Anataka tuachane na tayari nimekwishalipa mahari kwao na mipango ya ndoa ipo

Watu Huwa mnanichekesha sana nyie!

Unaishi ndoa pika pakua halafu una stress za kufunga ndoa!!

Yaani unafanya ndoa tayari halafu unawaza kufunga doa ambayo tayari unaiishi!!!

Wewe ungeendelea kumzalisha huku ukiona msimamo wake!unahofu ya nini!!?
Jamaa ni mazuu .... hayo tunaita matatizo ya mpumbavu ....ni sawa sawa na zile familia zinazo jali makaburi kuliko maendeleo...wapo tayari kutumia mamilioni kujengea makaburi wakati wao na watoto wao wanaishi kwenye mabanda ya kuku.
 
Hello wanajamvi
Mimi ni kijana wa miaka 30, ninaishi mkoa x kikazi.. nimekuwa na mahusiano na mwanamke kwa muda wa miaka 5 tumekuwa tukiishi pamoja, mwaka jana nilikwenda kwao na kutoa mahali

Mwezi uliopita niliomba likizo moja ya vitu tulivyotarajia kuvifanya kipindi hicho cha likizo ni pamoja na kurudi nyumbani mkoa Y kwa ajili ya kusalimia wazazi na kuweka mipango ya ndoa.
Baada ya kulifikisha swala hili kwa mpenzi wangu yeye aliniomba kuwa aende mara moja kwao mkoa Z kumsalimia bibi yake then baada kama ya siku kama 3 atarudi kuungana na mimi.

Nilimpa ushirikiano wote katika safari yake hiyo pamoja na kufanya shopping, na kumlipia nauli, na kuwa na mipango mingi ya kufanya baada ya yeye kurudi na kuungana na mimi.

Cha kushangaza baada tu ya kufika kwao tu nikaanza kunotice hata pattern ya mawasiliano yamebadilika, hanijulii hali, nikimpigia simu anadai yupo busy. Nikimuuliza atarudi lini hanipi majibu ya uhakika.

Baada ya siku kama nne akanipigia simu kuwa anataka kurudi ila atapitia mkoa T kwa rafiki yake ninayemfahamu before kuja kuungana na mimi na kuniomba nimtumie nauli nikafanya hivyo.

Siku ninayotarajia kuwa atakuwa safarini anakuja kuungana na mimi akanitumia sms kuwa anaumwa sana, baadaye akaniambia kuwa amekosa magari ya kuja huku nilipo, ukimpigia simu hapokei lakini wakati wa jioni nikampata kwenye simu katika kumuuliza kuwa anaendeleaje ana mpango gani na hiyo safari akaniambia kuwa kuna ujumbe amenitumia kwenye simu.. kucheki ule ujumbe alikuwa ameandika kuwa anaona ni wakati umefika wa kumaliza mahusiano yetu.

Hivi sasa hapa nyumbani walikuwa wanamsubiria kwa ajili ya kudiscuss naye kuhusu swala la ndoa na tayari nimekwishalipa mahari kwao.

Hapa nipo kwenye dilema sijui la kufanya nimezungumza na mama yake na yeye anashangaa anajaribu kuwasiliana naye ila hapokei simu zake.

Huyu mpenzi wangu sijawahi kuwa na ugomvi wowote mkubwa tumekuwa tukiishi vizuri tu.
Achana naye usilazimishe huyo hakutaki endelea na mipango yako ya maisha
 
Hello wanajamvi
Mimi ni kijana wa miaka 30, ninaishi mkoa x kikazi.. nimekuwa na mahusiano na mwanamke kwa muda wa miaka 5 tumekuwa tukiishi pamoja, mwaka jana nilikwenda kwao na kutoa mahali

Mwezi uliopita niliomba likizo moja ya vitu tulivyotarajia kuvifanya kipindi hicho cha likizo ni pamoja na kurudi nyumbani mkoa Y kwa ajili ya kusalimia wazazi na kuweka mipango ya ndoa.
Baada ya kulifikisha swala hili kwa mpenzi wangu yeye aliniomba kuwa aende mara moja kwao mkoa Z kumsalimia bibi yake then baada kama ya siku kama 3 atarudi kuungana na mimi.

Nilimpa ushirikiano wote katika safari yake hiyo pamoja na kufanya shopping, na kumlipia nauli, na kuwa na mipango mingi ya kufanya baada ya yeye kurudi na kuungana na mimi.

Cha kushangaza baada tu ya kufika kwao tu nikaanza kunotice hata pattern ya mawasiliano yamebadilika, hanijulii hali, nikimpigia simu anadai yupo busy. Nikimuuliza atarudi lini hanipi majibu ya uhakika.

Baada ya siku kama nne akanipigia simu kuwa anataka kurudi ila atapitia mkoa T kwa rafiki yake ninayemfahamu before kuja kuungana na mimi na kuniomba nimtumie nauli nikafanya hivyo.

Siku ninayotarajia kuwa atakuwa safarini anakuja kuungana na mimi akanitumia sms kuwa anaumwa sana, baadaye akaniambia kuwa amekosa magari ya kuja huku nilipo, ukimpigia simu hapokei lakini wakati wa jioni nikampata kwenye simu katika kumuuliza kuwa anaendeleaje ana mpango gani na hiyo safari akaniambia kuwa kuna ujumbe amenitumia kwenye simu.. kucheki ule ujumbe alikuwa ameandika kuwa anaona ni wakati umefika wa kumaliza mahusiano yetu.

Hivi sasa hapa nyumbani walikuwa wanamsubiria kwa ajili ya kudiscuss naye kuhusu swala la ndoa na tayari nimekwishalipa mahari kwao.

Hapa nipo kwenye dilema sijui la kufanya nimezungumza na mama yake na yeye anashangaa anajaribu kuwasiliana naye ila hapokei simu zake.

Huyu mpenzi wangu sijawahi kuwa na ugomvi wowote mkubwa tumekuwa tukiishi vizuri tu.
Hii imeendaa 😂😂😂 hao viumbe ni matapeli hawana mfano. Kikubwa we jua tu kuwa imeisha hio na huko aliko kwa bibi ni kwa mume mwenzio!
 
Kama wewe ni mtu WA kisasi,mpotezee kausha, tafuta mke mwngine, Wana wake wengi sana wanasaka ndoa, ila utakuja kulipa kisasi siku anafunga ndoa unaweka,kikwazo kuwa ni mchumba wako na mahali ulitoa, bint aolewi.

Pia kama sio mtu WA kisasi, samehe kila kitu kuanzia mahali ad mchumba huyu atakuja anasotea matako kuomba radhi umrudie alipitiwa na shetan
 
Mkuu pole sana! Kuna watu ni wakatiri sana aiseee…Mkuu achana nae kabisa kata mawasiliano naye na usikubali kabisa kusuluhishwa na mtu yeyote kabisa kamwe usikubali huyo mwanamke hakupendi na hakutaki kabisa!
Ila wanawake muda mwingine unaweza usiwaelewe kabisa unaweza kuta anadanganywa na kajamaa wala hakato muoa kabisa na akana mpango kabisa!

Kitakachofata hapo ni wewe kusumbuliwa na huyo binti na watu ili msuluhishwe..kamwe usikubali kuwa na suluhu na mtu aliyekukataaa kwenye hiyo hatua …..usikubali suluhu hiyo kamwe kamwe…tafuta mwanamke mwingine oa huyo achana nae kabisa wala usikubali kukaa kikao nae….
 
Back
Top Bottom