewa, akamfokea kidogo akanirudishia ile simu, muda kidogo akaondoka kulala, nikabaki na simu yake Mara SMS ikaingia yule binti akimlaumu baba yake kwamba anamfokea bila sababu au nyupo na mwanamke mwingine? Nilishangaa nikapotezea tu, ilikuwa hainiingii akilini, nikafikiri labda kamsevu huyu mchepuko kwa jina na mwanae ili akipiga km yupo na mkewe isiwe tabu.
Kubwa kuliko sasa Leo asubuhi alinipigia nikachukue mzigo Fulani hiv, akanambia alipo nikamfuata, kufika nikamkuta Yupo na binti yake, tukasalisamiliana Hapo, sasa huo mkao binti aloukaa mbele ya babake, na hayo mavazi aliyovaa niliduwaaa, kilichonishangaza zaidi alikuja kijana mmoja akaambiwa aindoke na binti, binti sijui alikuwa hataki bwana weee!!, binti alianza kuongea km kafungiwa mota mdomoni, baba waniambia niondoke wakati safari yetu bado haijaisha, siku hizi umekuwaje lkn?? Km una mwanamke mwingine unambie, nadhani walikuwa wamepishana kabla hata kufika pale, babake aliona aibu sanaa binti karopa vitu mbele ya wageni me na yule kaka alokuja kumchukua, tulivyoona hali si hali tukaondoka, sasa tulipotoka nnje nikamuuliza yule kijana akanipa mkanda wote kwamba pale ni MTU na mpenzi wake na huyo kaka ndo dereva wake japo alikuwa hajui km ni baba na mwana me ndo nilimwambia na Mara nyingi ndo anamchukuaga.
Kwakweli imeniuma sana hiv wanawake wameisha hadi ulale na binti yako??? Aiseeee!! Sitasahau tukio LA leo
Kwa mambo yanoendelea hapa duniani sasa Hiv, ni zaidi ya sodoma na gomoraLaana hiyo
Switi ndo namkuta mume wangu anamwingilia mtoto wetu, nitaenda jelakwa wanaume kichwa cha chini kinawacontrol sana kuliko cha juu..usishangae wala usisikitike ni nyakati za mwisho omba sana na fanya yanayokuhusu.
Sasa hapo unalaumu mwanaume kwanini usimlaumu mwanamke kwanza maana labda alianza kumtega baba yakekwa wanaume kichwa cha chini kinawacontrol sana kuliko cha juu..usishangae wala usisikitike ni nyakati za mwisho omba sana na fanya yanayokuhusu.
Aiseee barikiwa sana huko ulipo kiongozi,Ndiyo ulimwengu huo, la kufanya hapo, wewe kama ni Ke, iombee sana familia yako binafsi utakayokuwa nayo ama uliyonayo tayari (mumeo asije haribu), maana shetani huwa hana hodi, ombea kuanzia kizazi chako kilichopo na vijavyo, ili pepo hilo lisiikute familia yako binafsi. Narudia tena, omba omba omba sana tu. Wapo watakaochangia uzi wako huu na kukuita majina ya ajabu ama hata kukukebehi kwa hilo uliloliona, maana wao kwao kufanya haya ni kawaida sana, utakuta atakayekukebehi, yeye anatoka na mtoto wa dada / kaka yake, awe wa kike / kiume na wanaona sawa, maisha yanaenda. Yooote unayomuomba Mungu akuepushie, ni pamoja na hili, maana naiona hiyo laana katika ukoo wenu, maana kama aliwahi kumuoa dada yako, tayari ukoo ulishaunganika hapo. Pole kwa maelezo marefu, nimejikuta tu nikisikitika na kuhuzunika zaidi. Nasi sote wana jukwaa humu, tuombe kuepushwa na hili.
Ahsante!
Mkuu Ajabu sana hii, sijui wanaitana mpenzi, mume, au inakuwaje sijui, jamii imepotoka kwa kiasi kikubwa sana, mashoga na wasagaji bado mama na mwanae au baba na bintie, niwapi tulipojikwaaa hadi tumefikia huku,Kupenda utajiri wa haraka umekuja na madhara mengi mno na hilo lawezekana likawa moja wapo.....Juzi nilisikia mama mmoja nadhani mikoa ya kusini ameolewa na mtoto wake wa kumzaa kabisa na huyo kijana alikuwa na mke baada ya kuanza na mama ake mzazi akafukuza mke...Na wao hawajifichi wanaishi nyumba moja kitanda kimoja kabisa hafu ukimcheki mama mwenyewe kapigwa na maisha ile mbaya hadi unajiuliza ni nin wanafanya huko kitandani usiku na kijana mwenye nguvu hivyo...So si kwa wanaume tu ni jamii kwa ujumla imepotoka kupita kiasi
kwa wanaume kichwa cha chini kinawacontrol sana kuliko cha juu..usishangae wala usisikitike ni nyakati za mwisho omba sana na fanya yanayokuhusu.
Mkuu mambo ni mengi kuna imani za kishirikina na mambo za kimagharibi tunayoyaiga na tunashindwa jizuia...Mzungu anaweza lala na mtoto wake wa kike mkubwa na still baba akaplay part ya baba mzazi ila wabongo tunaiga hivyo then night unakuta mdingi kaamka anamchek mtoto wake akiwa amelala unasikia anasema ''duh lakini haka katoto kazzuri jaman eeh Mungu nisaidie tu shetani asinishinde" hapo tayar katika ulimwengu wa roho ushazin na mtoto wako na shetani atakula sahani moja na wewe hadi ufurahi cha msingi nikukaa mbali tu na umagharibi maana hatuuwezi kabisaMkuu Ajabu sana hii, sijui wanaitana mpenzi, mume, au inakuwaje sijui, jamii imepotoka kwa kiasi kikubwa sana, mashoga na wasagaji bado mama na mwanae au baba na bintie, niwapi tulipojikwaaa hadi tumefikia huku,